Nyie wote bado madogo sana mimi nilinunua soda kwa senti 70 mwaka gani sijui nishasahau.
Teh teh teh teh
Japo sio ya kucheka imenilazimu kucheka.
Nakumbuka wakati nasoma Primary, Ada ya mwaka mzima ilikuwa Sh. 100. Lakini cha ajabu kuna mwaka eti nilirudishwa nyumbani sijalipa ada, Sh. 100? nikikumbuka ninachofanyia Sh. 100 sasa hivi na nilivyorudishwa nyumbani kwa kukosa mia hiyo hiyo enzi nasoma, nasikitika sana jinsi maisha yalivyopanda.
Shs 100 ya siku hizi imechakachuliwa sana. ya wakati ule kwanza ilikuwa ni noti. tena hapo unahesabu noti za sh. kumi kumi zikifika kumi moja unakunjiaTeh teh teh teh
Japo sio ya kucheka imenilazimu kucheka.
Nakumbuka wakati nasoma Primary, Ada ya mwaka mzima ilikuwa Sh. 100. Lakini cha ajabu kuna mwaka eti nilirudishwa nyumbani sijalipa ada, Sh. 100? nikikumbuka ninachofanyia Sh. 100 sasa hivi na nilivyorudishwa nyumbani kwa kukosa mia hiyo hiyo enzi nasoma, nasikitika sana jinsi maisha yalivyopanda.
Wakati nasoma UDSM miaka ya mwanzo ya 80 soda ilikuwa sh. 1, kama nakumbuka vizuri. Wakati huo USD ilikuwa ni sh. tano za Kitanzania, na mabasi ya binafsi yaliporuhusiwa kubeba abiria Dar, yalikuwa yanatoza sh. tano na ndio neno dala dala likatokea hapo maana wapiga debe walikuwa wanasema 'panda hapa, dala dala tu'!