Bank teller alivyotapeliwa

Bank teller alivyotapeliwa

Unamaana hakuzipitisha kwenye Ile mashine ya kuhesabia?
 
Yani teller apewe pesa tena asithibitishe kama amount ipo sahihi? HAIWEZEKANI. Teller atasahau vyote lakini si kuhesabu pesa..Hiyo ni kanuni namba moja ya bank teller.

Story nzuri anyway
Hujalazimishwa kuamini
 
Hakuna teller fala kiasi hicho (labda kama sijawahi tumia benki nyingi)

Hawa jamaa kwenye suala la kuhesabu fedha wapo serious sana. Labda useme ni teller wa tigo pesa
 
kwani siku hizi bank teller wanakaa ndani ya vioo vyenye tinted

visivyoonyesha hata mteja anachofanya nnje ya kioo?
Mkuu haujawahi kukumbana na mikono ya tapeli namna anavyoweza kukuonesha kitu halisi, utapojipinda kuhesabu hela ya kumlipa, muda huo huo kwake ni fursa ya kupokezana na kubadilishana hicho kifaa na tapeli mwenzake?

Utakapokamilisha kuhesabu, utakuta kakaa position ileile na furushi ama kifungashio kilekile chenye fekelo ndani.

Hauwezi kukanyagwa panya na kushituka muda huo huo, utapokea furushi na kulipia kisha kuondoka.

Ukienda kugundua baadaye ukarudi umekasirika ili ukomeshe kibaka, hauwezi kumkuta na hauwezi kutana naye popote maishani mwako, na ndiyo inakuwa imetoka hiyo.

Kwa kisa hiki, huyo teller kwa kuwa tayari alikuwa kazihesabu na kuzipima na kujiridhisha kwamba ni zenyewe, ule muhu wa kurejelea kuhesabu hata ungelikuwa ni wewe ungelilizwa tu, kubali ama kataa.
 
Mawakala wamepigwa sana katika mfumo huo kuna dada alipewa laki sita akahesabu ziliporudi mara yapili zikawa laki na hamsini aliwekewa elfu mbilimbili kati
Kumbe siku hiyo na wewe ulikuwepo? Mimi ndio nilifika nataka kutoa pesa nikamtajia kiasi nachotoa. Akazitoa azihesabu, alichokikuta ni siri ya wengi.

Halafu kalikuwa kabishi sana tunakaambia piga simu customer care waambie umekosea namba, kakaanza kutuuliza "mnanifundisha kazi?" Utadhani polisi. Basi bwana kakasema MIMI NI WAKALA NIMEMTUMIA MTU PESA LAKINI AMENIPA KIASI PUNGUFU, BADALA YA LAKI SITA AMENIPA LAKO NA NUSU. Voda wakamwambia MUONGOZO UNAMKUTAKA KUHAKIKI KIASI KABLA YA KUMUHUDUMIA MTEJA, ASANTE. Nilicheka kama mazuri vile, hii ilikuwa Mwanza mwaka 2015 hv
 
Benkteller kilaza.
Iko hivi..

Jamaa mmoja alikuwa na Dola za kimarekani elfu kumi (kama milioni 20 za kitanzania). Akafika bank na kwenda dirishani moja kwa moja.

Baada ya kufika dirishani akampa pesa hizo dola ili abadilishe na kuwa pesa za kitanzania. Yule teller akapokea na kuzihesabu pamoja na kuhakiki kama ni halali. Baada ya kuridhika nazo kuwa zipo sawa wakati anataka kuanza kuhesabu za kitanzania yule jamaa akauliza exchange rate ipo vipi?

Akatajiwa akasema ndogo sana naomba dola zangu. Akarudishiwa akajifikiria kama sekunde kadhaa akamrudishia tena yule teller basi nipe hivyo hivyo tu.

Yule teller bila hata kuzikagua tena zile Dola akapokea na kuanza kumuhesabia jamaa pesa zake na kumpatia.

Jamaa akaondoka, kufika muda wa kufunga hesabu anafungua zile dola anakuta ya juu na ya chini ndio pesa halisi. Yaliyobaki yote makaratasi.

Maoni yangu:
Matapeli wawe wanachomwa moto maana wanaharibu maisha ya watu fikiria pesa zaidi ya milioni ishirini unaenda kumtapeli mwenzio ni sawa na kutaka kumuua.

Nawasilisha.
 
Madogo wameajiriwa branch ya Mtwara halafu wakakbidhiwa kuoperate ATM, Branch controller naye kawaamini asubuhi anaacha kubalance akaunti ya ATM. Madogo pesa zinazobaki jana yake wanaweka pembeni wanabalance akaunti alafu wanaweka hela zingine kwa siku husika. Baada ya miezi michache washanunua magari na mishahara miaka ile ilikuwa midogo lazima uchukue mkopo ndo ununue gari. Madogo gheto limesheheni mazaga kibao. Ikabidi tuitwe wazee wa fraud investigation miaka hiyo. Wangekuwa wajanja walikuwa hawana kesi na msala ungebaki kwa controller. Madogo tumewaweka sawa na ahadi kemkem wakaingia line. Msala ukawa wao na kazi ikaisha. Sijui wako wapi siku hizi.
Boss fraud investigation ni kitengo cha polisi au hapo hapo benk kuna kitengo hiko
 
Sasa mimi nakwambwia hiyo ya 2008 ilitokea kabisa nakuhakikishia kwa asilimia mia, tena wale walikuwa na kama USD 20K. Tena waliokuwa wafanyakazi miaka ile walisomewa hadi email toka HQ kuwatahadharisha
Zile pesa zinahesabiwa na machine,karatasi nazo alizihesabu au inakua vp
 
Boss fraud investigation ni kitengo cha polisi au hapo hapo benk kuna kitengo hiko
Sijui benki zingine ila hiyo benki wana kitengo cha fraud kwa ajili ya matukio ambayo mengi yanahusisha wafanyakazi, mwisho wa siku ikibidi unakabidhiwa kwa vyombo vya usalama
 
Wana
Zile pesa zinahesabiwa na machine,karatasi nazo alizihesabu au inakua vp
kuwa na bundle mbili, ile ya kwanza inakuwa ni hela kweli, ili ukiwarudishia watakachokupa ndo hizo katikati makaratasi. Ni kitendo cha haraka na lile begi lililoko miguuni wewe cashier huwezi kuliona, akiinama akiinuka mzigo feki tayari mkononi.
 
Back
Top Bottom