Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
Wanachadema ni vyema CDM wakainvest kwenye tafiti na kujua tabia za wananchi kwenye majimbo husika kwa kuwa utamaduni na tabia zetu kimakabila pia zinaathiri maamuzi yetu na utendaji wetu.
Kwa tabia ninavyowajua wanyamwezi na wasukuma ni watu walio watiifu kitabia kwa wenye mamlaka [Royal],Msukuma au mnyamwezi ni mwoga kwa mwenye mamlaka hata wakati mwingine utaniwa kuwa unaweza kumkuta kituo cha polisi selo,kashikilia nondo za sero ukamuuuliza vipi tegemea jibu kama "NDO SHIDA" yaani kwa kiswahili HAKUNA TATIZO.Sasa kama hakuna tatizo sero unafanya nini?Huyo ndio Msukuma na Mnyamwezi ambao kitabia wanashabiana sana.
Hivyo kwa jimbo la IGUNGA ushauri wangu kwa CHADEMA waende wakajifunze tabia za jamaa hao na uenda siku za mbele wakajua jinsi ya kudeal nao.
Waliipo lia juu ya jamaa yao Rostam ni kweli,kwa kuwa wao huwa si watu wa kujua kitu kwa undani ndio maana ni moja ya makabila yaliyongoza miaka ya nyuma enzi za ukoloni kukubali kuwakaribisha wageni na kuwapa Ardhi na mabinti zao.
Ukitembele mikoa ya uko ni lahisi na si ajabu kusikia baadhi ya majina kama MASKATI FISI,yaani ni sehemu ya jina la mji mmoja uko uarabuni lakini ndani ya Tanzania.
Hivyo CHADEMA kajifunzeni jinsi ya kuwabadilisha wenyeji hao,kwa kuwa kikabila wanautamaduni wao ambao ni mzuri kwa watawala lakini ukiwaponza wao kama Watanzania wenye kuitaji maendeleo.Moja ya mapungufu yao ni kupenda kutawaliwa na wageni.Mikoa hiyo ukiitazama sana wawakilishi wake wengi wa bungeni wana asili ya mchanganyiko.
Hivyo wajue dhahiri jimbo la IGUNGA bado ni mali ya CCM japo kidogo sana CUF wanaweza kuthubutu nao kama watamtumia mtu mwenye asili ya mchanganyiko kwa kuwa ndio moja ya mapungufu [kilema] ya watu wa huko.ILA SIO MBAYA waende wakajaribu kwa kuwa something is better than nothing na hivyo pia watachangia kuwaamsha kizazi kipya kuwa na mwamko japo itachukua muda tofauti na mikoa mingine ambayo watu wenye asili ya mchanganyiko hawako.
Kumbe kweli akutukanae hakuchagilii tusi, au hawa ni watanizako.