Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Uzoefu wa toka JK ameingia madarakani vijana waliobahatika kupewa uwaziri wamegeuka kuwa genge la majizi na wahujumu uchumi. Lau Masha, Wiliam Ngeleja, Ezekiel Maige, Cyril Chami, Adam Malima, na wengine wametufanya tuamini kuwa vijana wa sasa hawajalelewa katika maadili mema ya uadilifu. Wanaiba wake za watu, wanatembea na wanafunzi, walevi kupindukia huku wizara zao zinaongoza kwa utendaji mbovu na hakuna ufanisi. Mfano wizara ya Ngeleja mgao wa umeme toka ameingia madarakani.
Mimi mtazamo wangu vijana wasipewe uwaziri, wachache wapate unaibu ili tuwachunguze kama wanaweza kuongoza na hawana tamaa. Mimi pia ni kijana lakini naona dhahiri vijana waliopo katika wabunge wa CCM hakuna msaada, wote ni majizi yanayotafuta vijiwe vya kufanyia uhalifu.
Nawakilisha...
Mimi mtazamo wangu vijana wasipewe uwaziri, wachache wapate unaibu ili tuwachunguze kama wanaweza kuongoza na hawana tamaa. Mimi pia ni kijana lakini naona dhahiri vijana waliopo katika wabunge wa CCM hakuna msaada, wote ni majizi yanayotafuta vijiwe vya kufanyia uhalifu.
Nawakilisha...