BAVICHA yaingia nchini Zambia kuwajulia hali wafanyabiashara waliokimbia unyanyasaji Tanzania

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,231
No_Hate_No_Fear_on_Instagram:_“Mapema_asubuhi_ya_leo_na_Mwenyekiti_@bavicha_taifa_Mh._@johnpam...jpg

Ile Taasisi bora ya vijana barani Africa kwa sasa, BAVICHA, imewasili nchini Zambia ambako inawajulia hali Lundo la Wafanyabiashara wa Tanzania kutoka Tunduma na maeneo mengine ambao walitafuta hifadhi ya kibiashara nchini humo baada ya kukimbia manyanyaso nchini mwao.

Bavicha imeongea na wafanyabiashara hao katika nchi jirani ambao wamekiri kupokelewa vema nchini Zambia na kwamba kodi wanayolipa katika nchi ya watu ni Rafiki mno na kwamba wanaimudu bila shaka na wanapata faida.

Wengi wao wameapa kutorudi tena kufanya biashara nchini Tanzania.

Juhudi za kuwabembeleza bado zinaendelea.
 
Ni aibu sana kwa nchi kukimbiwa na Raia wake kwa sababu za kubambikia kodi
Nchi nyingi zilizoendelea zinafurahia watu wake kuwekeza nje ya nchi ili zilete kitu kinaitwa Remittances, ndiyo mojawapo ya nchi kupata foreign currencies. Wewe na ukihiyo wako huoni. Nchi zenye akili zinapeleka watu nje wakabebe maboksi kama Kenya, Uganda, Philippines etc ili wafaidi remittances, wewe unapinga! Hamjui nyie
 
Nchi nyingi zilizoendelea zinafurahia watu wake kuwekeza nje ya nchi ili zilete kitu kinaitwa Remittances, ndiyo mojawapo ya nchi kupata foreign currencies. Wewe na ukihiyo wako huoni. Nchi zenye akili zinapeleka watu nje wakabebe maboksi kama Kenya, Uganda, Philippines etc ili wafaidi remittances, wewe unapinga! Hamjui nyie
Wafanya biashara wakwetu wamekimbia ugandamizaji,mfano ulioutoa unawahusu wale walioenda kwa hiari na mapenzi yao,acha kuchanganya mambo!
 
Hakuna mtu mweusi ambae anataka kulipa kodi hata siku moja na mama akileta utani kwenye kukusanya kodi ajue kuna siku atashindwa kulipa watu mishahara
Njoo Tunduma hapo uone truck la pombe linalipa kiasi gani likiwa limeshachajiwa TBS milion saba na laki tatu mkishiba ugali pili pili kichaa mnaongea chochote harafu uone ni wazungu wanalipa hiyo pesa...huku VAT uliyolipia SA unairudisha ukifikisha mzigo Tanzania
 
Back
Top Bottom