Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 254
- 892
Habari zenu wakuu.
Natumaini wote mko salama hapa. Leo nimekuja na malalamiko juu ya wafanyakazi wa benki ya NMB tawi la Mafinga mjini.
Wafanyakazi wa benki hii wanadharau sana wateja, hasa wale waliopo katika dawati la customer care.
Jana tarehe 22/1/2020 nimeenda kuchukua ATM card yangu, nikamkuta mama mmoja yupo pale, nikamwambia shida yangu. Akaniambia nisubiri. Basi nilisimama saa tatu nikisubiri achezee kompyuta yake ili anipatie kadi yangu ambayo ilikuwa kando tu na alipokuwa.
Nilisimama saa hizo na kadi sikuipata. Mwishowe nikaondoka kwa hasira.
Jamani, mpo hapo kwa ajili yetu. Sisi ndio tunaowafanya mlipwe mishahara hapo. Kama mimi ni mteja mkubwa wa benki yenu. Basi tupeni thamani yetu kama wateja.
Msitunyanyase.
Nawasilisha.
Naitwa Six Man.
Sent using Jamii Forums mobile app
Natumaini wote mko salama hapa. Leo nimekuja na malalamiko juu ya wafanyakazi wa benki ya NMB tawi la Mafinga mjini.
Wafanyakazi wa benki hii wanadharau sana wateja, hasa wale waliopo katika dawati la customer care.
Jana tarehe 22/1/2020 nimeenda kuchukua ATM card yangu, nikamkuta mama mmoja yupo pale, nikamwambia shida yangu. Akaniambia nisubiri. Basi nilisimama saa tatu nikisubiri achezee kompyuta yake ili anipatie kadi yangu ambayo ilikuwa kando tu na alipokuwa.
Nilisimama saa hizo na kadi sikuipata. Mwishowe nikaondoka kwa hasira.
Jamani, mpo hapo kwa ajili yetu. Sisi ndio tunaowafanya mlipwe mishahara hapo. Kama mimi ni mteja mkubwa wa benki yenu. Basi tupeni thamani yetu kama wateja.
Msitunyanyase.
Nawasilisha.
Naitwa Six Man.
Sent using Jamii Forums mobile app