fdizzle
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 1,902
- 2,405
Iko hivi..
Jamaa mmoja alikuwa na Dola za kimarekani elfu kumi (kama milioni 20 za kitanzania). Akafika bank na kwenda dirishani moja kwa moja.
Baada ya kufika dirishani akampa pesa hizo dola ili abadilishe na kuwa pesa za kitanzania. Yule teller akapokea na kuzihesabu pamoja na kuhakiki kama ni halali. Baada ya kuridhika nazo kuwa zipo sawa wakati anataka kuanza kuhesabu za kitanzania yule jamaa akauliza exchange rate ipo vipi?
Akatajiwa akasema ndogo sana naomba dola zangu. Akarudishiwa akajifikiria kama sekunde kadhaa akamrudishia tena yule teller basi nipe hivyo hivyo tu.
Yule teller bila hata kuzikagua tena zile Dola akapokea na kuanza kumuhesabia jamaa pesa zake na kumpatia.
Jamaa akaondoka, kufika muda wa kufunga hesabu anafungua zile dola anakuta ya juu na ya chini ndio pesa halisi. Yaliyobaki yote makaratasi.
Maoni yangu:
Matapeli wawe wanachomwa moto maana wanaharibu maisha ya watu fikiria pesa zaidi ya milioni ishirini unaenda kumtapeli mwenzio ni sawa na kutaka kumuua.
Nawasilisha.
Jamaa mmoja alikuwa na Dola za kimarekani elfu kumi (kama milioni 20 za kitanzania). Akafika bank na kwenda dirishani moja kwa moja.
Baada ya kufika dirishani akampa pesa hizo dola ili abadilishe na kuwa pesa za kitanzania. Yule teller akapokea na kuzihesabu pamoja na kuhakiki kama ni halali. Baada ya kuridhika nazo kuwa zipo sawa wakati anataka kuanza kuhesabu za kitanzania yule jamaa akauliza exchange rate ipo vipi?
Akatajiwa akasema ndogo sana naomba dola zangu. Akarudishiwa akajifikiria kama sekunde kadhaa akamrudishia tena yule teller basi nipe hivyo hivyo tu.
Yule teller bila hata kuzikagua tena zile Dola akapokea na kuanza kumuhesabia jamaa pesa zake na kumpatia.
Jamaa akaondoka, kufika muda wa kufunga hesabu anafungua zile dola anakuta ya juu na ya chini ndio pesa halisi. Yaliyobaki yote makaratasi.
Maoni yangu:
Matapeli wawe wanachomwa moto maana wanaharibu maisha ya watu fikiria pesa zaidi ya milioni ishirini unaenda kumtapeli mwenzio ni sawa na kutaka kumuua.
Nawasilisha.