Bernard Membe, kama basi limekuacha chukua pikipiki ufike

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,749
21,202
Siwezi kusema kauli ya Father of The Nation Mwl. JKN kuwa mpinzani wa kweli atatoka ndani ya CCM, maana hata wakati wa Edo kauli hii ilitamkwa sana na kuaminisha umma kuwa sasa siasa ya Tanzania imepata uhalisia.

CCM ni chama chenye mizizi iliyosambaa sana kiasi ukichimba juu juu huwezi kuiona na unaweza kusema huu mti utakufa mbona unaishi pasipo mbolea hahahaaaa.

Hapana/Ndiyo kwa mtizamo unaoweza kuwa nao, hapa tunakutana na safari nyingine ya kisiasa ambayo kila uchaguzi mkuu unapokaribia visa vya aina hii huwa haviishi kabisa toka jemedari JKM alipokuwepo ukikumbuka wakati wa kambona mpaka yule jamaa aliyetaka kuanzisha jeshi la msituni ili kumng'oa Julius.

Leo tunaye (kitengo mbobezi au lijendari) Bernard Camilius Membe, jamaa anaonyesha nia adhimu ambayo naweza kusema inaleta chachu kuufikia uchaguzi wa mwaka huu kupitia (chama babu) CCM ambapo kwa uharisia hawezi kupenya kwa vyovyote na njia yoyote.

Hapa anakwambia "Unaweza kwenda Dar es Salaam kwa basi, kama basi limekuacha chukua pikipiki utafika"

Lakini anakwambia, "ningekupa majina yote sita ya vigogo wanaoniunga mkono"

Hebu mfuatilie kwenye mahojiano hayo nimekuwekea hapo.
 

Attachments

  • Mahojiano ya Membe.mp3
    3.5 MB · Views: 2
Ili ni suala muhimu ambalo hata waliopo kwenye system sasa walitafakari . Akiwepo mpinzani wa Dr wa udsm.
 
Afrika mfumo ukishakutupa huna chako hata kina jiwe atakuja mwingine atawanyoosha kwa katiba hii hii japo Sasa ni vipofu Kama walivokuwa kina membe, Lowasa, Mkapa,sumaye.
Ni sawa na mwanasheria kutunga Sheria Kandamizi akiwa huru kesho ni mfungwa kwa Sheria ile ile aliyoitunga
 
Afrika mfumo ukishakutupa huna chako hata kina jiwe atakuja mwingine atawanyoosha kwa katiba hii hii japo Sasa ni vipofu Kama walivokuwa kina membe, Lowasa, Mkapa,sumaye.
Ni sawa na mwanasheria kutunga Sheria Kandamizi akiwa huru kesho ni mfungwa kwa Sheria ile ile aliyoitunga
Sawa na hii ndiyo ile tunayosema haki inabaki kwa wenye maamuzi, kuna kitu unaweza kuwaza juu ya mfumo wa siasa na hatima ya maisha ya raia wa kawaida.

Sheria inakulinda ukiwa unaisimamia ndipo hapa tunaona hata hawa kina Mbowe nk wanasema katiba, katiba, katiba, hapana wakiingia kwenye lile jumba hawawezi kubadirisha.

Maana itakuwa inawalinda na hawawezi kutufanya raia tuunde katiba kama ile ya jaji Warioba ambayo wanajua inambana mmojawapo na kumtupa nje ya ulingo.
 
Back
Top Bottom