WanaJF
Ni jambo la kawaida kwa sasa kukuta watu mbalimbali majumbani,vijiweni,makazini,mashuleni na sehemu mbalimbali wakijadili siasa za Taifa letu.Na kote huko ni lazima katika kujadili siasa hizo CHADEMA itajwe.Hapo ndipo tulipofika watanzania.CHADEMA inaweza kuzungumzwa kwa njia yeyote iwe ni kwa mazuri au mabaya.Lakini jibu hapa tunapata kwamba hakuna asiyeijua CHADEMA.Nikiri tu kama makala zangu mbalimbali za huko nyuma nilivyosema CHADEMA kimefikishwa hapa kutokana na viongozi madhubuti wa chama hicho,Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa.Bila kuwasahau wabunge wote machachari wa chama hicho na viongozi wengine wa Kamati kuu na Baraza kuu la uongozi.
Dhumuni la bandiko hili ninataka kuzungumzia Baraza la Wanawake la CHADEMA-BAWACHA.Kwa hakika ukiniuliza hata kiongozi mmoja wa baraza hili ni nani simjui.Niwe muwazi kabisa siridhishwi na ukimya wa BAWACHA.Tukirudi nyuma kwenye chaguzi mbalimbali katika nchi yetu ni wazi wanawake ndio wapiga kura wakuu na tuseme ndio nguzo kuu ya CCM.Wanaume wanaweza kuwa wapiganaji wazuri na wasemaji sana lakini siku ya uchaguzi hawajitokezi kupiga kura.
Kwanini nawalaumu BAWACHA?
Ni ukweli ulio wazi kwamba ngome kuu ya CHADEMA kwa sasa ni vijana chini ya baraza lao BAVICHA.Na binafsi nimefurahishwa na jitihada zinazofanywa na viongozi wa vijana chini ya Mwenyekiti wao John Heche na katibu wake Deogratius Munisi.Ni juzi tu BAVICHA wamezindua jengo lao na hakika wanastahili pongezi za dhati.Sasa nikiangalia jitihada za vijana hawa kwanini jumuiya kubwa kama Baraza la wanawake wa chama liwe kimya hivyo? Tunafahamu kupitia Baraza hili CHADEMA imeteua wabunge wa viti maalum 25.Sasa hapa najiuliza idadi hii kubwa ya wabunge wa viti maalum si ndio inapaswa kuwa chachu ya kuunganisha nguvu ya kina mama mikoani? Mbona sijawahi kusikia hata mkutano mmoja umeandaliwa na BAWACHA? Ninadhani wakati mwingine unaweza kuiga mazuri kutoka kwa mtani wako.Sasa ni wakati wa BAWACHA kuangalia jinsi UWT ya CCM ilivyo imara na jinsi ilivyo chachu ya kuipa CCM ushindi wa kishindo hasa vijijini.BAWACHA wanapaswa kujua kwamba kinamama wa vijijini hawana uhuru wa kifikra na wakati mwingine wamekuwa wakibebwa na viongozi wa jumuiya ya UWT kwenda kumpigia kura hata mtu wasiyemtaka.BAWACHA wanapaswa kujua kwamba mageuzi katika mataifa mbalimbali kama ya Afrika Magharibi na kwingineko kama Zambia na Malawi yalichochewa sana na wanawake.Ilifika mahali katika kupigania demokrasia wanawake katika mataifa haya wamekuwa hata wakivua nguo na kuandamana ili dunia isikie kilio chao.BAWACHA mpo wapi?
BAWACHA wanapaswa kufanya nini?
· Wanapaswa kuunganisha nguvu ya kinamama kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa
· Wanapaswa kuwa mstari wa mbele kulaani na kukemea maovu mbalimbali kwenye jamii hasa madhila dhidi ya kinamama na watoto..mf wamtazame mama Ananilea Nkya
· Wanapaswa kujitambulisha kama nguzo kuu ya kinamama kote nchini
· Wanapaswa kuzunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara na ya ndani kuhamasisha kinamama kutokuogopa mageuzi
· Wanapaswa kujitambulisha kama nguzo kuu ya CHADEMA
· Wanapaswa kuwa na viongozi machachari wasiotishwa na wapinzani wao.
· Wanapaswa kuepuka kuwa Baraza la kufanya mkutano siku tu wanapoteua wabunge wa viti maalum.
· Wanapaswa kuandaa program ya kuwaimarisha vijana wakike walio masekondari na vyuoni ili kuwa wakakamavu na kuwaondolea hofu ya kuwa viongozi miaka ijayo
· Wanapaswa kujua kazi ya BAWACHA sio kupigania ubunge wa viti maalum tu.
Wito wangu.
Ninatoa wito kwa viongozi wakuu wa CHADEMA hasa Katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa kwamba hakika jumuiya hii inapaswa kuangaliwa upya na ni vema ikawa na mvuto kama wa BAVICHA.Si dhambi kama viongozi wa BAWACHA wameshindwa majukumu yao wakakaa pembeni wakawapisha wengine watakaoifanya BAWACHA ionekane kweli ni moto kama chama kilivyo. Nionavyo mimi BAWACHA inaweza kuichelewesha CHADEMA kuingia madarakani
WanaJF karibuni kwa mjadala!
Ni jambo la kawaida kwa sasa kukuta watu mbalimbali majumbani,vijiweni,makazini,mashuleni na sehemu mbalimbali wakijadili siasa za Taifa letu.Na kote huko ni lazima katika kujadili siasa hizo CHADEMA itajwe.Hapo ndipo tulipofika watanzania.CHADEMA inaweza kuzungumzwa kwa njia yeyote iwe ni kwa mazuri au mabaya.Lakini jibu hapa tunapata kwamba hakuna asiyeijua CHADEMA.Nikiri tu kama makala zangu mbalimbali za huko nyuma nilivyosema CHADEMA kimefikishwa hapa kutokana na viongozi madhubuti wa chama hicho,Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa.Bila kuwasahau wabunge wote machachari wa chama hicho na viongozi wengine wa Kamati kuu na Baraza kuu la uongozi.
Dhumuni la bandiko hili ninataka kuzungumzia Baraza la Wanawake la CHADEMA-BAWACHA.Kwa hakika ukiniuliza hata kiongozi mmoja wa baraza hili ni nani simjui.Niwe muwazi kabisa siridhishwi na ukimya wa BAWACHA.Tukirudi nyuma kwenye chaguzi mbalimbali katika nchi yetu ni wazi wanawake ndio wapiga kura wakuu na tuseme ndio nguzo kuu ya CCM.Wanaume wanaweza kuwa wapiganaji wazuri na wasemaji sana lakini siku ya uchaguzi hawajitokezi kupiga kura.
Kwanini nawalaumu BAWACHA?
Ni ukweli ulio wazi kwamba ngome kuu ya CHADEMA kwa sasa ni vijana chini ya baraza lao BAVICHA.Na binafsi nimefurahishwa na jitihada zinazofanywa na viongozi wa vijana chini ya Mwenyekiti wao John Heche na katibu wake Deogratius Munisi.Ni juzi tu BAVICHA wamezindua jengo lao na hakika wanastahili pongezi za dhati.Sasa nikiangalia jitihada za vijana hawa kwanini jumuiya kubwa kama Baraza la wanawake wa chama liwe kimya hivyo? Tunafahamu kupitia Baraza hili CHADEMA imeteua wabunge wa viti maalum 25.Sasa hapa najiuliza idadi hii kubwa ya wabunge wa viti maalum si ndio inapaswa kuwa chachu ya kuunganisha nguvu ya kina mama mikoani? Mbona sijawahi kusikia hata mkutano mmoja umeandaliwa na BAWACHA? Ninadhani wakati mwingine unaweza kuiga mazuri kutoka kwa mtani wako.Sasa ni wakati wa BAWACHA kuangalia jinsi UWT ya CCM ilivyo imara na jinsi ilivyo chachu ya kuipa CCM ushindi wa kishindo hasa vijijini.BAWACHA wanapaswa kujua kwamba kinamama wa vijijini hawana uhuru wa kifikra na wakati mwingine wamekuwa wakibebwa na viongozi wa jumuiya ya UWT kwenda kumpigia kura hata mtu wasiyemtaka.BAWACHA wanapaswa kujua kwamba mageuzi katika mataifa mbalimbali kama ya Afrika Magharibi na kwingineko kama Zambia na Malawi yalichochewa sana na wanawake.Ilifika mahali katika kupigania demokrasia wanawake katika mataifa haya wamekuwa hata wakivua nguo na kuandamana ili dunia isikie kilio chao.BAWACHA mpo wapi?
BAWACHA wanapaswa kufanya nini?
· Wanapaswa kuunganisha nguvu ya kinamama kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa
· Wanapaswa kuwa mstari wa mbele kulaani na kukemea maovu mbalimbali kwenye jamii hasa madhila dhidi ya kinamama na watoto..mf wamtazame mama Ananilea Nkya
· Wanapaswa kujitambulisha kama nguzo kuu ya kinamama kote nchini
· Wanapaswa kuzunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara na ya ndani kuhamasisha kinamama kutokuogopa mageuzi
· Wanapaswa kujitambulisha kama nguzo kuu ya CHADEMA
· Wanapaswa kuwa na viongozi machachari wasiotishwa na wapinzani wao.
· Wanapaswa kuepuka kuwa Baraza la kufanya mkutano siku tu wanapoteua wabunge wa viti maalum.
· Wanapaswa kuandaa program ya kuwaimarisha vijana wakike walio masekondari na vyuoni ili kuwa wakakamavu na kuwaondolea hofu ya kuwa viongozi miaka ijayo
· Wanapaswa kujua kazi ya BAWACHA sio kupigania ubunge wa viti maalum tu.
Wito wangu.
Ninatoa wito kwa viongozi wakuu wa CHADEMA hasa Katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa kwamba hakika jumuiya hii inapaswa kuangaliwa upya na ni vema ikawa na mvuto kama wa BAVICHA.Si dhambi kama viongozi wa BAWACHA wameshindwa majukumu yao wakakaa pembeni wakawapisha wengine watakaoifanya BAWACHA ionekane kweli ni moto kama chama kilivyo. Nionavyo mimi BAWACHA inaweza kuichelewesha CHADEMA kuingia madarakani
WanaJF karibuni kwa mjadala!