ADC Party
Member
- Sep 14, 2020
- 28
- 29
Mgombea wa RAIS Jamhuri ya Muungano WA Tanzania Bi Queen Cuthbert Sendiga aliwaambia wananchi wa PEMBA endapo atachaguliwa kuwa Rais wa Tanzania atahakikisha wananchi wa PEMBA watanufaika na zao la karafuu kwa kulipandisha thamani ili liweze kuingiza fedha za kigeni na kuwafanya wananchi hao kuwa na maisha bora na kufurahia kuwepo kwa zao hilo
Aidha mgombea huyo amewaahidi wanachi kuwa atahakikisha wanapatiwa Viwanda vya kusindika samaki ili kuweza kupata ajira za kutosha katika visiwa hivyo, na kuwaondoa wananchi wa Pemba katika lindi la umasikini, hasa wananchi wa Micheweni ambao kwa takwimu za kitaifa inaonesha Wilaya hii ni masikini ya kutupwa hivyo ADC itafanya jitihada Za makusudi kuhakikisha wananchi hao wanindokana na umasikini,
Katika kuhakikisha wananchi wanapata Afya ya kutosha hasa kuepusha vifo vya Mama na mtoto ADC itawekeza katika secta ya Afya kwa upande wa Zanzibar ili kuhakikisha wananchi hao wanaondoka na kuzorota kwa afya zao,
Zaidi amewaasa wanamicheweni na watanzania wote kujihadhari na wanasiasa wanaoleta sera za uvunjifu wa amani,Queen amesema wanasiasa hao waogopwe Kama Corona na amesisitiza kulinda amani ni jukumu la kila mtanzania.
Mgombea huyo anaendelea na kampeni zake kesho katika mkoa wa TANGA
Wilaya ya TANGA, Korogwe, Handeni pamoja na Kilindi
Zanzibar 2020 - Alliance for Democratic Change (ADC) kuzindua Kampeni Kisiwani Pemba kesho Septemba 16, 2020