Mwingereza
JF-Expert Member
- Jan 21, 2014
- 1,110
- 2,736
Naona Serikali ilifanya kazi nzuri kuyavamia maduka ya fedha za kigeni. Kwa sasa DOLA ya Marekani, Euro pamoja na Pound ya Uingereza inapatikana kwa njia ya magendo tena kwa bei nzuri zaidi ya ile ya madukani (FOREX Black Market). Fedha nyingi sana zinatembea mtaani ambayo inaikosesha serikali mapato makubwa sana.
Jumamosi, nikiwa eneo Fulani maarufu hapa Arusha, jamaa mmoja aliuza kiasi cha $125,000 ndani ya gari. Mimi nilikwa nahitaji $1,300 kwa ajili ya safari yangu Zambia, Mlangoni mwa Bureau De Change, jamaa kanivuta mkono na kuninong’onezea kwamba, hapo utasumbuka.
Piga hii namba, alinipa namba na baada ya kuipiga, haikuchukua muda, kama dakika 6 nilifika sehemu fani na kupata fedha za kigeni kwa bei nafuu.
Bila kunificha, hii biashara ni nzuri mtaani kuliko kwenye maduka. Watu wengi wanauza fedha hizi kimagendo kwa maana wanaona ni usumbufu kwenda kwenye bureau de change.
Naona Serikali imeamua kujikosesha fedha makusudi
Jumamosi, nikiwa eneo Fulani maarufu hapa Arusha, jamaa mmoja aliuza kiasi cha $125,000 ndani ya gari. Mimi nilikwa nahitaji $1,300 kwa ajili ya safari yangu Zambia, Mlangoni mwa Bureau De Change, jamaa kanivuta mkono na kuninong’onezea kwamba, hapo utasumbuka.
Piga hii namba, alinipa namba na baada ya kuipiga, haikuchukua muda, kama dakika 6 nilifika sehemu fani na kupata fedha za kigeni kwa bei nafuu.
Bila kunificha, hii biashara ni nzuri mtaani kuliko kwenye maduka. Watu wengi wanauza fedha hizi kimagendo kwa maana wanaona ni usumbufu kwenda kwenye bureau de change.
Naona Serikali imeamua kujikosesha fedha makusudi