chikakatata
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 220
- 98
NDUGU WANABODI,
Kuna taarifa kwamba Waziri wa Manbo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa Mhe. Bernard Membe ame-engage wanasheria wake dhidi ya Ndg. Hussein Bashe, Kada wa Chama Cha Mapinduzi asiye na wadhifa wowote ule, juu ya kumkashifu na kumuita na kumshambulia kwa maneno makali yasiyo saizi ya heshima aliyonayo Waziri membe. Mhe. Membe ameamua kumburuza kortini Ndg Bashe mnamo siku ya Jumatatu ijayo, kwa mujibu ya jopo la wanasheria wake watatu maarufu na mahiri. Ndg. Bashe, siku moja kabla ya Mkutano Mkuu wa Nane Dodoma alituita waandishi wa habari na kutueleza kuwa "...Membe hafai hata kupewa ubalozi wa nyumba kumi kwa kuwa ni muongo, mnafiki na amezoea kuishi kwa kubebwa..."
Itakumbukwa Mhe Membe alikuwa ni mgombea maarufu na mahsusi wa U-NEC wajumbe kumi na akina Bashe na Lowassa walikuwa kwenye jitihada za hali ya juu kuhonga pesa ili asipite katika kinyang'anyiro kile sambamba na uhamasishaji mkubwa waliokuwa wakiufanya pia kutaka Rais JK ambaye pia alikuwa ni mgombea wa Kiti Taifa cha CCM apate kura za Hapana ili kumuaibisha, ikiwa ni pamoja na hoja ya Hussein Bashe na kundi lake kutaka Uenyekiti wa CCM utenganishwe na U-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkutano huu baina ya waandishi wa habari na Ndg Bashe ulichukuliwa kama sehemu ya mkakati madhubuti wa kutaka kuhakikisha Membe anaaibika na anashindwa uchaguzi ule ili kumkatisha tamaa na kumshusha hadhi kama mgombea Urais haswa ukizingatia kuwa Mkutano Mkuu ule ndiyo utakaopitisha jina la mgombea wa Urais wa CCM 2015; kinyume na mipango na fitna zao, pamoja na hela walizohonga aliibuka kidedea akishika nafasi ya sita bila kutoa hongo wala kuzunguka mikoani kutafuta kura, jambo ambalo liliwashangaza sana wanaCCM na wanahabari wengi waliokuwepo Mkutanoni pale - hali ambayo ilidhihirisha kuwa Membe ana umaarufu wa kutosha kushinda URais huku akigombea kwa kufuata misingi yote ya uadilifu. Pia ikizingatiwa kuwa mshindani wake mkubwa Mhe Lowassa aliliogopa kundi la kifo la NEC na kwenda kugombea UNEC jimboni kwake Monduli.
Kuna taarifa kwamba Waziri wa Manbo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa Mhe. Bernard Membe ame-engage wanasheria wake dhidi ya Ndg. Hussein Bashe, Kada wa Chama Cha Mapinduzi asiye na wadhifa wowote ule, juu ya kumkashifu na kumuita na kumshambulia kwa maneno makali yasiyo saizi ya heshima aliyonayo Waziri membe. Mhe. Membe ameamua kumburuza kortini Ndg Bashe mnamo siku ya Jumatatu ijayo, kwa mujibu ya jopo la wanasheria wake watatu maarufu na mahiri. Ndg. Bashe, siku moja kabla ya Mkutano Mkuu wa Nane Dodoma alituita waandishi wa habari na kutueleza kuwa "...Membe hafai hata kupewa ubalozi wa nyumba kumi kwa kuwa ni muongo, mnafiki na amezoea kuishi kwa kubebwa..."
Itakumbukwa Mhe Membe alikuwa ni mgombea maarufu na mahsusi wa U-NEC wajumbe kumi na akina Bashe na Lowassa walikuwa kwenye jitihada za hali ya juu kuhonga pesa ili asipite katika kinyang'anyiro kile sambamba na uhamasishaji mkubwa waliokuwa wakiufanya pia kutaka Rais JK ambaye pia alikuwa ni mgombea wa Kiti Taifa cha CCM apate kura za Hapana ili kumuaibisha, ikiwa ni pamoja na hoja ya Hussein Bashe na kundi lake kutaka Uenyekiti wa CCM utenganishwe na U-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkutano huu baina ya waandishi wa habari na Ndg Bashe ulichukuliwa kama sehemu ya mkakati madhubuti wa kutaka kuhakikisha Membe anaaibika na anashindwa uchaguzi ule ili kumkatisha tamaa na kumshusha hadhi kama mgombea Urais haswa ukizingatia kuwa Mkutano Mkuu ule ndiyo utakaopitisha jina la mgombea wa Urais wa CCM 2015; kinyume na mipango na fitna zao, pamoja na hela walizohonga aliibuka kidedea akishika nafasi ya sita bila kutoa hongo wala kuzunguka mikoani kutafuta kura, jambo ambalo liliwashangaza sana wanaCCM na wanahabari wengi waliokuwepo Mkutanoni pale - hali ambayo ilidhihirisha kuwa Membe ana umaarufu wa kutosha kushinda URais huku akigombea kwa kufuata misingi yote ya uadilifu. Pia ikizingatiwa kuwa mshindani wake mkubwa Mhe Lowassa aliliogopa kundi la kifo la NEC na kwenda kugombea UNEC jimboni kwake Monduli.