Yofav
JF-Expert Member
- Mar 12, 2021
- 4,309
- 7,856
Ni kamchezo fulani ambako usipokuwa na displine anguko lako lipo karibu, Sikuelewa wakati nilipomuona mtu anaedai kupoteza kila kitu kwenye kamari, Nilimuona mjinga nikijiuliza "Amepotezaje???"
Kamchezo ambako usipokuwa makini unaweza kujikuta unadundulizia humo kila senti yako unayoona ni ndogo kwa matumaini ya ipo siku utapata nyingi.
Akili inakufanya uhisi kama unachanga fedha kumbe umechanganyikiwa, Na kama huamini pitia bet history ulinganishe hela uliyopoteza na uliyopata ipi nyingi???
Wapo ambao ni njia yao ya kutobolea sikatai ila amini kwamba kama sio njia yako mkuu kuna siku utaongea mwenyewe.
Nilikuwa na utaratibu wa kujifanya na-bet kiasi kidogo ambacho hata nikipoteza siumii, Imeenda kwa zile chache zilizonipa ushindi nilipata relief na kuhisi mimi pia namkanda muhindi, Nikafika muda naweza ku-stake high na bado nikashinda na ikanipa confidance kiasi nikaanza kuwa hata zile high stake siogopi kupoteza.
To be honest zipo nilizoshinda lakini nimepoteza zaidi, Nimekuja kuangukia pua zaidi mwanzoni mwa week iliyoisha, Ghafla bin vuu kila mkeka wangu unachana, Nimechana mfululizo kiasi nikibiga hesabu akili inaniambia nistake high zaidi ili nirudishe hela yangu lakini bado nimepasuka vibaya mno... Katika hali isiyo ya kawaida imenichukua week tu kupuputishwa 3/4 ya akiba yangu.
Kila nikijaribu kurudi duniani ni kama nazidi kuongeza amount of loss... Na hapa naandika nimetoka kulost hela ambayo ilikuwa ya bill ya moja ya service ya nyumbani... What a loss man!!!!? Nimekuwa mjinga sana kuamini kuwa bet inaweza kudouble hela wakati mwanzo nilikuwa nabet nikiweka 90% za kupoteza eti leo naweka 90% za ku-win what a shame!!?
Naacha hii kitu hadi baada ya world cup kuisha nitarudi tena nikiwa na nguvu mpya inshaallah, Muhimu sijapoteza vyote kabisa acha nikubali kwamba kanji kashinda kwa sasa... Me ni muelewa.
Kamchezo ambako usipokuwa makini unaweza kujikuta unadundulizia humo kila senti yako unayoona ni ndogo kwa matumaini ya ipo siku utapata nyingi.
Akili inakufanya uhisi kama unachanga fedha kumbe umechanganyikiwa, Na kama huamini pitia bet history ulinganishe hela uliyopoteza na uliyopata ipi nyingi???
Wapo ambao ni njia yao ya kutobolea sikatai ila amini kwamba kama sio njia yako mkuu kuna siku utaongea mwenyewe.
Nilikuwa na utaratibu wa kujifanya na-bet kiasi kidogo ambacho hata nikipoteza siumii, Imeenda kwa zile chache zilizonipa ushindi nilipata relief na kuhisi mimi pia namkanda muhindi, Nikafika muda naweza ku-stake high na bado nikashinda na ikanipa confidance kiasi nikaanza kuwa hata zile high stake siogopi kupoteza.
To be honest zipo nilizoshinda lakini nimepoteza zaidi, Nimekuja kuangukia pua zaidi mwanzoni mwa week iliyoisha, Ghafla bin vuu kila mkeka wangu unachana, Nimechana mfululizo kiasi nikibiga hesabu akili inaniambia nistake high zaidi ili nirudishe hela yangu lakini bado nimepasuka vibaya mno... Katika hali isiyo ya kawaida imenichukua week tu kupuputishwa 3/4 ya akiba yangu.
Kila nikijaribu kurudi duniani ni kama nazidi kuongeza amount of loss... Na hapa naandika nimetoka kulost hela ambayo ilikuwa ya bill ya moja ya service ya nyumbani... What a loss man!!!!? Nimekuwa mjinga sana kuamini kuwa bet inaweza kudouble hela wakati mwanzo nilikuwa nabet nikiweka 90% za kupoteza eti leo naweka 90% za ku-win what a shame!!?
Naacha hii kitu hadi baada ya world cup kuisha nitarudi tena nikiwa na nguvu mpya inshaallah, Muhimu sijapoteza vyote kabisa acha nikubali kwamba kanji kashinda kwa sasa... Me ni muelewa.