Bei ya unga wa Sembe yapanda, Serikali iingilie kati

Bei ya unga wa Sembe yapanda, Serikali iingilie kati

Natoa tu angalizo kwa katibu wa idara ya uchumi ya chama changu CCM, huku mtaani bei ya Unga wa Ugali ( Sembe na Dona) ni kati ya sh 1500 hadi 1700 kwa kilo.

Ikumbukwe kuwa mahindi yamevunwa juzikati tu sasa ikifika February 2020 sijui hali itakuwaje?

Serikali itoe ruzuku kwa wakulima wa mahindi ili kuwasaidia na kumpa nafuu mwananchi wa kawaida.

Watanzania Ugali ndio mkate wetu wa kila siku

Maendeleo hayana vyama!
Tatizo wabongo tumezoea lawama. Serikali ilipopiga marufuku mahindi kuuzwa nje ya nchi watu walilalamika.
Sasa wameruhusiwa matokeo ndio haya.
Mi nazani ifike kipindi kila mwananchi walau awe na kashamba walau nusu heka.
Wakulima wanaonewa Sana! Gharama za kilimo Ni kubwa Sana na anazibeba mkulima mwenyewe, ikifikia kipindi cha mavuno wasiogharamia chochote wanampangia mkulima bei ya kuuza.
 
Dah..afadhali...na upande au uadimike au upotee kabisa...
"ugali hufanya ubongo kuwa mzito" - utafiti
 
Kama mahindi yalipatikana kwa wingi msimu uliopita na wakulima wana ziada, mwelekeo ni kuuza nje ya nchi kwa bei ya juu zaidi ya ile ya ndani!.

Wakulima wamechagua kuuza nje ya nchi na hivyo kunufaika kimapato, kama utapenda kununua mahindi ya mkulima ni lazima uyanunue kwa bei ya nje ya nchi.

Suruhisho ni kununua mazao mbadala kama mchele viazi na mtama, Au kuwazuia wakulima wasiuze mahindi nje ya nchi.

Uwazie kuuza nje ili wapate hasara?

Limeni nyinyi muuze bei rahisi.
 
Uwazie kuuza nje ili wapate hasara?

Limeni nyinyi muuze bei rahisi.
Arawaaa!... Soma kwa makini bandiko langu uone kama ulichoandika hapo juu kina tofauti na nilichoandika mimi, anzia mstari wa kwanza tu.... 😳 😳

Uwazie= Uwazuie .... nadhani una maana hiyo.
 
Acha kulialia, nenda kalime uone mziki wake... acheni wakulima wanufaike.
 
Kweli wewe huelewi!
Mimi nilidhani ni mtu mkubwa na cheo chake kwenye chama cha CCM kumbe ni mngangaa njaa tu. Hiyo ni pesa ndogo sana, tena napenda tununue unga wa sembe kilo moja 5,000 ili wakulima nao wafaidike. Kilimo ni kazi ngumu sana kwahiyo acha nao wapate faida.
"Ukiona mtu analia maisha magumu ujue alikuwa mpiga dili by CCM"
 
Pale Vijana wa Lumumba wanapochukua nafasi ya Dr abbas.
 
Back
Top Bottom