Barua fupi kwa ndugu Maxence Melo huko katika kuta za magereza (sehemu 1)

Shukrani A. Ngonyani

JF-Expert Member
Feb 23, 2014
1,179
2,004
Ndugu Maxence,
Salaam,

Pole na hongera kwa kipindi hiki unachopitia, ni kipindi kigumu lakini ni kipindi cha kujenga ujasiri na kukokomaza kifikra na msimamo.

Ndugu Maxcence wakati wewe umelala ktk kuta nene na ndefu za magereza, kwa "kosa" la kuweka jukwaa la kutoa maoni, mawazo na habari kwa matakwa ya ibara ya 18(1-1V) ya katibu huku ,kuna Wenzako wanakula raha.

kuna wezi wa ESCROW wapo wamelala na wake zao, wezi wa IPTL wamelala na mahawara zao, waliotupiga pesa ya radar wamelala na vimada wao, huku wewe uliyeweka jukwaa la kufichua uovu huo ukiwa nyuma ya milango ya chuma na kuta nene za magereza.

Wengi tulitarajia na tulijua kuwa wale malaika wa kufungia mitandao ya kijamii wataangukia Jamiiforums.

Jitahidi Kuwa mvumilivu wakati huu ambapo "malaika" wanakushikilia huku "mungu" wao akiwa kimya kama hajui kinachoendelea huku ikifahamika malaika wametumwa na mungu.

Ndugu Mello, tafadhali upatapo barua yangu nakuomba tulia utafakari na utambua unapigana vita muhimu sana tena muhimu kuliko hata maisha na roho yako.

Unalinda uhuru wa kutoa mawazo, maoni na kupashana habari, hivyo si suala dogo, kuwa mvumilivu, kuwa mzalendo, unaipigania Tanzania, Tanzania ni muhimu kuliko roho yako. hata hao mawakala wakikuua usijali, damu yako itakuwa imetumika kama wino wa kuandikia maneno mawili, UHURU na UKOMBOZI.


Hakika unaumia na unateseka sana kwa unayopitia, usife moyo, ukifa moyo tutaumia wengi, ni bora uvumilie upweke wako na mateso yako huko gerezani.

Ndugu yangu Maxcence tafadhali pokea pole, shukrani na pongezi kutoka kwangu.

Jisikie uko nasi hapo ulipo!

salaam!

Shukrani Ngonyani
Lilongwe.
 
Ndugu Maxcence,
Salaam,

Pole na hongera kwa kipindi hiki unachopitia, ni kipindi kigumu na lakini ni kipindi cha kujenga ujasiri na kukokomaza kifikra na msimamo.

Ndugu Maxcence wakati wewe umelala ktk kuta nene na ndefu za magereza, kwa "kosa" la kuweka jukwaa la kutoa maoni, mawazo na habari kwa matakwa ya ibara ya 18(1-1V) ya katibu huku ,kuna Wenzako wanakula raha.

kuna wezi wa ESCROW wapo wamelala na wake zao, wezi wa IPTL wamelala na mahawara zao, waliotupiga pesa ya radar wamelala na vimada wao, huku wewe uliyeweka jukwaa la kufichua uovu huo ukiwa nyuma ya milango ya chuma na kuta nene za magereza.

Hakika unaumia na unateseka sana kwa unayopitia, usife moyo, ukifa moyo tutaumia wengi, ni bora uvumilie upweke wako na mateso yako huko gerezani.

Ndugu yangu Maxcence tafadhali pokea pole, shukrani na pongezi kutoka kwangu.

Jisikie uko nasi hapo ulipo!

salaam!

Shukrani Ngonyani
Lilongwe.
Akitoka kwa mello nani atafuata, huyu ni lazima adhibitiwe mapema kabla hajawa nkurunzinza original
 
Naomba taratibu za Kuwatembelea Mahabusu au Wafungwa huko Gerezani nione kama nitafanikiwa kuonana na Max.
 
Namshukuru Mungu kwa kua mmoja kati ya wananchi wa nchi pendwa Tanzania

Kuna mengi yametokea chini ya serikali yetu yakishinikizwa na wachache kwa maslai ya kulinda utawala wao na si vinginevyo.

MELO ni mpiganaji mkubwa sana mpaka leo kuna platform kibao humu ndani na ata wewe unaesoma umekua ni sehemu ya jamii ilioguswa na kinachomkuta MELO.

Mwalimu Julias k Nyerere alijitoa akaacha ualimu akasimama kma mpiganaji kwa ajili ya watanzania wote leo tunazungumza kiswahili fasaha na tunafurahia uhuru wa kuendesha mambo yetu wenyewe, kulipa kodi, kujenga, kumiliki na ata kumilikisha asset kwa wengine lakini yote haya kulikua na that one man aliyeona mbali na ndio maana FREEDOM!!.

JF imekua mahala pa wanyonge Wengi kuweza kupaza sauti zetu moja kwa moja tukiamini kuwa sauti zetu zitapenya na kuwafikia wausika sababu sisi ni watoto wa baba mmoja ndio maana wote tuna kovu la sindano begani na utaifa wetu umejengwa katika mantiki ya amani, upendo na usawa.


Kama mzee Nyerere alifanikiwa kufanya alichokifanya mpaka leo tupo hapa same apply to Maxence humu JF. Guys it has to reach a point where by tusilizike na hii hali tuwe watu wakureason vitu kwa fikra pana zaidi.

Kukaa kimya tuu na kuanza kuzipuuza hizi habari tutaishia kubaya na hatutapata lolote sisi ndio tutakaokua victim as in LOOSER in Double kwanza mwenzetu pili FREEDOM ya humu Jf

Guys kukaa Nyuma ya key board peke hakutoshi, tusimame kwa ajili ya mwenzetu tusimame kwa ajili ya mtandao wetu pendwa

Tunaweza fikisha ujumbe huu kwa namna nyingi as in phyisical lakini Twitter,Fb, na humu Jf haitosh kwani tuliipinga cyber act law tukashindwa sasa Leo tuko kimya ila hakuna asie ujua mwisho wetu.
 
wataalamu wa Sheria naomba muongozo wenu

Maxence ni mmoja wa wamiliki wa jamii media company, nijuavyo mimi kampuni ni legal person ikimaanisha kwamba inazaliwa, kukua na hata kufa, inashitaki na kushitakiwa, inadai na kudaiwa na mengine mengi, kwa limited liability company owners hawawajibiki moja moja Bali kampuni Kama legal person.

Na ikitakiwa owners kuwajibishwa basi kuna taratibu za kihamakama za Kuomba uwajibishwaji wa wamiliki, na kuomba ku lift corporate veil ambapo hapo Sasa mahakama itaruhusu ama kukutaa ku treat makosa, madeni n.k ya kampuni Kama makosa binafsi ya wamiliki. Mkumbuke hapa tuna watu wawili kampuni Kama Mtu wa kisheria na wamiliki ambao sheria ya makampuni inawatambua Kama watu tofauti.

Ninachotaka kufahamu ni lini basi mahakama iliruhusu ku lift corporate veil na kumuhushisha Maxence na makosa ya kampuni ya jamii media?

Pili, ni Haki kwa Maxence peke take kukwamatwa?wako wapi wamiliki wengine wa jamii media?hawahusiki?
 
Kwamba malaika wanazima mitandao na Mungu wao kakaa kimya tu akidhani haachi trace,,au alama zake hatuzioni..Nadhani angepaswa ajiulize hii ni miaka gani?? iliobeba watu wa aina gani?? Wenye mtazamo upi?? Na kwa nini atamani Mwenyezi azime mitandao then akaizima yeye??
 
Kweli tuko pamoja nae ktk kipindi hiki kigumu na hatuta rudi nyuma na tunaendelea kumwombea kwa Mungu kuwepo na urahisi wa kushinda.
 
Ameni,Mungu atutetee sisi tusiokuwa na hatia kwa hii serikali,lakin pia wale wanotesa na kunyanyasa wengne wapewe adhabu kama wanavostahili.
 
Hizi nguvu angezielekeza kwa wezi wa mali za umma kama eskrow,iptl,meremeta,richmond nk nchi ingepata manufaa makubwa sana
Hizi nguvu angezielekeza kwa wezi wa mali za umma kama eskrow,iptl,meremeta,richmond nk nchi ingepata manufaa makubwa sana
Ajabu yake hao wezi ESCROW, RADA, IPTL NA MEREMETA wapo bungeni wanatunga sheria kandamizi zinazo muweka ndani Maxsence Melo!
Walaaniwe wote wanao nyanyasa na kudhulumu na kuonea Wafichua maovu Tanzania!!
 
Back
Top Bottom