Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,104
- 5,665
Akiwa amejawa na furaha na bashasha baada ya kuzukiwa na muujiza wa kusamahewa madhambi yake bila kuomba msamaha mdharauliwa, waziri mkuu mizengo pinda, jana jioni alilidanganya bunge kwa kuliahidi kwamba kila kilichoazimiwa na bunge kitatekelezwa kama kilivyoazimiwa kwa ukamilifu.
Pinda,akiwa na nguvu mpya zilizomuwezesha kucheka kwa mara ya kwanza toka siku ile PAC wasome report yao bungeni,akadai atatumia mfumo wa BANGO KITITA katika kuhakikisha utekelezaji wa maadhimio hayo.
Moja ya azimio ni utaifisishaji wa MALI ZA IPTL.
Najiuliza,Pinda atatekelezaje hili kwa ukamilifu?
Pinda,akiwa na nguvu mpya zilizomuwezesha kucheka kwa mara ya kwanza toka siku ile PAC wasome report yao bungeni,akadai atatumia mfumo wa BANGO KITITA katika kuhakikisha utekelezaji wa maadhimio hayo.
Moja ya azimio ni utaifisishaji wa MALI ZA IPTL.
Najiuliza,Pinda atatekelezaje hili kwa ukamilifu?