Behind the curtain: September 11

hii mbona ipo kwenye mitandao mingi tu sema labda kwa sababu ya lugha inawapa shida.uyu jamaa labda tumwite mkalimani

Wewe mbona ujaanzisha thread umutafsirie bibi ako kule kolomije tatzo lako kuzaliwa njiti na kubemendwa pia kulelewa na bibi ndio kinachokusumbua mlamba vumbi
 
The bold we ni changamotto sana mzee. Mi napenda sana maswala ya Intelligencia, Nakuomba ukishusha mzigo mpy unitag please. Najua hata movie/series huwa unaangalia vitu vitamutamu kama hivi mzee, nipe majina ya movie ama series boss wangu
 
The bold we ni changamotto sana mzee. Mi napenda sana maswala ya Intelligencia, Nakuomba ukishusha mzigo mpy unitag please. Najua hata movie/series huwa unaangalia vitu vitamutamu kama hivi mzee, nipe majina ya movie ama series boss wangu

same here
 
Huu uzi leo ndo nimeusoma,ukweli nimejikuta nasoma had sehem ya mwisho.Sijawah kwenda Amerika,sijawah kwenda nchi yeyote wala sijawah kwea ndege ila The bold amenipandisha ndege amenipeleka German,USA,AFGHAN,Pakistan na kwingineko,anajua kusimulia.
TAG BE BRO WA DARK CITY
 
Mkuu The bold niliuliza maswali yangu post no. 910 naona hukuweza kuyajibu, na swali la nyongeza ni kuwa siku ya tukio umeelezea kuna ndege ya kijeshi iliombwa kuifuatilia ndege moja wapo ya hizo zilizohusika, madhumuni ya ndege hiyo yalikuwa nini? Kuiokoa au kuiangamiza?
 
The Bold, mkuu wangu na role model wangu, kipaji chako cha kufuatilia, kutafiti, kuchambua, kutathmini, kujumuisha na ku wasilisha ni zaidi ya kipaji cha kawaida hasa kwa hoja kwamba kipaji hicho kimejumuisha vipaji vingine ambavyo si kawaida kuwa pamoja. Kwamba wewe unavyo pamoja (kwa maoni yangu) ni sawa na mfano wa kukuta shimo moja la madini lina almasi, dhahabu, ruby, uranium, nk.

Watu waliobahatika kuwa na kipaji cha namna hii ni watu walio bahatika kuwa na jumuiya njema kabisa ya vipaji. Wapo na wewe ni mmoja wao. Ni package inayofaa sana kwa Dunia tunayo ishi.

Kwa namna inayo shawishi utafiti watu wa namna hii pia wanaweza kuwa wahanga wa kipaji husika. Kwa ruksa, niruhusu kugusia baadhi ya changamoto zinazo weza kumkabili mtu mwenye kipaji cha aina yako.

Tahadhari: sina taaluma yeyote ya psychology wala mfanano wa hilo:

1. Kuwa muhanga wa kukosa mfanano. Yaani mtu mwenye kipaji cha kufanana nawe anaweza kuishi pweke hasa kwenye maisha ya kipaji chake. Mfano mzuri wa hili ni upweke wa maumbo mbalimbali kwenye universe. Yaani, kila akijaribu kutafuta wa kufanana naye analazimika kuishia kwenye tumaini kwamba yupo ila kwa wakati huo hamfahamu. Changamoto hii ingawa ni hasi ikikomaa huzaa tunda ambalo kwa kushangaza na kwa maoni yangu ni positive. Mhanga hufikia wakati wa kukubali kwamba hadi wakati huo atakapo pata mfanano anatakiwa kufananisha kipaji chake na watu wanao miliki sehemu tu ya kipaji chake. Mfano, mtu huyo hujenga urafiki na watafiti wasio wachambuzi, wachambuzi wasio wawasilishi nk. Madhara ya tunda hili kwa mhusika ni kuishi kwenye dunia yake lakini kwa kushirikiana na dunia fikirishi ya wengine.

2. Hamu ya kutafuta mfanano. Mtu mwenye kipaji cha namna hii huwa pia ni Mhanga wa kutafuta mfanano. Hoja hii kwa kiasi hufanana na hoja ya kwanza. Hatahivyo inatofautiana na hoja ya kwanza kwa msingi kwamba kama mwenye kipaji husika asipokuwa makini anaweza kuwa muhanga wa matarajio ya kupata mfanano wa wenye sehemu tu ya kipaji chake. Kuweka maneno vyema na kwa kuzingatia mfano wa mchimbaji wa madini, mtu huyu anaweza kutamani kuchimba madini kwenye shimo lake ila akaona inafaa kutoonesha kwamba shimo lake linatoa madini mengine mbali na madini yanayo shabikiwa na wachimbaji wengine!.

3. Mtafaruku wa kukidhi mahitaji ya wafuasi wanao hitaji zaidi ya matunda ya kipaji. Kipaji tajwa cha mhusika chaweza kwa kiwango kikubwa kuridhisha umma wenye sehemu tu ya kipaji hicho. Hatahivyo hili haliondoi uwezekano wa baadhi ya wafuatiliaji kujaribu na hasa kupenda package ya kipaji cha mhusika igusie vipaji vingine. Huu huwa ni mtihani sana kwa mwenye kipaji tajwa.

4. Vyovyote vile iwavyo, ujumbe wangu ni kusema: "the Bold wewe unakipaji adimu, mimi nakufuatilia kwa sababu ya kipaji chako, ni imani yangu kwamba utafika mbali sana. MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU ZAIDI".
 
The Bold, mkuu wangu na role model wangu, kipaji chako cha kufuatilia, kutafiti, kuchambua, kutathmini, kujumuisha na ku wasilisha ni zaidi ya kipaji cha kawaida hasa kwa hoja kwamba kipaji hicho kimejumuisha vipaji vingine ambavyo si kawaida kuwa pamoja. Kwamba wewe unavyo pamoja (kwa maoni yangu) ni sawa na mfano wa kukuta shimo moja la madini lina almasi, dhahabu, ruby, uranium, nk.

Watu waliobahatika kuwa na kipaji cha namna hii ni watu walio bahatika kuwa na jumuiya njema kabisa ya vipaji. Wapo na wewe ni mmoja wao. Ni package inayofaa sana kwa Dunia tunayo ishi.

Kwa namna inayo shawishi utafiti watu wa namna hii pia wanaweza kuwa wahanga wa kipaji husika. Kwa ruksa, niruhusu kugusia baadhi ya changamoto zinazo weza kumkabili mtu mwenye kipaji cha aina yako.

Tahadhari: sina taaluma yeyote ya psychology wala mfanano wa hilo:

1. Kuwa muhanga wa kukosa mfanano. Yaani mtu mwenye kipaji cha kufanana nawe anaweza kuishi pweke hasa kwenye maisha ya kipaji chake. Mfano mzuri wa hili ni upweke wa maumbo mbalimbali kwenye universe. Yaani, kila akijaribu kutafuta wa kufanana naye analazimika kuishia kwenye tumaini kwamba yupo ila kwa wakati huo hamfahamu. Changamoto hii ingawa ni hasi ikikomaa huzaa tunda ambalo kwa kushangaza na kwa maoni yangu ni positive. Mhanga hufikia wakati wa kukubali kwamba hadi wakati huo atakapo pata mfanano anatakiwa kufananisha kipaji chake na watu wanao miliki sehemu tu ya kipaji chake. Mfano, mtu huyo hujenga urafiki na watafiti wasio wachambuzi, wachambuzi wasio wawasilishi nk. Madhara ya tunda hili kwa mhusika ni kuishi kwenye dunia yake lakini kwa kushirikiana na dunia fikirishi ya wengine.

2. Hamu ya kutafuta mfanano. Mtu mwenye kipaji cha namna hii huwa pia ni Mhanga wa kutafuta mfanano. Hoja hii kwa kiasi hufanana na hoja ya kwanza. Hatahivyo inatofautiana na hoja ya kwanza kwa msingi kwamba kama mwenye kipaji husika asipokuwa makini anaweza kuwa muhanga wa matarajio ya kupata mfanano wa wenye sehemu tu ya kipaji chake. Kuweka maneno vyema na kwa kuzingatia mfano wa mchimbaji wa madini, mtu huyu anaweza kutamani kuchimba madini kwenye shimo lake ila akaona inafaa kutoonesha kwamba shimo lake linatoa madini mengine mbali na madini yanayo shabikiwa na wachimbaji wengine!.

3. Mtafaruku wa kukidhi mahitaji ya wafuasi wanao hitaji zaidi ya matunda ya kipaji. Kipaji tajwa cha mhusika chaweza kwa kiwango kikubwa kuridhisha umma wenye sehemu tu ya kipaji hicho. Hatahivyo hili haliondoi uwezekano wa baadhi ya wafuatiliaji kujaribu na hasa kupenda package ya kipaji cha mhusika igusie vipaji vingine. Huu huwa ni mtihani sana kwa mwenye kipaji tajwa.

4. Vyovyote vile iwavyo, ujumbe wangu ni kusema: "the Bold wewe unakipaji adimu, mimi nakufuatilia kwa sababu ya kipaji chako, ni imani yangu kwamba utafika mbali sana. MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU ZAIDI".
Mkuu George Dalali,

Usione nimekaa kimya siku ya tatu hii bila kujibu hii Comment, ni vile tu kuna muda mtu unajikuta uko speechless... Unaishiwa neno lolote la kusema! Ndivyo ambavyo nimeshindwa kwa siku tatu nijibu vipi..

Kwanza niseme kwamba umenigusa moyo kabisa na katika uhalisia hasa hapo ulipoandika kuhusu muda mwingine kuwa "muhanga wa kipaji"! Umenena jambo halisi na sahihi 100% ni kitu ambacho kinanikabili kila Leo...

Lakini zaidi niseme kwamba nashukuru sana sana kwa pongezi na kunitia moyo namna hii..

Ni watu kama wewe ndio mnanifanya niandike kila siku... Hata pale ninapopitia ugumu, au changamoto au vita fulani... lakini nikikumbuka kuwa mpo watu mnaoburudika na maandishi yangu, mpo watu mnajifunza kitu kwenye maandishi yangu na labda wako wanaotiwa moyo kupitia maandishi yangu, basi nasahau ugumu na changamoto zote na nainua kalamu na kuandika...

Nathamini sana hiki ulichokisema! Na umenitia moyo sana...

Ubarikiwe sana mkuu! Shukrani
 
kila neno ninalofikiri kulitoa naona halifai. Labda niseme tu, Shikamoo The Bold!! Fikiria kuandika vitabu, uweke kama riwaya ili kuepusha wafitini na wenye roho mbaya wa nchi hii kukudisturbalize. Jazakharah khair!!
 
Hili swala la september 11 lina wajuaji wengi sana...hasa wenye ngozi nyeusi hujifanya wanalijua sana....mtu anakrupuka tu anacopy copy na kupaste vitu toka mtandaoni...haya mambo nenda VATICAN ndo utayaelewa...maskini Osama aliwekwa chambo bila kujua effect yake...kumbe watu wana mipango yao
 
kila neno ninalofikiri kulitoa naona halifai. Labda niseme tu, Shikamoo The Bold!! Fikiria kuandika vitabu, uweke kama riwaya ili kuepusha wafitini na wenye roho mbaya wa nchi hii kukudisturbalize. Jazakharah khair!!
Shukrani sana mkuu!

Tuko pamoja sana..
 
Back
Top Bottom