salaam wana Bodi wote
Hongereni wana CCM kwa kufanya Mkutano wenu Mkuu huku kukiwa na mazingaombwe lukuki.
Naomba nimuongelee Bwana Hussein Bashe. Mwaka 2008 aligombea Umakamu mwenyekiti (UVCCM) na Beno Malisa akashindwa. Tena kwa mbinu kwani nilikuwa mmoja wa wajumbe wa mkutano Mkuu. Bashe alishindwa baada ya Mwenyekiti wa CCM kushawishi uongozi kubadili Ratiba ya Mkutano na kura kupigwa baada ya Hotuba ya Ufunguzi na si kesho yake kama ratiba ilivyovyokuwa isaema. Bwana bashe akakimbia Dodoma akiwa yeye na Bw. Nape, Rostam Azizi na wengine wengi baada ya matokeo kuvuja usiku wa saa 8.00.
Baada ya Mapacha watatu (R.A,E.L na A.C) kushambuliwa sana kwa tuhuma za Ufisadi na CCM kuanzisha slogan ya kuvuana Magamba Bwana Bashe akawa wakili kwenye media kwa kuwalinda na pengine kuwatetea na hata kuwajibia baadhi ya mambo (kwa Mfano Bashe alimjibia Rostam Kuhusu Uhusiano kati ya Caspian na Richmond) kuwashambulia kwenye media kina NAPE, SITA, MWAKYEMBE, MENGI nk. kuhusu tuhuma za Richmond na Ufisadi kupitia kampuni ya New Habari Coperation.kumbuka kuwa Nape NNauye ndiye aliekuwa wakala wa kuhesabu kura za Bashe 2008.
Bwana Bashe akagombea Ubunge nzega kupitia CCM wakamwambia sio Raia wa Nchi hii wakammwaga na mpaka leo hakuna lolote lilisomwa na Wizara ya mambo ya Ndani kuhusu Uraia wa Bashe. Haya tena akaomba NEC nako CCM wakamtosa. Anatajwa kuwa mtoa Rushwa kwenye uchaguzi wa UVCCM Leo anasambaza Vipeperushi vya kumpinga Mwenyekiti wao.
Kuna mambo mengi tu; Swali huyu Kijana CCM haimtaki, Lakini pia sio Raia kwenye hii nchi anafanya nini? Anaitakia nini CCM wakati imeonyesha kumkataa? Kwa nini anampinga Kikwete Uswahiba na kina beno waliokuwa wapinzani wake 2008 umeanza lini na uadui na kina membe Nape ,Sita waliokuwa wanambeba 2008 umeanza lini.
my Take: kama huyu kijana Chama chake Hakimtaki, Uraia wake ni Magumashi lakini bado anapata coverege kubwa kiasi hiki mi naona lipo Tatizo USALAMA WA TAIFA INGIENI KAZINI. Huyu mtu sie kabisa. Nahofia yasije yakawa ya yule waziri mhindi alikufa akaenda kuzikwa canada. Siku E.L akiwa Rais huyu Bwana atakuwa waziri wa Ulinzi msipoangalia.
Nawasilisha