BAVICHA iko wapi?

BAVICHA iko wapi?

Na mtamaliza kuni kuchochea mawe na hayataiva, hivi mmeshawahi kukaa chini na kutathmini ni kwa kiasi gani propaganda zenu dhidi ya CHADEMA zimewanufaisha!??? au ndo vile mkishatia ndani posho mnakua mmemaliza kazi na kuanza kufikiria jingine la kutoka nalo mkidhani kwamba mtaisambaratisha CHADEMA kwa mtindo huo, I dare say Mtasubiri sana meli airport huku CHADEMA ikichanja mbuga...
Kwamipasho weeee! Sikuwezi, enhe tungo hiyo ya nani Adija kopa au niyako mwenyewe?
 
Una uchungu sana na yanayoendelea CHADEMA ila yaliyoko ndani ya ccm na serikali yenu huyaoni!??, hivi mkishatung'oa kucha huwa mnazifanyia nini!???
Majibu ya maswali yako nenda kamuulize GAID
 
Minadhani mwenzetu kahoji kama mdau wa siasa hakuhoji kama yeye ni CCM, chamsingi nachamaana naingekua busara zaidi kama hoja hii inge jibiwa na viongozi wa CDM sio vifuata upepo,ambao hata yalipo makao makuu ya chama hampajui
Unataka kutuambia mleta mada ni Kiongozi wa CCM?
 
Nawaomba wafusi/wanachama wa CDM muwe wastaarabu kwenye kujibu hoja. Mipasho, dhihaka inaonyesha ni jinsi gani mulivyo mambulula kwenye kujibu hoja. Tusifanye mijadala kishabiki kama Yanga na Simba. Pia nilazima tujue kuwa watu hatufanani kimitazamo nandivyo inavyo itajika ktk demokrasi. Laiti kama wanasiasa wote wakiwa na mtazamo mmoja ( hakuna wa kuping) nchi yetu haiwezi kufika pale tupatakapo.
 
Kwahiyo kwenye mizani yako wewe Zitto aendelee kuchafuliwa mpaka siku pesa za EPA zitakapokuwa hazijaibiwa?

Kwani wakati waliomchafua Dr. Slaa wanapewa adhabu kulikuwa hakuna pesa za EPA zilizoibiwa?

Tatizo unataka kuwapangia Bavicha kazi.kama wengine walifukuzwa kwa hiyo unataka Ben naye afukuzwe zaidi ya lile kalipio kali alilopewa?.Hapo ndipo uridhike kuwa swala la utawala bora limezingatiwa.
 
Tatizo unataka kuwapangia Bavicha kazi.kama wengine walifukuzwa kwa hiyo unataka Ben naye afukuzwe zaidi ya lile kalipio kali alilopewa?.Hapo ndipo uridhike kuwa swala la utawala bora limezingatiwa.

Kumbe Bavicha mambo yao haipaswi kuhojiwa!!!

Nazidi kuelewa kwanini miaka 20 tangu upinzani urushusiwe rasmi Tanzania lakini hakuna aliyefanikiwa kupata hata asilimia 30 ya kura za Urais. Wapiga kura wanataka kuona nia ya dhati ya kujenga nchi sio hizi longolongo...
 
Kwahiyo kwenye mizani yako wewe Zitto aendelee kuchafuliwa mpaka siku pesa za EPA zitakapokuwa hazijaibiwa?

Kwani wakati waliomchafua Dr. Slaa wanapewa adhabu kulikuwa hakuna pesa za EPA zilizoibiwa?

Mkuu hujanielewa!
Mm napinga watu wa CCM kuja hapa na kuanza kutuhubiria kuhusu utawala bora maana kama kuna serikali inayopindisha utawala bora DUNIANI ukiiacha serikali ya JK wanazuoni WATAKUSHANGAA!

Sikuwa na maana kuwa Zitto aendelee kuchafuliwa by any means ingawaje Ben KALIPINGA ANDIKA LAKO!

Zemarcopolo UNAWEZA TUTHIBITISHIA pasipo shaka yyt ile kuwa Ben anamchafua MB Zitto?
 
Mkuu hujanielewa!
Mm napinga watu wa CCM kuja hapa na kuanza kutuhubiria kuhusu utawala bora maana kama kuna serikali inayopindisha utawala bora DUNIANI ukiiacha serikali ya JK wanazuoni WATAKUSHANGAA!

Sikuwa na maana kuwa Zitto aendelee kuchafuliwa by any means ingawaje Ben KALIPINGA ANDIKA LAKO!

Zemarcopolo UNAWEZA TUTHIBITISHIA pasipo shaka yyt ile kuwa Ben anamchafua MB Zitto?

Hivi ndugu yangu, wewe hujaona thread ya Ben akitaka Zitto ahojiwe kwa kuwa Ben anaamini kuwa Zitto anahusika na ugaidi? Kama uko sio kumchafua ni nini?
Unajua its like this, Ben is a minuature figure. Tatizo ni wanaomtuma...
 
Kumbe Bavicha mambo yao haipaswi kuhojiwa!!!

Nazidi kuelewa kwanini miaka 20 tangu upinzani urushusiwe rasmi Tanzania lakini hakuna aliyefanikiwa kupata hata asilimia 30 ya kura za Urais. Wapiga kura wanataka kuona nia ya dhati ya kujenga nchi sio hizi longolongo...

Hivi kweli matatizo ya CCM yameisha kiasi cha kupata mda wa ziada wa kuhangaika na ya CDM? Angalizo tu ni kuwa ''mali'' mliyo-import toka CDM ni demaged beyond repair
 
Mkuu samahani, wee unahoji kama nani

Najua vijana wa chadema mmefundishwa kwamba anayeruhusiwa kuhoji mambo ni Slaa na Mbowe peke yao, nyinyi wengine kazi yenu ni kuitikia kile mnachoambiwa tu. Mpaka siku mtakapogundua kuwa mmelaghaiwa itakuwa TOO LATE...
 
Back
Top Bottom