Barua ya Kighoma Malima kujiuzulu, amlaumu Kikwete

Barua ya Kighoma Malima kujiuzulu, amlaumu Kikwete

Mema yepi, ebu tukumbushe mkuu. Au unazungumzia kujenga misikiti kwenye kila shule ya serikali?
akiwa mipango ndo alipanga na kusimamia mpango wa mageuzi ya kisiasa na kiuchumi(structural adjustment programe),ndiyo yalizaa mfumo wa soko huria na mfumo wa kisiasa wa vyama vingi,lilikuwa agizo la wordbank.

Na kwakuwa siasa ya ujamaa ilikuwa imeua uchumi wa nchi pia alipanga na kusimamia mpango wa National economy recovering programme.
By recovering hapa waka initiate kubana matumizi,safari za nje zikaminywa,watumishi walipunguzwa pamoja na kuanzisha costsharing katika huduma za elimu na afya,
huo ndo ukawa mwanzo wa kujinasua kutoka katika uchumi wa kufunga mkanda uliokuwepo baada ya vita vya uganda.
Malima alikuwa kwenye cabinet toka miaka ya 1981
 
Kwa hiyo hata uwakilishi uliukosa?

Na washawasha!

ha ha ha ha
wapi ndugu yangu, ni jazba za kuilipenda Taifa langu mkuu. Ila hali ya huyo binti baada ya kurudi kutoka UK haikuwa kama alivyotoka.

Ndoa yenyewe ilikua kwa kuwakilishwa si unajua dini yetu inaruhusu mtu kusimama badala ya mtu katika kuweka ahadi ya ndoa!!!!
 
Napata picha kwamba JK alikuwa akitekeleza maamuzi fulani kutoka kwa wakubwa, ambao hawakuridhishwa na mienendo ya RIP Malima. Nahisi kwamba TISS ya wakati ule ilikuwa ikimfuatilia kimya kimya profesa huyu.

JK kwa sababu alishakuwa na ambitions za muda mrefu mbeleni, akawa tayari kujitoa mhanga, ili wasifu wake na heshima yake, viwe ni vitu vya kumbeba mbele ya macho ya wakubwa wa CCM enzi hizo.
 
Prof. angekuwepo hadi leo sijui hali ingekuaje. Maana jamaa alikuwa mdini aliyepindukia Lipumba ni cha mtoto.
Rejea kitabu cha Dr. Sivaron kinachoitwa Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania bara utajuwa nani mdini na nani sio mdini
 
Jk ni Mwanasiasa na hiyo ndio ilikuwa Kick yake 1995 mpaka akaingia 3 bora ya Mbio za Urais kwa kuwa alionekana ni Mwanasiasa Jasiri ( alikuwa na Miaka 5 tu Kama Waziri akiwa na Miaka 45) kumtuhumu Mwanasiasa Kama Prof Kighoma Tena wa Enzi zile

Prof Malima alikuwa Mjenzi mzuri sana wa hoja lakin tusisahau Jk alikuwa anasoma Majibu ya CAG sio Mawazo yake

Zile zilikuwa Figisu za Mbio za Urais 1995 huku ikionekana Prof Malima alikuwa na nia ya Urais!

Kwny Siasa zetu kuonesha Nia ya kuwania Urais ni Changamoto sana


Kwa haraka haraka naweza kusema Jk ndio Waziri Pekee wa Fedha kwa zaid ya Miaka 20 aliyetoka pale Hazina bila ya Msuko suko

Kighoma Malima, Wizara ya Fedha ndio chanzo cha kupotea

Prof Simon Mbilinyi 1996 Wizara ya Fedha ndio chanzo cha kupotea kisiasa

Daniel Yona na Mramba Wizara ya Fedha ndio chanzo cha Matatizo ya kufungwa yaliyomkuta

Zakhia Hamdani Meghji Wizara ya Fedha ndio chanzo cha kupotea 2007

Mustapha Mkulo Wizara ya Fedha ndio iliyosababisha akapotea

William Mgimwa Wizara ya Fedha ndio ilipelekea Kifo chake

Jk ndio pekee kafanikiwa kutoka Treasury na kuendelea na Siasa zake Tangu 1990!
Ni kweli ila hakukaa muda mrefu ,muda mfupo aliokaa pale alionyesha kumudu...na alikuwa kijana mjamaa...machachari wakati huo ambaye alifurahisha wazee kama Mwalimu kwa...kujinasibu kuwa.mfuasi wa ujamaaa ..na ndio maama akawapiga nyundo...kina Malima ..pamoja na..kuwa..inside alikuwa na malengo...ya kumuondoa malima kama kiongozi...mashuhuri toka ukanda huu...ambayo ni..muhimu sana kwenye mbio.za.urais
 
Nchi hii kuna master Strategists wakubwa wawili tu katika siasa
1. JK
2. EL

Wengine ni wanasiasa "mfumo", yaani mfumo unadictate their political fate, bahati ikiwa upande wao sawa, isipokuwa kwao sawa
 
Ndiyo hapo napojiuliza. Kabla ya Kighoma kuna jamaa yangu alitumia namba kwenye mtihani. Leo tunaambiwa Kighoma Malima ndiye aliyeanzisha namba!!
Hayo ni ushabiki tu. Kama mtu amefeli shule hakuna namna. By the way mke wa ndoa wa Marehemu Malima alikuwa mkristu na hajabadili dini mpaka kesho
 
Bond ya Slaa na Mbowe iliimarika 2007 na ilitengenezwa kwa Kazi ya kupambana na Lowassa bila ya wao kujijua na ilipomalizika kazi ile bond ikavunjwa bila ya kutegemea!



Kama wangeamua Slaa, Mbowe na Lowassa na kundi Lao la kina Rostam kumkazia Jk 2010 Basi moto ungewaka lakin ndo hivyo the Rest is history

Vita ni akili na Mipango

Alisaidia Makundi yote hasimu ndani ya Chama kuwapa nguvu kwa kuwapa Nyadhifa nyeti ili Mgogoro uchelewe kuisha ili yeye atumie Muda huo kujiimarisha na kupanga safu Mpya

Mzee Kingunge, Sophia Simba, Dkt Nchimbi walipewa Mashavu kwa upande wa Kambi ya Lowassa

Akina Mwakyembe, Sitta, Benard Membe nao wakawa wanapewa Mashavu ili wasidhoofike

2007 alimtumia Sitta na Chadema kumchomoa Lowassa kwny Uwaziri Mkuu

2010 akamtumia Lowassa kumchomoa Sitta kwny U Spika

2011 alipovuka salama kwny Uchaguzi wa 2010 akampa Siku 90 Rostam ajiuzulu Siasa kwa style ya Kujivua gamba Muhindi akatii order

Akaunda Kamati ya Kina Mzee Mwinyi eti kusuluhisha Mgogoro kuzuga tu

Baada ya Makundi kudhoofisha vya kutosha akamchomoa Wilson Mukama na kumteua Comrade Kina a na kuanza kuunda kikosi cha Ushindi 2015 akijumuisha kina Nape

2015 Lowassa akachinjwa, Sitta akachinjwa, Benard akachinjwa

Timu ya Lowassa ingekuwa Makini Siku ile Lowassa kachinjwa na wangefuata Maelekezo ya Mzee Kingunge pale St Gasper Basi Chama Hata Kama kisingeshindwa Basi Majeraha yangekuwa Makubwa zaid lakin wakapuuza wakashika ushauri wa Kina Nchimbi Wazee WA Mihemko

Quite interesting and plausible analysis. But I find no joy in watching these kinds of games. The most sad thing: it makes me wonder exactly where do we place Tanzanians in this sort of schema? If not mere pawns then just a bunch of zombies in a nasty game of wits played by mafia-like characters in their name! Sounds insulting to our collective intelligence.

People could try to celebrate the moves of the chess masters but then, the consequences to the nation are sinister.

Haya ndiyo mambo yanayonifanya nisipatane kabisa na siasa za kushabikia watu na vyama uchwara vya siasa tulivyo navyo nchini mbavyo imekuwa nadra sana kuona ueledi wa kiitikadi ndani yao zaidi ya ushabiki wa kimichezo huku mwelekeo wa nchi ukiendelea kuwa ovyo tu. Nimetoka kusikiliza uchaguzi wa Iran na kuona jinsi tulivyo pembeni kabisa kidemokrasia (wala sio nyuma).
 
..siyo mjanja kiasi hicho.

..mengi ameyafanikisha kwasababu vyombo vya DOLA viko nyuma yake.

..lingine ni kwasababu kama Raisi ana vyeo na nafasi nyingi mno anaweza kuvizigawa kwa yeyote yule ambaye analeta kilomolomo na akatulia.

..wapinzani ndiyo wagumu sana kuwaongoza. Hakuna aliyemzidi mwenzake na ndiyo maana ukasikia Juma Duni akidai ndani ya CDM kila mtu ni "kambale."
Unashuka nondo kali sana kama kawaida yako
 
Nimeisoma hiyo barua na nimevuta kumbukumbu ya Malima Enzi zile pamoja na homeboy wake JK na mwishoni nimeendelea kuamini vile vile nilivyokua najua kuhusu Kighoma Ali Malima kwamba wanao mtetea wengi ni kwasababu ya dini yake tu but huyu nae ni miongoni mwa maprofesa wa hovyo walio wahi kutokea nchini. Kwenye wizara zote alizopitia alivurunda. Kwangu mimi sina la maana la kujifunza from this guy. Alale salama mahali panapomtastahili.
Hovyo is the best word...hana legacy yoyote ya kujenga Tanzania wala utanzania
 
kwa mjibu wa barua,Malima hakuwa mfanyabiashara,
alikuwa mfanyakazi,na kaeleza kuwa aliufuta utaratibu wa wafanyabiashara kuingiza bidhaa na kulipa kodi kwa awamu,
sasa yeye malima kaingiza gari mbili kama mfanyakazi na kama walivyofanya mawaziri wote akawa analipa kwa awamu kutoka katika mshahara wake,

inaonekana mdhibiti mkuu wa hesabu alichanganya mambo,
Kwa enzi zile hela nje ya nchi alitoa wapi na yeye hakuwa mfanyabiashara?
 
Wakati malima anakamata wizara ya fedha mwaka 1994,ilibidi aitishe min burdget kwani kipindi alikuta makusanyo ya kodi yako hoi,
serikali inakusanya bilion 200 kwa mwezi wakati matumizi ni bilion 500,
ilibidi aanze kufuta misamaha ya kodi kwa makampuni mbalimbali ili ipatikane pesa ya kuendesha serikali kwa miezi 6 kufikia bajeti mpya ya 94/95.
Kibona alikuwa kaprove failure ,
lakini reform ya malima itakuwa haikumfurahisha boss,maana baada ya kuanza kufuta misamaha ya kodi,rais akaondoa mamlaka ya kusamehe kodi toka kwa waziri wa fedha na kupelekwa kwenye tume ya uwekezaji,

baadae mwaka huohuo malima alihamishiwa wizara ya viwanda na biashara hadi anaachia ngazi
I don't think unachosema ni sahihi....Rais kuchukia kuondolewa misahama ya kodi? Without being abused?
 
Hayo ni ushabiki tu. Kama mtu amefeli shule hakuna namna. By the way mke wa ndoa wa Marehemu Malima alikuwa mkristu na hajabadili dini mpaka kesho
Ni kweli kabisa Ndahani, yule Mama alikuwa rafiki mkubwa wa Marehemu Mama yangu. Walikuwa wafugaji wa mwanzo mwanzo wa jiji la Dar miaka ile ya 1980.
 
Kwani tukisema Wahalifu waliua Askari wetu Mkuranga maana yake wale Vijana wasingekuwa Askari wasingekufa?,

Ila bado ni sahihi kusema waliuawa kwa kuwa ni Askari otherwise wasingeuawa

Tukisema Urais wa znz ndio ulimuua Abeid Karume ni sahihi japo si lazima iwe hivyo
Pohamba, sasa sisi wakulima kwanini tunakufa?
 
Acha kukurupuka!

Nimezungumzia u Prof wake kwa kuwa umekejeliwa u Prof wake!

Halafu inaonekan Mweupe sana Kichwani ndio sababu unadhani kila anachotangaza Waziri Basi ni Msimamo binafsi wa Waziri ndio sababu unamlaumu Tena Prof Mbalawa na kumsifu JPM
Sawa Mimi mweupe. Na wewe mweusi kichwani kakojoe ukalale. Akili yako haiwezi kutafakari mistari na bahati mbaya ni mweusi kichwani kwelikweli. Kama hujui jambo kaa kimya badala ya kukosoa jambo usilo na taarifa nalo. Pia unaposoma jiongezee. Kengele zako.
 
Nashukuru kwa kumbukumbu hii. Nilikuwa mdogo sana wakati ule lakini walau nakumbuka kwa kiasi kujiuzulu kwa Prof. Kighoma Ali Malima. Nilikuwa nimesahau kisa hasa kilichopelekea ajiuzulu
 
Back
Top Bottom