Barclays imeinunua Benki ya Taifa ya Biashara (NBC)?

Barclays imeinunua Benki ya Taifa ya Biashara (NBC)?

hapa gavana inabidi atuelezee vizuri inakuwaje makampuni yaendeshe account zao kutokea south Africa? kuna siku nilitaka bank statement kutoka stanbic nilizungushwa kama week nilivyokomaa nikaambiwa haijatumwa kutoka south Africa kwa hasira nikafunga account yangu stanbic hadi wa leo sinao hamu tena.

haya makampuni ya kigeni kushika njia kuu za uchumi hapana inabidi lifanyiwe kazi lazima economic hub zote ziendeshwe na state au local companies. hengera kwa tpdc kuanza utafiti wa mafuta yenyewe badala ya kutegemea wawekezaji.

Nimelipenda hitimisho lako lkn it's too late now, NBC ilikuwa bank muhimu sana kwa uchumi wa nchi,bahati mbaya sana tuliongozwa na viongozi wa.pu.mbavu sana waliosababisha yote haya kwa tamaa zao za fedha. Natamani tungempata Magufuli baada ya Mwinyi haya yote yasingetokea,alaaniwe Mkapa.
 
Acha uongo, taarifa za NBC zipo kitambo humu jamvini. Tafuta uzi wa Katibu wa Mwl.Nyerere ili ujue ni kwa kiasi gani Mwl..alikerwa na nkapa kuuza NBC.

Ni kweli Nyerere alikerwa na aliumia sana hata mimi najua hivyo. Lakini nasema tena kuwa alikuwa hana sababu ya kukerwa kwani NBC iliundwa kutokana na mabenki binafsi yaliyotaifishwa mwaka 1967 yakiwemo Barclays' Bank, Standard Bank, Bank of Baroda, National Grindlay's, etc. Kwa hiyo NBC ilikuwa ni benki feki iliyoendeshwa na watu ambao hawakuwa na uchungu wala utalaamu wa maana wa kuendesha benki. Baadaye ilikuwa ni kichaka cha serikali kujichotea pesa kadiri inavyotaka.
 
Ni kwamba Barclays imeinunua ABSA ya Afrika kusini ambayo ndio kampuni mama iliyoinunua NBC ngoja niitafute link nikuwekeeni hapa jamvini
 
Ni kweli Nyewrere alikerwa na alimumia sana hata mimi najua hivyo. Lakini nasema tena kuwa alikuwa hana sababu ya kukerwa kwani NBC iliundwa kutokana na mabenki binafsi yaliyotaifishwa mwaka 1967 yakiwemo Barclays'Bank, Standard Bank, Bank of Baoda, National Grindlay's, etc. Kwa hiyo NBC ilikuwa ni bemki feki iliyoendeshwa na watu ambao hawakuwa na uchungu wala utalaamu wa maana wa kuendesha benki. Baadaye ilikuwa ni kichaka cha serikali kujichotea pesa kadiri inavyotaka.

Mwl.Nyerere hakufanya pupa kutaifisha hayo mabenki. Ilichukua muda mrefu kuchunguza hata kuyataifisha. NBC ilikuwa miongoni mwa benki zilizofanya vizuri. Inasemekana, Mwl.aliposikia NBC inauzwa kwa masharti ya WB na IMF, aliwauliza watu wa WB na IMF. Taarifa zinasema WB na IMF walikanusha kuhusika na NBC.

Wazushi wanasema, eti hapo ndipo timbwili timbwili na prezidaa ndipo lilipoanzia. Hatimaye Mwal. akaenda UK "kupimwa" afya yake; lakini akarudi maiti.

Hizo ni taarifa za vijiweni, wala hatuziamini, ila zinasemwa.
 
Mwl.Nyerere hakufanya pupa kutaifisha hayo mabenki. Ilichukua muda mrefu kuchunguza hata kuyataifisha. NBC ilikuwa miongoni mwa benki zilizofanya vizuri. Inasemekana, Mwl.aliposikia NBC inauzwa kwa masharti ya WB na IMF, aliwauliza watu wa WB na IMF. Taarifa zinasema WB na IMF walikanusha kuhusika na NBC.

Wazushi wanasema, eti hapo ndipo timbwili timbwili na prezidaa ndipo lilipoanzia. Hatimaye Mwal. akaenda UK "kupimwa" afya yake; lakini akarudi maiti.

Hizo ni taarifa za vijiweni, wala hatuziamini, ila zinasemwa.

Benki ya NBC ilikuwa inafanya vibaya tokea miaka ya 80. Tatizo mojawapo lilikuwa ni kuingiliwa na serikali hasa utoaji wa mikopo kwa vyama vya ushirika na bodi za mazao. Sababu nyingine ilikuwa ni uendeshaji mbaya. Kwa vile ilikuwa ndiyo benki pekee ilikuwa na wafanyakazi wenye kiburi, wavivu na wazembe. Mwaka 1990 serikali ilishauriwa na Presidential Banking Commission ya Mr. Nyirabu iivunje hiyo benki ili kupata benki ndogondogo lakini serikali ilisita na kuamua kupeleka madeni fulani ya NBC LART, kupunguza wafanyakazi 2,800 na kufunga branches 23. Hiyo haikusaidia. Mambo yakazidi kuwa mabaya.

Siwezi kusimulia yote lakini ni vyema tu ukweli uwekwe wazi. Nyerere alilia kwa vile yeye alikuwa ni mjamaa kwelikweli. Kuna watu ng'ombe akivunjika mguu atamfungilizia miti hata kwa mwaka mzima kuliko kumuua auze nyama. Mwishoni ng''ombe huyo hufia porini.
 
Uuuzwaji wa NBC ulimtoa Mwl. machozi. By the way, ni kwanini NMB kabenki kanokadaiwa ka mafukara ambako ni katawi kalikomegeka kutoka giant NBC inafanya vizuri wakati li-giant linakufa kifo cha mende? Tatizo ni menejimenti? Au ni kitu gani?

Mkubwa mbona hata hiyo NMB waholanzi wamejaa kuanzia juu, sidhani kama tutaendelea kua na benki ya Taifa tena.

wacha upotoshaji, kuna waholanzi wnagapi huko?
je wajua major share holder hapo ni rabobank ya uholanzi ?

Unajua maana ya upotoshaji? Hapo nilikua najbu suala la management kwamba huko NMB inaongozwa na Waholazi, na sio kweli kwamba NMB bado ni benki ya makabwela au benki ya serikali tena, kwa sababu hiyo Rabobank ya waholanzi inamiliki share nyingi. Nimepotosha wapi?
 
Benki ya NBC ilikuwa inafanya vibaya tokea miaka ya 80. Tatizo mojawapo lilikuwa ni kuingiliwa na serikali hasa utoaji wa mikopo kwa vyama vya ushirika na bodi za mazao. Sababu nyingine ilikuwa ni uendeshaji mbaya. Kwa vile ilikuwa ndiyo benki pekee ilikuwa na wafanyakazi wenye kiburi, wavivu na wazembe. Mwaka 1990 serikali ilishauriwa na Presidential Banking Commission ya Mr. Nyirabu iivunje hiyo benki ili kupata benki ndogondogo lakini serikali ilisita na kuamua kupeleka madeni fulani ya NBC LART, kupunguza wafanyakazi 2,800 na kufunga branches 23. Hiyo haikusaidia. Mambo yakazidi kuwa mabaya.

Siwezi kusimulia yote lakini ni vyema tu ukweli uwekwe wazi. Nyerere alilia kwa vile yeye alikuwa ni mjamaa kwelikweli. Kuna watu ng'ombe akivunjika mguu atamfungilizia miti hata kwa mwaka mzima kuliko kumuua auze nyama. Mwishoni ng''ombe huyo hufia porini.

Umenifungua macho! Shukurani.
 
Ni kweli Nyerere alikerwa na aliumia sana hata mimi najua hivyo. Lakini nasema tena kuwa alikuwa hana sababu ya kukerwa kwani NBC iliundwa kutokana na mabenki binafsi yaliyotaifishwa mwaka 1967 yakiwemo Barclays' Bank, Standard Bank, Bank of Baroda, National Grindlay's, etc. Kwa hiyo NBC ilikuwa ni benki feki iliyoendeshwa na watu ambao hawakuwa na uchungu wala utalaamu wa maana wa kuendesha benki. Baadaye ilikuwa ni kichaka cha serikali kujichotea pesa kadiri inavyotaka.

Je! Sasa tuna benki yoyote ya umma?
 
Barclays ndo ilinunua ABSA ambayo ilikuwa inamiliki majority shares NBC.

The Barclays Africa Group Limited (JSE: BGA), also known as Barclays Africa or the Group, formerly Absa Group Limited, is a South African subsidiary of Barclays; it is a financial services provider, offering personal and business banking, credit cards, corporate and investment banking, wealth and investment management as well as bancassurance. ABSA stands for "Amalgamated Banks of South Africa", and is a wholly owned subsidiary of ABSA Group Limited.[SUP][4][/SUP]

Oh yeah I got the otherway round, Coz mpaka leo South Africa Baclays ina signatures za ABSA ndo maana It gets to confuse me Who bought who...nimeelewa now.
 
mkuu asante kwa hapo kwenye red, nimejifunza kitu. ila usijeukawa umedanganya.

Mkweli mtupu mkuu haya mambo mbona yako wazi ni kuconnect dots tu ingia hata kwenye website ya Barclays soma historia yake Tz
 
Hii nimeiona kwenye changes za banking system ya NBC maana wamekuwa paperless na risiti zinafanana na zile za barclays
 
Je! Sasa tuna benki yoyote ya umma?

Kwa maana ya umiliki wa Serikali zipo nazo ni Twiga Bancorp, TIB Development Bank, TIB Corporate Bank, Bank ya Wanawake, TPB, Bank ya Maendeleo ya Kilimo na kwa upande wa Zanzibar kuna PBZ ambayo inamilikiwa na serikali ya mapinduzi.
 
Back
Top Bottom