BBC waianika Tanzania tena!

BBC waianika Tanzania tena!

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,461
Baada ya kufanikiwa kwenye pembe za ndovu, BBC wametukung'uta tena. Safari hii ni kwenye madini ya tanzanite. Wanadai tanzanite inachimbwa na watoto. Wameweka video ya "the gemstone mined by child labour". Huu utakuwa ni mkakati wa makaburu wa tanzaniteone ambao mara zote wameutangazia ulimwengu kuwa tanzanite yao pekee ndiyo halali maana haichimbwi na watoto. Hili ni pigo jingine kwa ndugu zetu wanaotegemea tanzanite kuendesha maisha yao.
===================================



Utumikishaji watoto katika migodi bado unaendelea nchini Tanzania licha ya serikali ya nchi hiyo kupiga marufuku utumikishwaji wa watoto.
140611230020_tanzania_watoto_304x171_bbcswahili_nocredit.jpg

Hali duni ya maisha huwalazimu watoto kufanya kazi hizo

Mererani mkoani Manyara, Kaskazini mwa Tanzania ni maarufu kwa uchimbaji wa madini aina tanzanite. Hata hivyo mgodi huo na hasa kwa wachimbaji wadogo bado tatizo la utumikishwaji linaendelea.

Mazingira ya uchimbaji madini ya Tanzanite yanaonekana ni ya hatari kwani inawalazimu wachimbaji mgodi kutumia shimo dogo la kipenyo cha takribani mita moja au mbili hivi kushuka kwenda chini ardhini kwa kutumia ngazi au kamba.

Mashimo haya ni marefu yanafikia takribani mita 300 na mengine hadi mita mia 800 toka usawa ardhi, ndani ni giza na hewa ni nzito na sura za wachimbaji mgodi hazitamaniki kwani ni wametapaa vumbi jeusi na nguo zao zimechafuka.
Sheria sio kizuizi
140611225054_tanzania_mgodi_304x171_bbcswahili_nocredit.jpg

Watoto wa kati ya umri wa miaka 12 na 13 hutumikishwa katika migodi

Lakini hilo haliwazuii wachimbaji mgodi wakubwa kwa wadogo kuendelea kufanya kazi hiyo katika mazingira hayo.
Mbali na serikali ya Tanzania kupiga marufuku watoto kufanya kazi kwenye migodi lakini baadhi yao wanaokadiriwa kuwa na miaka kati ya 12 au 13 na wengine kati ya miaka 15 hadi 17 wanafanya kazi katika migodi mbali mbali ya wachimbaji wadogo eneo hilo la Mererani.
Baadhi ya watoto wamepoteza maisha na wengine wamekuwa wakiishi maisha ya tabu na hata kukosa chakula.

Tanzania ni miongoni mwa nchi 174 zilizoridhia azimio namba 182 la kukomesha utumikishaji watoto chini ya umri wa miaka 18.
Hata hivyo pamoja na jitihada za serikali ya nchi hii kujaribu kupiga vita utumikishaji watoto bado watoto wamekuwa wakitumikishwa.

Chanzo;bbc
 
The Boss, hujui kitu. Watoto wapo nje wanaokota tu. Hakuna anayeingia shimoni. Nimekaa miezi miwili pale sikuona mtoto "nyoka" akizama chini. Wanaozama ni wana-apollo.
 
Kwani uongo watoto hawachimbi Mererani ndo yale yale yale ya kuandamana hatuli mapanki wakati tunakula.
 
Baada ya
kufanikiwa kwenye pembe za ndovu, BBC wametukung'uta tena. Safari hii ni
kwenye madini ya tanzanite. Wanadai tanzanite inachimbwa na watoto.
Wameweka video ya "the gemstone mined by child labour". Huu utakuwa ni
mkakati wa makaburu wa tanzaniteone ambao mara zote wameutangazia
ulimwengu kuwa tanzanite yao pekee ndiyo halali maana haichimbwi na
watoto. Hili ni pigo jingine kwa ndugu zetu wanaotegemea tanzanite
kuendesha maisha yao.

kwani kuna nchi nyengine inayo chimba Tanzanite?
 
Huyu sio journalist ni kanjanja...

Matusi hayasaidii. Mimi nimesema nyoka hawazami. Wanaokoteza mabaki nje tu
Pale kuna vyama kama arema na tamida vinazuia watoto kuzama. Walioko nje ni kawaida kama ilivyo kwenye fukwe ambako kuna watoto wengi au ktk masoko.
 
Matusi hayasaidii. Mimi nimesema nyoka hawazami. Wanaokoteza mabaki nje tu
Pale kuna vyama kama arema na tamida vinazuia watoto kuzama. Walioko nje ni kawaida kama ilivyo kwenye fukwe ambako kuna watoto wengi au ktk masoko.

Ila wapo ambao wanaochukuliwa na migodi kuchekecha michanga.
 
Kwani waliyosema ni uongo? Mbona ni ukweli kabisa? Hii habari itasaidia wanaohusika waamke na wafanye yanayowahusu katika kusimamia sheria.
 
Child labour kule ipo,hata kama atakaa akiokota,bado atakuwa anafanya kazi eneo la migodi.Sio kwa Tanzanite tu,in almost every sector hapa nchini kuna child labour.Wacheni ukweli usemwe,serikali yetu haiko serious na haya mambo,wamekaza macho kwenye ishu zenye maslahi kwao,OSHA nao wamebase na viwanda vikubwa vikubwa tu,TUJIFUNZE KUKUBALI UKWELI NA KUWAJIBIKA KUTATUA MATATIZO.....Waache waseme.
 
Back
Top Bottom