Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 255
Taarifa za hivi punde zinasema kwamba Basi la Kampuni ya Abood lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam limepata ajali maeneo ya Mswiswi.
Mtoa taarifa amesema: "Abood kutoka Mbeya kwenda Dar asubuhi ya Leo maeneo ya Mswiswi.
"Poleni sana aisee, taarifa kamili itakuja baadae na itatolewa na mamlaka husika."
Mungu awanusuru wote.
----------- ----------------
Updates...
POLISI WAFIKA SEHEMU YA TUKIO
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema “Ni kweli ajali imetokea na basi limelalia ubavu mmoja, kuna majeruhi kadhaa ambao wamepelekwa hospitali.”
“Inavyoonekana chanzo cha ajali ni dereva kukosa umakini wakati akiwa katika mwendo kasi, bahati mbaya dereva amekimbia na hatujui alipo, abiria wengine wameondoka kwa usafiri mwingine.
“Tunaendelea kulifanyia uchunguzi basi kisha tutatoa taarifa kamili baadaye.”