msambaa mwenyewe
Member
- Aug 17, 2016
- 69
- 45
Umetwacha na fadhaa Ben mwana wa Saanane
Fokasi yako ni taa, Ya usiku wa manane
Fesibuku unang’aa, Mithili ya manemane
Mlete wetu shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hupimiki kwa dhiraa Si mnyama ulingane
Mizani inakataa, Faru Joni mianane
Hata ukijaza paa , Makumi elfu nane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Sasa ni siku kadhaa, bila Ben Saanane
Mitandao imejaa simanzi bila Saanane
Nimakini si kichaa, bila hoja apambane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hawezi zimika waa ! eti asionekane
Sio kama mshumaa, msitake tubishane
Mtachochea balaa, mapema tuelewane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Mwachieni bila waa, uwanja wa nanenane
Tutakuja kumtwaa, hata usiku Saanane
Mkizidi kukomaa, tutakuja tupigane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hoja zake ni makaa, yenye moto mwanawane
Shuti zake ni balaa, kama zile za Zidane
Mahasimu waduwaa, utadhani masenene
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Kimya sisi tumekaa, leo kwa Ben Saanane
Kesho nani wamtwaa? Kizani wakambane
Hasira yazidi jaa, msitake tubanane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Nasepa nikitambaa, wanakuja wanibane
Mwaona mi shujaa? nisubiri tupambane?
Mie sitaki balaa , namtafuta Saanane
Tunamtaka shujaa, Ben Rabiu Saanane
Fokasi yako ni taa, Ya usiku wa manane
Fesibuku unang’aa, Mithili ya manemane
Mlete wetu shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hupimiki kwa dhiraa Si mnyama ulingane
Mizani inakataa, Faru Joni mianane
Hata ukijaza paa , Makumi elfu nane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Sasa ni siku kadhaa, bila Ben Saanane
Mitandao imejaa simanzi bila Saanane
Nimakini si kichaa, bila hoja apambane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hawezi zimika waa ! eti asionekane
Sio kama mshumaa, msitake tubishane
Mtachochea balaa, mapema tuelewane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Mwachieni bila waa, uwanja wa nanenane
Tutakuja kumtwaa, hata usiku Saanane
Mkizidi kukomaa, tutakuja tupigane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Hoja zake ni makaa, yenye moto mwanawane
Shuti zake ni balaa, kama zile za Zidane
Mahasimu waduwaa, utadhani masenene
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Kimya sisi tumekaa, leo kwa Ben Saanane
Kesho nani wamtwaa? Kizani wakambane
Hasira yazidi jaa, msitake tubanane
Tunamtaka shujaa, Ben mwana wa Saanane
Nasepa nikitambaa, wanakuja wanibane
Mwaona mi shujaa? nisubiri tupambane?
Mie sitaki balaa , namtafuta Saanane
Tunamtaka shujaa, Ben Rabiu Saanane