stabilityman
JF-Expert Member
- Jul 9, 2024
- 604
- 1,238
Kijana ukikosa ajira acha kulia lia tafuta biashara uwe unafanya.
Biashara ina hela sana
Biashara ina hela sana
Ingekuwa rahis hivyo wengi wangekuwa wametoka leoKijana ukikosa ajira acha kulia lia tafuta biashara uwe unafanya.
Biashara ina hela sana
Naongea hvo kwa sababu lengo lao weng limeishia kulalamikaHaya ni mawazo ya hovyo, biashara haipaswi kuwa mbadala kwa wakosa ajira bali lengo kuu.
Urahisi au ugumu inategemea na akili yako ulivyoitune.Ingekuwa rahis hivyo wengi wangekuwa wametoka leo
Kila kitu huwa kina maandalizi yake . Nasema hivi kwa sababu ukiangalia asilimia kubwa ya elimu yetu imejikita kwenye kuajiriwa zaidi kuliko kujiajiri. Lakini pia familia nyingi ni maskini kiasi kwamba wanapambana watoto wao wapate elimu angalau waje waajiriwe ili kujikomboa na kuikomboa familia. Biashara inatakiwa maadalizi pia kuanzia namna ya uendeshaji na changamoto kubwa kwa watanzania ni mtaji. Kama nilivyosema familia nyingi ni maskini hivo hata mtaji ni changamoto. Pili biashara huingii kichwa kichwa ni kitu ambacho lazima uwe umefanya tafiti ya kutosha maana hakuna biashara mpya utakayokuja nayo kwa sasa ukajikuta upo peke yako. Mfano mdogo juice sasa hivi kuna wafanyabiashara wakubwa tu na teknolojia zao wanapambana yupo Azam, Mo, Jambo na wengine. Ukisema maziwa kuna Tanga Fresh, Asas . Ukisema mkate Azam humkosi.Hiyo ni mifano midogo tu ambapo kwa mtu ambaye anataka kweli biashara ni kuwa na mtaji mkubwa na utaalamu wa kutosha. Ukisema labda nguo hapo pia mtaji unahitajika lasivyo utakuwa na fremu zenye nguo chcche na hatimaye tozo zikakushinda lipa.Kijana ukikosa ajira acha kulia lia tafuta biashara uwe unafanya.
Biashara ina hela sana
hata hiyo ajira sio rahisi kutoboa.Ingekuwa rahis hivyo wengi wangekuwa wametoka leo
Watanzania wengi tunafeli kwa sababu ya mawazo kama haya.Kumachawa ww biashara utaifanya bila mtaji unadhan wote wanaolalamika ajira hawana mawazo ya kufanya biashara kama mtu hana hata hela ya vocha jero na anaish kwao hiyo biashara anaifanyaje au ndo utaleta porojo za kuwa winga au siyo.
Unatumia mfano WA hao ....ukumbuke wamerithishwa hao yaani utajiri WA kizaziUrahisi au ugumu inategemea na akili yako ulivyoitune.
Kama wakina Bakhresa,Mo na Gsm wangekuwa na mawazo kama yako leo hii pia wangekuwa maskini pia
kingine hela haitafutwi Ina tegwa
Kwa nini na wewe haujarithi ili uwe kama Mo?Najua hapa utanijibu kwamba baba yako hana mali za kukurithisha ambapo tutarudi palepale kwamba ni mtazamo wa kuanzia Mzazi hadi wewe mwenyewe ndio imeleta umaskini.Unatumia mfano WA hao ....ukumbuke wamerithishwa hao yaani utajiri WA kizazi
Hamna tajiri atakwambia ukweli wa mambo.Urahisi au ugumu inategemea na akili yako ulivyoitune.
Kama wakina Bakhresa,Mo na Gsm wangekuwa na mawazo kama yako leo hii pia wangekuwa maskini pia
Kumanini?Kumachawa