Biashara ambazo huwezi toboa kamwe!

Biashara ambazo huwezi toboa kamwe!

amshapopo

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
2,376
Reaction score
5,372
Hii ni list ya biashara ambazo huwezi toboa kamwe labda upate hela ya kula tu
1; kuuza karanga
2; Machinga
3; Bodaboda
4; Kubet
5; Muuza Chipsi
6; Grocery
7; Kuchoma mahindi - Hadi upate hela ya IST utakuwa umechoka sana!
8; Speculation kwenye hisa kwa pesa ya kuungaunga etc(Hapa wengi sana wamepigwa za uso)

Hizi ni miongoni mwa biashara ambazo kutoboa labda utoboe pua!

NB; Kutoboa maana yake ni kuwa na levo ya maisha standard ie kula chakula kizuri, kuishi sehemu nzuri, kusomesha watoto shule nzuri, usafiri wa kukufikisha sehemu moja na nyingine, kuweza kumudu shida mbalimbali bila kulialia.
 
Ni biashara za kuanzia, kama una muendelezo unaenda hatua ingine kwa kile unachopata kuanzia kwenye hicho kidogo.

Tatizo la mtu kutoendelea ni kukosa nidhamu hata ya kidogo alichonacho
100%, ukweli ni kuwa hakuna biashara moja inayoomfanya mtu atoboe, unaanza na moja kwanza ,the unaenda nyingine hatua kwa hatua
 
100%, ukweli ni kuwa hakuna biashara moja inayoomfanya mtu atoboe, unaanza na moja kwanza ,the unaenda nyingine hatua kwa hatua
Ni kweli kabisa mkuu, na kinachoweza fanya mtu awe na progress ni nidhamu na muendelezo kwenye kile ameanza, changamoto pia ya watu niliyo ona ni ile mtu unaanza mala unaacha unahamia kwingine bila mipangilio
 
Safari ya mafanikio ni mjumuiko wa mambo madogo madogo mengi sana. Mtu anaweza kuanzia kwenye chips akajiongeza na kukuza biashara yake ikakua. Cha muhimu ni nidhamu kwa kile kidogo unachopata. Tatizo mtu akianza kuuza chips labda za 30k kwa siku ataoa, atataka kununua plot na kuanza ujenzi. Mwishowe anaanguka au kuwa mtumwa wa milele wa hizo chips.
 
Shida inaanzia hapo
Safari ya mafanikio ni mjumuiko wa mambo madogo madogo mengi sana. Mtu anaweza kuanzia kwenye chips akajiongeza na kukuza biashara yake ikakua. Cha muhimu ni nidhamu kwa kile kidogo unachopata. Tatizo mtu akianza kuuza chips labda za 30k kwa siku ataoa, atataka kununua plot na kuanza ujenzi. Mwishowe anaanguka au kuwa mtumwa wa milele wa hizo chips.
 
Back
Top Bottom