jingalao hata kama umeandika kwa namna ya kutengeneza exaggeration lakini Bashe ana point!
Hii nchi ina changamoto nyingi sana tena sana na miongoni mwa hizo changamoto kuna zile ambazo attractive for private sector na zingine sio attractive!!!
Unapokuwa huna pesa za kutosha basi unatakiwa kuelekeza pesa hizo kwenye zile changamoto ambazo sio attractive kwa private sector kwa sababu, unajua zile ambazo ni attractive, itakuwa na mbadala wa ku-outsource fund!!
Kwa mfano, Tanzania tunataka maji safi na salama na pia tunahitaji reli ya uhakika!!!
Sekta ya maji sio attractive kwa private sector lakini sekta ya usafiri ni very attractive!!
Wakati unaweza ku-initiate PPP kwenye sekta ya usafiri, including ujenzi wa reli na ukapata wabia toka sehemu mbali mbali duniani; PPP kwenye sekta ya maji inaweza kukosa wabia!!!
Sasa kama una shilingi moja tu na wakati huo huna maji wala reli; rational decision making ni kuipeleka hiyo shilingi moja kwenye maji kwa sababu unafahamu kule kwenye reli unaweza ku-initiate PPP na mambo yakaenda!!!