Bashiru Ally: Vyama vya siasa Vya Maslahi

Bashiru Ally: Vyama vya siasa Vya Maslahi

Kwenye kipindi chao cha 'je tutafika?'. Eti wanasema serikali 3 ni UBAGUZI. Na kumshushua mzee Warioba. Siwaelewi wasomi wetu siku hizi. Wamekaririshwa neno moja, MABEBERu



Siku hiyo sikupenda mawazo ya huyu msomi wa UDSM hasa aliposema Rasimu ya katiba Siyo kesi ya Babu Seya kwamba haisemwi tena labda kwa msamaha wa Rais. Nikaona huyu anafundisha jamii nini Kuoanisha Katiba na kesi hiyo? Mara oh serikali tatu ni Ubaguzi na mengineyo nikakosa hamu ya kumsikiliza Nikatune Channel nyingine nikaachana naye
 
Wanachama,wafuasi &mashabiki wa CHADEMA wanapaswa kujifunza kuheshimu na kuvumilia hoja kinzani kwa sababu haiwezekani watu wote ndani na nje ya taasisi hiyo ya kisiasa kuwa na fikra,mawazo na mitazamo inayofanana.
Usibomoe mtu,badala yake,boma hoja.

Na wewe ungetumia neno baadhi....sio wapenzi wote wa CHADEMA hutoa maoni sawa!
Wengine huwa hatuchotwi na hisia!
 
kama kweli hayo kasema bashiru hayupo sawa kwani akisema watu wamekata tamaa namuliza ni watu gani waliokata tamaa? au yy ndo kakata tamaa? mbona ccm wakifukuza watu asemi kua watanzania wamekata tamaal na suala la migogoro sio suala la kukata tamaa, ni vp mtatatua then msonge mbele, mawazo anayotoa yy ndo yakukatisha tamaa.
 
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Bw. Bashiru Ally amesema upinzani hauongezeki nchini kwa sababu hakuna uwajibikaji ndani vyama na kwamba wananchi wamekata tamaa.
Amesema vyama vinaweza kuahidi katiba ndani ya siku 100 na wananchi wakakimbilia hayo matumaini hewa kumbe lengo lao na kuingia Ikulu.

Anaendelea kusema mgogoro wa Chadema umewakatisha tamaa wananchi kwani wapo watu waliowekeza nguvu,muda na fedha wakidhani wamepata chama Mbadala.Kwamba kilichotokea ni kama mimba imetoka.


Source: jamhuri jan.13-20,2014


My take:Huyu eti ni msomi.

Kinachomtia upofu ni udini au mapenzi ya uccm?

Alichokosea ni msomi kuongea kama wazushi wa mitaani tu!
Yeye alipaswa kuongea kwa facts,kutoa percent ya waliokata tamaa (from his research results)....na pia idadi ya ambao wametiwa moyo na suala hili.....na mwisho maoni ya wananchi kwa vyama vya sias as how they give answers to questionnaire!
Sasa msomi amepingana na "no research,no right to speak".
 
Kwa kweli ni janga kuwa na eti mhadhiri katika chuo kama hiki.
 
Back
Top Bottom