Barabara Dar kwenda Chalinze kuwa ya kulipia

Barabara Dar kwenda Chalinze kuwa ya kulipia

tamimusalim

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
1,822
Reaction score
499
ImageUploadedByJamiiForums1411555938.450699.jpg ImageUploadedByJamiiForums1411556185.439800.jpg

Serikali inafikiria kuipa sekta binafsi barabara Dar kwenda Chalinze kuijenga upya ,kwa mujibu ya muheshimiwa Omari Issa anayehusika na uwezeshaji na utekelezaji ofisi ya rais kama alivyoongea na kituo cha ITV katika kipindi cha dakika 45, alisema sekta iyo binafsi itapewa dhamana ya kukusanya pesa kwa magari yatakoitaji kupita katika barabara iyo ya kisasa itakayojengwa.
 
afadhali, kuliko kale kanjiwa pori kila wakati ajali au masaa 6 toka chalinze hadi mbezi
 
hawa wez kila lita 1 inatozwa shs 200 kwa ajili ya barabara, je wametengeneza zipi?
je kod zetu zinalipia nn..
hii nchi hii tutakuja kuonana wabaya.
oya hiyo uliyoshika mkononi hauna ya ziada nyumba tuwafanyie hawa watu...
 
barabara hii imeharibiwa na malori,inadidimia kila siku,pale mailimoja litakuwa bwawa la maji mda si mrefu inavyotitia kwa kasi kwenda chini!ccm oyee
 
There is a secret behind the move, wakishindwa kuendesha mradi ndipo unasikia Serikali inakusudia kupunguza viwango vya pensheni kwa wafanyakazi wake - wizi mtupu
 
View attachment 187854 View attachment 187856

serikali inafikilia kuipa sekta binafsi barabara Dar kwenda Chalinze kuijenga upya ,kwa mujibu ya muheshimiwa Omari Issa anayehusika na uwezeshaji na utekelezaji ofisi ya rais kama alivyoongea na kituo cha ITV katika kipindi cha dakika 45, alisema sekta iyo binafsi itapewa dhamana ya kukusanya pesa kwa magari yatakoitaji kupita katika barabara iyo ya kisasa itakayojengwa.

Kwanza kutakuwa na adha kubwa ya usafiri toka ubungo mpaka chalinze kwa sababu makandarasi , serikali na maconsultants hawaonyeshi kujali watumiaji wa barabara kama tulivyoonyeshwa na DART.
Pili, serikali ilipashwa kuwa imeshatenga maeneo ya ujenzi kwa maana ya road reserve na siyo kuanza kukimbizana na wananchi mahakamani wakati mkandarasi amepewa kazi. Serikali iwe imemalizana na wananchi waliovamia au kupewa maeneo kando ya barabara.
Tatu, ili watumiaji wa barabara waje kulipia, road toll katika mafuta iondolewe.
Nne, nahitimisha nadhani hii bado ni mipango ya kufikirika tu mpaka tuone kweli. Isije kuwa ni porojo za kampeni tukaletewa ujinga kama wa DART. Poor design kiasi kwamba ni nyembamba mno,ina foleni zisizoisha, ina matuta kila kituo, stendi ziko katikati ambapo ni hatari kwa watembeao kwa miguu. Mambo ya kiabunuasi kwa gharama za pesa za wananchi au madeni.
 
hawa wez kila lita 1 inatozwa shs 200 kwa ajili ya barabara, je wametengeneza zipi?
je kod zetu zinalipia nn..
hii nchi hii tutakuja kuonana wabaya.

Imagie ni liter ngapi Zinazo uzwa kwa siku mara 200... Kwa kweli kua hela nyingi zinapotea hivi hivi
 
hatutaki poroje atuambie mradi umefikia wapi utaanza lini na utaisha lini
Au ndo harakati za uchaguzi hizi
 
View attachment 187854 View attachment 187856

Serikali inafikiria kuipa sekta binafsi barabara Dar kwenda Chalinze kuijenga upya ,kwa mujibu ya muheshimiwa Omari Issa anayehusika na uwezeshaji na utekelezaji ofisi ya rais kama alivyoongea na kituo cha ITV katika kipindi cha dakika 45, alisema sekta iyo binafsi itapewa dhamana ya kukusanya pesa kwa magari yatakoitaji kupita katika barabara iyo ya kisasa itakayojengwa.

loh!
Utafiti mpya wa kisayansi
umefichua kwamba uwezo wa
binadamu kukumbuka na shughuli
nyingine za ubongo huanza kufifia
katika miaka ya arobaini - mapema
zaidi kinyume na ilivyodhaniwa
awali.
Wanasayansi wamefanyia
uchunguzi uwezo wa kiakili wa
watu elfu saba wafanyakazi wa
umma nchini Uingereza walio na
umri wa miaka kati ya arobaini na
tano na sabini katika kipindi cha
miaka kumi.
Walishangazwa kupata kwamba
watu wa umri wa miaka arobaini na
tano na arobaini na tisa
walionyesha kufifia kwa asilimia
tatu kwa uwezo wao wa
kukumbuka, kuelewa na kufikiria.
Awali ilidhaniwa ni katika miaka ya
sitini ambapo binadamu hushindwa
kukumbuka na kuelewa vyema.
 
Inamaana wanamaanisha barabara lililopo liko chini ya kiwango?
Pia nchi itafaidika vip na mradi huo? au ndo tuseme watavuna kwa miaka kumi kufidisha gharama ya ukarabati wa barabara hiyo?
 
Kwanza ilikua Kibamba city the wakahamia Kigamboni city huko kote baado kabisa na awamu inaisha mwakani. Then barnar Dar Chz. hii sio posibo. kwanini tulipe kodi halafu tulipishwe ? this is double taxation.
 
Back
Top Bottom