Nendubotho Sunguya
Senior Member
- Oct 9, 2019
- 126
- 112
Tumeamua kuchanga kutengeneza barabara ya Msongola iwe kiwango cha lami tusaidiane kuisambaza hii barua ifikie watu wote hasa mh Rais John Joseph Magufuli
NEEMA JOHN MOLLEL
KITONGA-MSONGOLA,
0746715216.
DAR-ES-SALAAM.
RASI WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
DAR-ES-SALAAM.
Tafadhali rejea kichwa cha habari hapo juu. Barua hii nimeielekeza ikulu kwa sababu ndio sehemu ya juu inayotuunganisha pamoja na viongozi wengine wote ikiwemo mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya ya temeke na Ilala ambazo zinaunganishwa na barabara hii, lakini kikubwa kwa wananchi wanaoishi Msongola, Kitonga, Mbande, Kisewe pamoja na wanaopita njia hii kwenda Chanika na Mvuti, pamoja na wafanya biashara wote waletao bidhaa zao maeneo tajwa hapo juu.
Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli, sisi wananchi wa Kitonga, Mbande, Msongola na Kisewe na maeneo mengi yanayoungwa na barabara hii tunapata tabu sana na hii barabara kwa nyakati zote, kipindi cha jua ni makorongo na vumbi zito na kipindi cha mvua ni madimbwi pamoja na tope lisiloolezeka. Ni tabu isiyoelezeka. Kuna mama alishawahi jifungua barabarani kwa kushindwa kufika hosipitali kwa wakati, nayo magari ni shida kufika huku hivyo kupekelea kuchelewa maeneo ya kazi na pia gharama kubwa ya usafiri.
Tunajua fika kwa sasa kuna miradi mingi ya maendeleo inayoendelea kujengwa ndio nikapata wazo hili la kuchangia kiasi tutakachofikisha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa hiyari. Nilitaka kutafuta namna ya kuendesha mikutano ya hadhara tutafute namna ya kuchangisha pesa hizo maana kwa hali ya barabara hii hakuna mwananchi atakayekataa kujitoa kwa namna atakayoweza, kabla ya hapo nimeona niandike barua hii ya wazi tuisambaze kwenye vyombo vya habari ili kuwapa taarifa wananchi ili tupate muongozo wako maana kwa mimi peke yangu bila msaada taarifa haitasambaa vizuri.
Mheshimiwa Rais kama tunachangia maharusi mamilioni ya pesa na barabara tutaweza tena kwa moyo wote, hivyo tunakuomba utupe muongozo lakini kikubwa tunaomba Baraka zako na sapoti kutoka kwako, Maana tunajua ni pesa nyingi inahitajika kwenye ujenzi wa kilomita chache tu lakini kwa kipande hichi ambacho kwa makadirio ni kama kilomita sita hivi, hata tukipunguza kilomita moja tutakua tumepunguza adha tunayopata.
Nimejaribu kuongea na baadhi ya wananchi wenzangu wanaonaje kama tukijichanga kwa ajili ya ujenzi wa barabara kila mmoja anasema yupo tayari hata kushika sururu, maana huku tukiona mvua tunawaza barabara itapitika? Wakati wenzetu wanawaza wakalime na kuifurahia mvua.
Barua hii pia imfikie mkuu wa mkoa Paul Mkonda, mkuu wa wilaya ya Ilala pamoja na mbunge wa Jimbo hili la Ukonga ambako barabara hii ipo.Tunaomba muongozo waheshimiwa hii barabara tangu enzi na enzi ni korofi.
Mwisho kabisa barua hii ifikie vyombo vyote vya habari, magazeti, televisheni na mitandao yote ya kijamii, tunaomba mtusaidie kusambaza barua hii kwa watanzania wote kwani tunaitaji sapoti ya kila mtanzania, tutatangaza tarehe rasmi ya kuanza mikutano na harambee mbalimbali kama tukipata Baraka kutoka kwa viongozi wetu hasa Rais wetu John Joseph Pombe Magufuli
NEEMA JOHN MOLLEL
KITONGA-MSONGOLA,
0746715216.
DAR-ES-SALAAM.
RASI WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
DAR-ES-SALAAM.
YAH: KUCHANGIA UJENZI WA BARABARA YA MSONGOLA ILALA DAR ES SALAAM IWE KIWANGO CHA LAMI.
Tafadhali rejea kichwa cha habari hapo juu. Barua hii nimeielekeza ikulu kwa sababu ndio sehemu ya juu inayotuunganisha pamoja na viongozi wengine wote ikiwemo mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya ya temeke na Ilala ambazo zinaunganishwa na barabara hii, lakini kikubwa kwa wananchi wanaoishi Msongola, Kitonga, Mbande, Kisewe pamoja na wanaopita njia hii kwenda Chanika na Mvuti, pamoja na wafanya biashara wote waletao bidhaa zao maeneo tajwa hapo juu.
Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli, sisi wananchi wa Kitonga, Mbande, Msongola na Kisewe na maeneo mengi yanayoungwa na barabara hii tunapata tabu sana na hii barabara kwa nyakati zote, kipindi cha jua ni makorongo na vumbi zito na kipindi cha mvua ni madimbwi pamoja na tope lisiloolezeka. Ni tabu isiyoelezeka. Kuna mama alishawahi jifungua barabarani kwa kushindwa kufika hosipitali kwa wakati, nayo magari ni shida kufika huku hivyo kupekelea kuchelewa maeneo ya kazi na pia gharama kubwa ya usafiri.
Tunajua fika kwa sasa kuna miradi mingi ya maendeleo inayoendelea kujengwa ndio nikapata wazo hili la kuchangia kiasi tutakachofikisha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa hiyari. Nilitaka kutafuta namna ya kuendesha mikutano ya hadhara tutafute namna ya kuchangisha pesa hizo maana kwa hali ya barabara hii hakuna mwananchi atakayekataa kujitoa kwa namna atakayoweza, kabla ya hapo nimeona niandike barua hii ya wazi tuisambaze kwenye vyombo vya habari ili kuwapa taarifa wananchi ili tupate muongozo wako maana kwa mimi peke yangu bila msaada taarifa haitasambaa vizuri.
Mheshimiwa Rais kama tunachangia maharusi mamilioni ya pesa na barabara tutaweza tena kwa moyo wote, hivyo tunakuomba utupe muongozo lakini kikubwa tunaomba Baraka zako na sapoti kutoka kwako, Maana tunajua ni pesa nyingi inahitajika kwenye ujenzi wa kilomita chache tu lakini kwa kipande hichi ambacho kwa makadirio ni kama kilomita sita hivi, hata tukipunguza kilomita moja tutakua tumepunguza adha tunayopata.
Nimejaribu kuongea na baadhi ya wananchi wenzangu wanaonaje kama tukijichanga kwa ajili ya ujenzi wa barabara kila mmoja anasema yupo tayari hata kushika sururu, maana huku tukiona mvua tunawaza barabara itapitika? Wakati wenzetu wanawaza wakalime na kuifurahia mvua.
Barua hii pia imfikie mkuu wa mkoa Paul Mkonda, mkuu wa wilaya ya Ilala pamoja na mbunge wa Jimbo hili la Ukonga ambako barabara hii ipo.Tunaomba muongozo waheshimiwa hii barabara tangu enzi na enzi ni korofi.
Mwisho kabisa barua hii ifikie vyombo vyote vya habari, magazeti, televisheni na mitandao yote ya kijamii, tunaomba mtusaidie kusambaza barua hii kwa watanzania wote kwani tunaitaji sapoti ya kila mtanzania, tutatangaza tarehe rasmi ya kuanza mikutano na harambee mbalimbali kama tukipata Baraka kutoka kwa viongozi wetu hasa Rais wetu John Joseph Pombe Magufuli