Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Kumbukumbu zangu zinaonyesha kwamba JK aliingia madarakani akiwa anaungwa mkono na kundi kubwa la vijana. Naye alipoingia madarakani hakuwatupa mkono vijana. JK aliwateua vijana lukuki kwenye Baraza lake la Mawaziri; wengi wakiwa ni manaibu waziri. Ndani ya safari, akaja kuwapandisha wengi wao kuwa mawaziri kamili: William Ngeleja alipandishwa kushika uwaziri wa Nishati na Madini, Lawrence Masha akachukua uwaziri kamili wa Mambo ya Ndani, Dr. Emmanuel Nchimbi akachukua wizara ya Vijana Utamaduni na Michezo, Ezekiel Maige akachukua Uwaziri kamili wa Maliasili na Utalii na Dr. Cyril Chami naye akautwaa Uwaziri kamili wa Viwanda na Biashara.
Kwenye safari yake ya miaka kumi ambayo haijafika mwisho, JK tayari amewaacha baaadhi ya vijana njiani kwa wao wenyewe kushindwa kutekeleza majukumu aliyowakabidhi hadi umati ukapiga kelele.
Masha alishindwa Ubunge japokuwa watu walikuwa wakipigia kelele utendaji wake. Imekuja hii kubwa ya hawa wa sasa kwamba wamewajibishwa kwa kushindwa kusimamia wizara zao/Ufisadi.
Mimi ni muumini wa vijana kupewa madaraka kwa kuwa bado wana nguvu na wanaweza kuhimili misukosuko. Lakini naona akina Ngeleja, Maige na Chami wameshindwa kuwatendea haki vijana wenzao ambao waliwategemea wao kuwa mfano wa kupigiwa chapua. Wameshindwa kutenda kufikia matarajio ya wananchi wakiwa bado vijana mno.
Nashindwa kuelewa hatima yao ya kisiasa. Kwa umri wa hawa vijana kuondolewa kwenye uwaziri kwa sababu za ufisadi/uwajibikaji ina maana hawana nafasi tena ya kuweza kuwa mawaziri!
Nimpe hongera Dr. Comrade Emmanuel Nchimbi manake naona tangia ameingia serikalini nyota yake imekuwa iking'ara na sasa amekabidhiwa roho za Watanzania; Niamini tu kwamba atatutendea haki na si vinginevyo.
Pamoja na hao kumwangusha lakini naona JK bado ana imani na vijana. Sasa amewaleta akina January, Masele na Simbachawene. Ummy Mwalimu naye amekabidhiwa dhamana ya kuingia kwenye mikutano ya Baraza la Mawaziri. Comrade Nchimbi amekabidhiwa roho za watanzania ambalo ni jukumu zito hasa katika changamoto za sasa za kisiasa. Basi na ninyi vijana mlioingia ama kubakishwa basi msimuangushe tena. Fanyeni kazi kwa uadilifu Tanzania ya sasa si ya mwaka 47 ni ya dot.com mnamulikwa na kila mtu.
Tunasemaje?
Kwenye safari yake ya miaka kumi ambayo haijafika mwisho, JK tayari amewaacha baaadhi ya vijana njiani kwa wao wenyewe kushindwa kutekeleza majukumu aliyowakabidhi hadi umati ukapiga kelele.
Masha alishindwa Ubunge japokuwa watu walikuwa wakipigia kelele utendaji wake. Imekuja hii kubwa ya hawa wa sasa kwamba wamewajibishwa kwa kushindwa kusimamia wizara zao/Ufisadi.
Mimi ni muumini wa vijana kupewa madaraka kwa kuwa bado wana nguvu na wanaweza kuhimili misukosuko. Lakini naona akina Ngeleja, Maige na Chami wameshindwa kuwatendea haki vijana wenzao ambao waliwategemea wao kuwa mfano wa kupigiwa chapua. Wameshindwa kutenda kufikia matarajio ya wananchi wakiwa bado vijana mno.
Nashindwa kuelewa hatima yao ya kisiasa. Kwa umri wa hawa vijana kuondolewa kwenye uwaziri kwa sababu za ufisadi/uwajibikaji ina maana hawana nafasi tena ya kuweza kuwa mawaziri!
Nimpe hongera Dr. Comrade Emmanuel Nchimbi manake naona tangia ameingia serikalini nyota yake imekuwa iking'ara na sasa amekabidhiwa roho za Watanzania; Niamini tu kwamba atatutendea haki na si vinginevyo.
Pamoja na hao kumwangusha lakini naona JK bado ana imani na vijana. Sasa amewaleta akina January, Masele na Simbachawene. Ummy Mwalimu naye amekabidhiwa dhamana ya kuingia kwenye mikutano ya Baraza la Mawaziri. Comrade Nchimbi amekabidhiwa roho za watanzania ambalo ni jukumu zito hasa katika changamoto za sasa za kisiasa. Basi na ninyi vijana mlioingia ama kubakishwa basi msimuangushe tena. Fanyeni kazi kwa uadilifu Tanzania ya sasa si ya mwaka 47 ni ya dot.com mnamulikwa na kila mtu.
Tunasemaje?