Manyerere,
Kuna mengi ningeweza kusema...
Prof. Hirji kaandika baada ya mimi kusema.
Alikuwa wapi siku zote?
Mimi huna haja ya kunihimiza.
Siku zote nimekuwapo.
Ningependa kutoa historia fupi ya kibinafsi
Mwaka 1969: Mimi, Karim Hirji, nilikuwa Mhariri Mkuu wa jarida la wanafunzi wa UDSM
liitwalo CHECHE. Tuliunga mkono siasa ya ujamaa lakini tulisema ukweli kuwa utekelezaji
wake na TANU ilikuwa mbaya sana. Wazee wa TANU walikasirika sana na Jarida letu ilpigwa
MARUFUKU.
Mwaka 1973:Niliandika makala kukosoa sera ya Mwalimu Nyerere kuhusu elimu ya kujitegemea
iliochapishwa UDSM kwenye jarida la Maji Maji Nilionyesha utekelezaji wake shuleni ilikuwa una
mapungufu mengi. Wakati ule nilikuwa Assitant Lecturer wa Mathematics. Mwalimu alikasirika
na mimi nilifukuzwa UDSM na nilipelekwa SUMBAWANGA.
Mwaka 1979: Niliandika chapter kwenye kitabu A HISTORY OF COLONIAL TANGANYIKA kuhusu
sera za wajaremani ya elimu na niligusia suala la dini pia.
Na kuna mengi zaidi. Watu wengi wana sema mambo ambayo kwa wakati ule walikaa kimya.
Mmi nili sema ukweli wazi wazi na nilipewa adhabu kali.
Ndugu Saidi mimi pia nina historia ndefu ya kuandika mambo ya social historical analysis.
Na wewe pia una historia ndefu ya kufanya hivyo. Lakini mimi sisemi kwa wengine
nyinyi mlikuwa wapi wakati wote huu.
Kuuliza swali kama hilo ni a diversionary tactic. Hai fai hata kidogo. Leo wewe na mimi
tumekutana kwenye majadiliano ya mambo muhimu kwenye nchi yetu. Tujaribu kujibu
hoja kwa hoja, wazo kwa wazo, na siyo kuuliza ULIKUWA WAPI? Kila mtu ana haki ya
kujiingiza katika mjadiliano yeyote wakati wowote.
Prof. Karim Hirji