Barua ya Kinana kwa Mwigulu Nchemba ni faida na hasara kwa Chama

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Nimepata taarifa ya kusambaa kwa barua ambayo amepewa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndg Mwigulu Nchemba, yenye maudhui ya katazo la kufanya ziara.

Kimsingi ni sahihi kuwa Mhe Mwigulu, Mbunge wa Iramba, Naibu waziri wa fedha na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara amepewa barua ya kumtaka kusitisha ziara zake kwa minajali kuwa;
Ziara zake hazifuati utaratibu wa chama, ambao unataka ziara hizo kupangwa na kuratibiwa katika mfumo wa vikao rasmi ndani ya Chama.
Mwigulu ni miongoni mwa wanaotajwa kuwania Urais kwa tiketi ya CCM, na imehisiwa kuwa ziara hizo ni maandalizi na kampeni ya kujiandaa kwa jambo hilo kubwa.

Msimamizi wa Kanuni na Katiba ya Chama Cha Mapinduzi ni Katibu Mkuu na ndiye mwenye mamlaka ya kusimami shughuli za kila siku za chama hicho. Hii ni pamoja na ku-oversight utendaji wa subordinates wake (Mwigulu akiwemo)

Suala hili limeshaibua mijadala katika forum mbalimbali, mijadala yenye hoja na hisia mbalimbali, baadhi wakiiunga mkono hatua hiyo na wengine wakiipinga.

Wanaoipinga wanastress on the point kuwa ziara hizo zinajenga chama, zinarudish imani ya watu kwa Chama na watendaji wake. Ni ukweli kuwa kukubalika kwa Mwigulu ndio kukubalika kwa CCM and vice versa is true.

Katika kipindi ambacho wananchi wamevurugwa na mitazamo inayosimamiwa na ukawa inayokipaka chama cha mapinduzi matope, ziara hizo zilikuwa ni dozi ya nyongeza baada ya ile ya Katibu Mkuu.

Hoja nyingine inahoji busara iliyotumika, ikiwa kutangaza nia ya urais kunamuondolea kiongozi muandamizi wa Chama haki ya kufanya kazi yake ndani ya Chama, basi kanuni zetu hazituongozi sehemu salama, ikiwa waziri mkuu kutangaza kwake nia kungemfanya apate katazo la kufanya kazi zake kiserikali, ama waziri ama naibu waziri basi tungekuwa na taifa la ajabu. Ikiwa watu wanaofanya kazi za taasisi zetu kwa umakini na ari wanapoteza sifa siku tu wanapoonekana kuwa wanahamu ama kuna hisia tu kuwa wanataka nafasi za juu zaidi za utumishi kwa Chama na Serikali...wanahoji busara hii.

Lakini hoja nyingine ni ya ulinganishi (comparison analysis) inayodai kuwa zipo taarifa mbalimbali za makada wa CCM na baadhi viongozi ambao wanakihujumu chama waziwazi, kwa maneno na matendo na hatua za makatazo na karipio hazijaelekezwa kwao. Lakini hoja hii pia inatanuka na kutathmin athari zinazopatikana kwa Ziara za Mwigulu ndani ya Chama na Nje ya Chama ndani ya jamii, na madhara yatakayopatikana kwa kusitishwa kwake na watetezi wa hoja hii wanasema madhara yake ni makubwa kuliko athari zake.

Wanaounga mkono hatua hiyo ya Katibu Mkuu wanatoa hoja zifuatazo;
katika kipindi ambacho baadhi ya watarajiwa wakiwa wanaendelea kutumikia adhabu, si busara wala haki kuwaacha wengine wanaofanya mfano wa yale waliyoyafanya wao waachwe wakiendelea kwa mwamvuli wa nafasi zao ndani ya Chama. Chama hiki kimejengwa katika misingi ya Haki, Usawa na Uadilifu, si vyema kwa katibu mkuu kuendesha chama nje ya misingi hiyo.
chama ni taratibu, siku CCM kikiacha kanuni zake, misingi yake na mila yake hakitabaki chama salama na itakuwa ndio mwisho wake. Na kimsingi utaratibu unaeleweka wazi kuwa muda wa kampeni bado, hivyo ni sahihi bila kujali nafasi, hadhi ama cheo kila mmoja akafuata utaratibu huo na atakayeenda kinyume achukuliwe hatua za kinidhamu kama ilivyokwishafanyika kwa wengine.
Ziara hizo hazijengi chama, bali zinalenga kumjenga mtu binafsi, kwa maana zinalenga kumjenga Mwigulu kama yeye na wala si kwa manufaa ya Chama, na zipo kimkakati maalum unaolenga Urais 2015.


Kimsingi mjadala huu utaendelea kujengwa kwa hoja zenye tafsir mbalimbali na zinategemewa hoja hizo kuijenga ama kuibomoa taswira ya MWIGULU lakini pia kwa kiwango hicho hicho na hoja hizo hizo zinaweza kujenga chama kwa maana kitachukuliwa ni chenye kusimamia taratibu zake na chenye kufanya maamuzi lakini pia zinaweza kuharibu murua wa chama na kutoa taswira kuwa ktk chama hicho kuna vita kali ya wenye uchu wa madaraka ambao hawafikirii chochote kwa maslahi ya chama hicho isipokuwa kukalia kiti cha Urais.

Hii ni tathimini tu..

By:

ALLEX KOWE.
 
Last edited by a moderator:
Hivi Nyalandu ameshaitwa na kamati ya maadili juu ya kutangaza nia waziwazi hadi kuahidi kukodisha kwaya ya kanisa kwa ajili ya kuapishwa novemba mwaka huu?

Hivi Kinana hamuoni Pinda aliyetangaza waziwazi kuwa ametangaza nia kimyakimya?Tena mjumbe wa kamati kuu ya chama?

Kinana anampigia nani kampeni maana inawezekana Mwigulu amekua tishio dhidi ya yule anayemtaka yeye Kinana

Juzi niliandika hapa style ya Mwigulu ya kupambana na mafisadi hasa wakwepa Kodi itamgharimu huko CCM maana hata Meli za Kinana sidhani kama zinalipa kodi.

Kitakachozidi kuiangamiza CCM ni double standard na uonevu

Hizo Hasira za Kinana mbona hazionekani kwa Samwel Sitta na hata akina Nyalandu?

Simply kwa sababu ana uhakika kuwa hao ni harmless na wanatabirika?
 
Mwigulu ana kampeni ya kujijenga yeye. Hata humu mitandaoni ameajiri vijana wanaopost daima kumjenga, mfano ni acer, ukwelinauwazi, Robert p r Mwaka Mpya 2015 na sasa CHAMVIGA .

Sasa amepigwa stop


attachment.php
 
Hivi Nyalandu ameshaitwa na kamati ya maadili juu ya kutangaza nia waziwazi hadi kuahidi kukodisha kwaya ya kanisa kwa ajili ya kuapishwa novemba mwaka huu?

Hivi Kinana hamuoni Pinda aliyetangaza waziwazi kuwa ametangaza nia kimyakimya?Tena mjumbe wa kamati kuu ya chama?

Kinana anampigia nani kampeni maana inawezekana Mwigulu amekua tishio dhidi ya yule anayemtaka yeye Kinana

Juzi niliandika hapa style ya Mwigulu ya kupambana na mafisadi hasa wakwepa Kodi itamgharimu huko CCM maana hata Meli za Kinana sidhani kama zinalipa kodi.

Kitakachozidi kuiangamiza CCM ni double standard na uonevu

Hizo Hasira za Kinana mbona hazionekani kwa Samwel Sitta na hata akina Nyalandu?

Simply kwa sababu ana uhakika kuwa hao ni harmless na wanatabirika?
Kwanza kabisa ni vyema ukatambua kuwa kutangaza nia ndani ya CCM sio dhambi wala kwa kufanya hivyo mtu hawi amefanya kosa la aina yeyote.

Lakini pia, ni vyema kufahamu kuwa kilichokatazwa ni kufanya kampeni ya kujitangaza na kuwashiwishi wananchi wakuone wewe bora kuliko wengine kwa maneno na matendo yako, kampeni ama kujinadi ndiko kulikokatazwa.

Ama hii hoja nyingine ya kuwa anapingana na ufisadi na kwamba kwa kitendo chake hicho Kinana kwa sababu binafsi za kuogopa kuchukuliwa hatua amemuandikia barua hiyo ni jambo la hovyo.
 
Hivi si ni juzi tu tulimsikia E Lowassa akifanya ziara ya kugawa pesa Zanzibar? Au ni nn maana ya ziara!
 
Kwanza kabisa ni vyema ukatambua kuwa kutangaza nia ndani ya CCM sio dhambi wala kwa kufanya hivyo mtu hawi amefanya kosa la aina yeyote.

Lakini pia, ni vyema kufahamu kuwa kilichokatazwa ni kufanya kampeni ya kujitangaza na kuwashiwishi wananchi wakuone wewe bora kuliko wengine kwa maneno na matendo yako, kampeni ama kujinadi ndiko kulikokatazwa.

Ama hii hoja nyingine ya kuwa anapingana na ufisadi na kwamba kwa kitendo chake hicho Kinana kwa sababu binafsi za kuogopa kuchukuliwa hatua amemuandikia barua hiyo ni jambo la hovyo.

Sasa mtu ambaye hajatangaza nia utamhukumuje kuwa anafanya kampeni ya kujitangaza.Hivi wananchi wakibeba mabango kumtaja Rais inakua kosa?Mbona tunanyang'anya watu haki ya kikatiba yaani freedom of expression?
 
Kwanza kabisa ni vyema ukatambua kuwa kutangaza nia ndani ya CCM sio dhambi wala kwa kufanya hivyo mtu hawi amefanya kosa la aina yeyote.

Lakini pia, ni vyema kufahamu kuwa kilichokatazwa ni kufanya kampeni ya kujitangaza na kuwashiwishi wananchi wakuone wewe bora kuliko wengine kwa maneno na matendo yako, kampeni ama kujinadi ndiko kulikokatazwa.

Ama hii hoja nyingine ya kuwa anapingana na ufisadi na kwamba kwa kitendo chake hicho Kinana kwa sababu binafsi za kuogopa kuchukuliwa hatua amemuandikia barua hiyo ni jambo la hovyo.

Kunahaja ya kufanya utafiti hapa hivi ni chama ndicho kinachoharibu watu au watu ndio wanaoharibu hiki chama. Maana mtu anaweza kuwa mzuri mwenye hoja makini, lakini akianza tu kujinasibisha na hiki chama lazima Akengeuke sijui ni kwanini..?

Sasa ndugu ya mleta mada, Mada yako hapo jui imekaa vizuri tu ila ukimjibu Ben hapa umeharibu tayari. Huwezi kukitetea chama na wakati huo huo ukataka kuonyesha madhaifu yake, badala yake wewe ndio utaonekana Dhaifu....!!

Hivi unawezaje ukatangaza nia ya kutaka jimbo,Kata au Urais halafu ukakaa kwenu na wanao?? Mtuanayetangaza kukitaka kitu hususani nafasi ya uongozi lazima aonyeshe kwamba kweli anaihitaji kwa vitendo. Huwezi ukaruhisu watu kutangaza nia na wakati huohuo ukawazuia kujinadi ni ujinga, Wananchi watamjuaje basi maana sharti anayetaka hiyo nafasi ajionyeshe kivitendo na kwa maneno. sasa wewe unataka kumdanganya nani hapa

BACK TANGANYIKA
 
Ukisoma vizuri barua hii, utabaini kuwa inazungumuzia kuzunguka kwa jamaa mikoani ambako anafanya kampeni za kipekee pekee bila kushirikisha ngazi yoyote ya CCM. Aidha, inaonyesha wanatambua nia ya Mwigulu kuutaka urais, barua iko wazi.

Hivyo, kama wengine wamekatazwa kuzunguka mikoani na wilayani kwa kazi hizo, si haki kwa Mwigulu kuendelea. Inaweza kuharibu taswaira ya chama tofauti na Saa8 unavyoweka mlinganisho wa "double standard".

Naona kilichofanyika ni sawa kama kiongozi.
 
Kwanza kabisa ni vyema ukatambua kuwa kutangaza nia ndani ya CCM sio dhambi wala kwa kufanya hivyo mtu hawi amefanya kosa la aina yeyote.

Lakini pia, ni vyema kufahamu kuwa kilichokatazwa ni kufanya kampeni ya kujitangaza na kuwashiwishi wananchi wakuone wewe bora kuliko wengine kwa maneno na matendo yako, kampeni ama kujinadi ndiko kulikokatazwa.

Ama hii hoja nyingine ya kuwa anapingana na ufisadi na kwamba kwa kitendo chake hicho Kinana kwa sababu binafsi za kuogopa kuchukuliwa hatua amemuandikia barua hiyo ni jambo la hovyo.

Kunahaja ya kufanya utafiti hapa hivi ni chama ndicho kinachoharibu watu au watu ndio wanaoharibu hiki chama. Maana mtu anaweza kuwa mzuri mwenye hoja makini, lakini akianza tu kujinasibisha na hiki chama lazima Akengeuke sijui ni kwanini..?

Sasa ndugu ya mleta mada, Mada yako hapo jui imekaa vizuri tu ila ukimjibu Ben hapa umeharibu tayari. Huwezi kukitetea chama na wakati huo huo ukataka kuonyesha madhaifu yake, badala yake wewe ndio utaonekana Dhaifu....!!

Hivi unawezaje ukatangaza nia ya kutaka jimbo,Kata au Urais halafu ukakaa kwenu na wanao?? Mtuanayetangaza kukitaka kitu hususani nafasi ya uongozi lazima aonyeshe kwamba kweli anaihitaji kwa vitendo. Huwezi ukaruhisu watu kutangaza nia na wakati huohuo ukawazuia kujinadi ni ujinga, Wananchi watamjuaje basi maana sharti anayetaka hiyo nafasi ajionyeshe kivitendo na kwa maneno. sasa wewe unataka kumdanganya nani hapa

BACK TANGANYIKA
 
Mwigulu, chapa mwendo na mikutano yako asikutishe mtu. Maadamu unayo kofia tatu, wewe badili mtindo. Moja: Vua kofia ya chama (CCM) na uvae kofia ya serikali (maana wewe ni waziri). Mbili: Ikishindikana kabisa vaa kofia ya ubunge na usonge mbele. Wasikuhadae huku wengine wakiachwa kuendelea kujiimarisha. Elewa kitu na kitu kisikuelewe.
 
Kunahaja ya kufanya utafiti hapa hivi ni chama ndicho kinachoharibu watu au watu ndio wanaoharibu hiki chama. Maana mtu anaweza kuwa mzuri mwenye hoja makini, lakini akianza tu kujinasibisha na hiki chama lazima Akengeuke sijui ni kwanini..?

Sasa ndugu ya mleta mada, Mada yako hapo jui imekaa vizuri tu ila ukimjibu Ben hapa umeharibu tayari. Huwezi kukitetea chama na wakati huo huo ukataka kuonyesha madhaifu yake, badala yake wewe ndio utaonekana Dhaifu....!!

Hivi unawezaje ukatangaza nia ya kutaka jimbo,Kata au Urais halafu ukakaa kwenu na wanao?? Mtuanayetangaza kukitaka kitu hususani nafasi ya uongozi lazima aonyeshe kwamba kweli anaihitaji kwa vitendo. Huwezi ukaruhisu watu kutangaza nia na wakati huohuo ukawazuia kujinadi ni ujinga, Wananchi watamjuaje basi maana sharti anayetaka hiyo nafasi ajionyeshe kivitendo na kwa maneno. sasa wewe unataka kumdanganya nani hapa

BACK TANGANYIKA

Ha ha ha Mkuu! ......!
 
Sasa mtu ambaye hajatangaza nia utamhukumuje kuwa anafanya kampeni ya kujitangaza.Hivi wananchi wakibeba mabango kumtaja Rais inakua kosa?Mbona tunanyang'anya watu haki ya kikatiba yaani freedom of expression?
Kwa mara ya kwanza nikupe big up kwa kusema jambo la sawasawa...
 
makubwa tena haya, naona mtifuano umekaa mahali pazuri sana sana, yetu macho

Adui muombee njaa..,uongo..!!!

Binafsi nilishajipambanua kuwa mimi ni mtu wa kizazi kipya, nchi hii imefika hapa ni kwa sababu ya aina ya ufikiri na utendaji ambao hauendani na mazingira ya siasa ya sasa.

Popote ninapokuwa ninaungana na yule mwenye fikra mpya, fikra changa zenye kushabihiana na mazingira na changamoto za sasa. Nilifanya hivyo nikiwa chadema na nikaungana na Zitto ambaye alikuwa anataka kuleta mabadiliko ya kiutendaji na uratibu ndani ya taasisi hiyo ambayo ilishindwa mpaka wakati huo kujibainisha kama chama cha siasa, wakabaki katika harakati ambazo hazikuwa na tija.

Niko CCM bado ninayo spirit hiyo, nikamuona na kuvutiwa na siasa ya Mwigulu, ya kutoogopa kusimamia kweli na haki hata kama kwa kufanya hivyo kunahatarisha nafasi yake..lakini nafasi na hadhi ninkut gani mbele ya utetezi wa haki ya mtanzania masikini, mnyonge wa nchi hii.

Nitaendelea kupambana, na kuhakikisha kizazi chetu kinapata uongozi sahihi wenye maarifa yanayoendana na changamoto za sasa.
 
Mwigulu, chapa mwendo na mikutano yako asikutishe mtu. Maadamu unayo kofia tatu, wewe badili mtindo. Moja: Vua kofia ya chama (CCM) na uvae kofia ya serikali (maana wewe ni waziri). Mbili: Ikishindikana kabisa vaa kofia ya ubunge na usonge mbele. Wasikuhadae huku wengine wakiachwa kuendelea kujiimarisha. Elewa kitu na kitu kisikuelewe.

"..Elewa kitu na kitu kisikuelewe.." ndivyo asemavyo masaningala wa JF.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom