Randy orton
JF-Expert Member
- Apr 29, 2019
- 1,338
- 3,541
Nafahamu kwamba huu mchakato wa kupandisha gharama za vifurushi ulianza tangia zamani, nafahamu pia moja ya mbinu za kisiasa ni kutengeneza tatizo na kulitatua mwenyewe hata kama ulikuwepo kwenye jopo la waliofanya maamuzi kufikia kupatikana kwa tatizo hilo.
Serikali ina kiongozi mpya ambaye pamoja na yote lazima aonyeshe amesimama upande wa watu wengi wanaolalamika kwa upandaji holela wa vifurushi ambao sio tuu utainyima serikali mapato bali utarudisha watu nyuma kutoka katika matumizi ya TEHAMA , kwa maana nyingine atajitenga na maamuzi ya kupandisha vifurushi.
Hivyo natabiri kuwa kuna vichwa vinaenda kuliwa pale TCRA na Wizara ya mawasiliano, maboss wote wanaohusika na haya maamuzi wajiandae, hii pasaka itakuwa pasaka yao ya mwisho kama maboss au viongozi wa sehemu husika..
Kama ni wajanja wachukue hatua za mapema sana kuonyesha wamesimama upande wa watu ili waokoe nafasi zao za kisiasa, kwani atakayeliwa kichwa hapa ndio atakuwa amekufa kisiasa na kiutumishi.
Serikali ina kiongozi mpya ambaye pamoja na yote lazima aonyeshe amesimama upande wa watu wengi wanaolalamika kwa upandaji holela wa vifurushi ambao sio tuu utainyima serikali mapato bali utarudisha watu nyuma kutoka katika matumizi ya TEHAMA , kwa maana nyingine atajitenga na maamuzi ya kupandisha vifurushi.
Hivyo natabiri kuwa kuna vichwa vinaenda kuliwa pale TCRA na Wizara ya mawasiliano, maboss wote wanaohusika na haya maamuzi wajiandae, hii pasaka itakuwa pasaka yao ya mwisho kama maboss au viongozi wa sehemu husika..
Kama ni wajanja wachukue hatua za mapema sana kuonyesha wamesimama upande wa watu ili waokoe nafasi zao za kisiasa, kwani atakayeliwa kichwa hapa ndio atakuwa amekufa kisiasa na kiutumishi.