Bandarini Dar: Utoaji wa gari!

Angalia msidanganyike kirahisi hivyo, bandari ya Dar kwa upande wa magari kwa kweli kwa sasa wamejitahidi sana, wameboresha huduma, hata ule wizi siku hizi hakuna tena. Hiyo ya Mombasa ni njia ilikuwa inatumiwa wakati ule TRA wanafanya uzembe kule mipakani ambapo watu walitumia ujanja kuingiza magari bila kulipia zile tax muhimu zote. Lakini kwa sasa ukitumia Mombasa nakuhakikishia it will cost you more than if you use Dar port. Ninafanya sana hizo biashara najua what is happening this time. Last week kuna gari ya mdogo wangu mmoja mbishi sana naye tumemshauri atumie dar port amebisha. Kilichomtokea anajuta hadi leo. Amelipa 2times more than mwenzake aliyepitisha dar port.

Kuhusu gari kuchukua muda mrefu pale dar port sometimes tunawalaumu TRA kumbe uzembe ni wetu, watu wana forge documents ili CIF ionekane ndogo walipe kidogo. Sasa zile documents zikishakuwa proccessed ziko kwenye final kuna CIA wa TRA ambao wanapitia at last!! wakishagudnua hilo wanazirudisha inabidi uanze upya zoezi zima na utalipa Uplifted CIF.

Mkuu nakushauri tumia document zako kama zilivyo bila forgery yeyote utapata gari lako within two weeks.

Mkuu hilo ni kweli, siku hizi wameimprove kwa magari, ila pia hakikisha una mpata agenti shapu!
 
"Mara watake kile mara hichi..." "hichi" ndio kitu gani hicho "hichi"? Labda tuwe specific zaidi.

Hii kuwapelekea biashara Kenya nako ni sawa na ufisadi tu. Fisadi haitakii nchi mema, kama wewe na wenzio hapo juu, "bora Mombasa." Tujenge nchi yetu wajameni. Tu-protest hiyo rushwa hapo bandari. Kwa kuanzia hebu jua na taja walikuomba nini specifically? Hakuna anaesema waliniomba karatasi hii na procedure ile na hii badala ya hiki na kile. Walikudai "hichi," what do you mean "hichi," taxes? Darn skippy customs will tax you.

Kumbe wateja wenyewe hawaleti genuine paperwork za mizigo. Unasema nataka kuingiza gari "kuja Bongo," kwa hiyo uko Dar, sasa kwa nini usiende Kurasini kusikia from the horses mouth? Know how to get there? Msimbazi Road all the way down, past Gerezani, past Nyerere Road, straight shot, can't miss it, if you hit blue waters you gone too far, alright, gosh! Hapa hakuna specifics, hakuna uzalendo, unaambiwa nenda Mombasa. Forget Mombasa, I'm not talking bout Mombasa. Tujenge vya kwetu, Holly Mecca!


Mkuu nashukuru sana kwa majibu yako na nimekuelewa tena vizuri sana...Sasa labda nikuambie kwamba kama ningekuwa bongo nisingeweza kuuliza hili swali vile vile ni kwamba sijawahi kushusha gari kutoka japan ndio mara yangu ya kwanza ila nina marafiki zangu wengi sana wanashusha gari hapo dar na kwa ujumla najuwa sana tena sana ni wasumbufu sana hapo bandarini hasa rushwa...Hicho kitu nafahamu na hata nikiileta lazima niandae hizo hela kwa ajili hiyo...ila nashukuru kwa msaada mkuu...Sasa wewe utakubali kutoa hela sehemu ambapo unaona unaliwa kimacho macho????
 
Mkuu naona hapa unapotosha kidogo......TRA hawana bei yao, in principle inatakiwa waanzie kny CIF value kucalculate taxes zote kuarrive at total taxes payable, sasa kama wewe documents zako hazieleweki, ni forged etc ndio wanafanya uplifting ya CIF na sio vinginevyo.....! refer post ya Mpendanchi!



Mkuu nimekupata so wakigundua kwamba document wamezi forge ndio wanaongeza hela au sio??Sasa watu wanafikiria nini mpaka waforge document?????Na pia wenyewe wanaruhusu kufanya uplifting ya CIF????
 
Kaaaaaaa!
Yani inazidi bei atakayonunulia kule.

Mimi nashauru uandae 25% of the purchasing price


Mkuu hapa sijakuelewa vizuri kabisaaaa.....Au labda nieleweshe vizuri kwa mara nyingine...Au na wewe hujaelewa pia??Niongeze 25% ya kununulia gari au ya kununulia hiyo gari pamoja na usafirishaji???
 
Lazima pia uwe na shilingi elfu tano tano kwa ajili ya kuwapa wapambe wakuonyeshe gari lilipo, wakukuonyesha ufunguo, wakukulindia, wakukuharakishia ili wasikufanyie mizengwe hadi 11.59 jioni, nn.k


Nashukuru sana mkuu kwa majibu yako mzeee mzima...Sasa kumbe kuna process ndefu sana kwa kweli..Mpaka kuwapa wapambe hizo hela...Kama ukifatilia mwenyewe kila kitu itashindikana??
 
nilisahau lazima pia umwombe mungu ashikilie hasira kwani waweza kumpiga / dunda DALALI wako pia


Duuu mkuu asante kwa yote na maelezo yako...Sasa huyo dalali na yeye ndio anahitaji nini zaidi...Au yeye anafatilia kila kitu mpaka kutoka???
 
wazo lingine bora baada ya kupiga mahesabu hakikisha hiyo pesa ipo.....ndugu usiombe
likafika huna pesa za kutolea ndugu gari hilo linakuwa la TRA..........hizi mistake wengi wanazifanya....all the best


Nashukuru sana MAMA kwa mawazo yako...Asante sana nitajitahidi kadri ya uwezo wangu nijitahidi maana inabidi kujitahidi kwa kila kitu!!
 
kutokana na uzoefu wangu (note: sikuwahi kuwa na Forged Document wala nini mara nyingi tu nimeagiza gari na haya masuala yamenikuta)...........suala la ku-uplift haliko wazi kabisa na vigezo vyake haviko wazi.........na ndio mlango mwingine wa Rushwa pale TRA.......Ikiwezekana lile lijitabu lao likubwa basi na liwe accessible na wananchi (na waliweke hivyo vigezo vyao mtandaoni kabisaa)......na sio kuwashangaza wananchi pale wanapoleta Uplift zao za KIUONEVU.....BTW kwanini nyintyi TRA hamjifunzi kutoka kwa vyombo vingine kama hivyo hapo jirani zetu....?

Mimi nazungumzia uzoefu wangu pale.......kamwe sijawahi ku-forge document........sasa kama wewe unataka mshikaji akaawaachie gari TRA wee enedelea.............

Ndg Papizo.......Jamaa wengine hapa wapo kutetea TRA pamoja na utendaji wao m-bovu...............kama walivyokuambia wengine hapo juu.........jiandae kukutana na mambo yatakayokutia HASIRA.........uwe mvumilivu......na please ni vema ukawa na pesa yako ya kutosha kama nilivyokushauri...............

Bytheway....Papizo ukisha litoa Gari lako tungependa kupata feedback mambo yaliendaje............



Duuu mkuu nimeona mambo ya TRA yanaingia na hapa.....ila hamna shaka nadhani kila process itakuwawepo lazima niweke hapa jamvini.....ila siku zote kizuri hakipatikani kwa urahisi so nitajaribu kukaribiana nao hao jamaa......Maana lazima twende nao sambamba.......Nashukuru mkuu!!
 
Nimetoa gari mara mbili, sijawahi kupata uplift au kucheleweshewa kutoa gari kiasi cha kulipia storage charge.

Kama gari ya million 4 unaandaa milioni 4 na zaidi, plus usumbufu na kusubiri muda mrefu; kwa nini usiende show room ukachague gari, ulipie vinavyopaswa the uko barabarani na mchuma wako.


Asante sana MAMA lakini sasa tuangalie gari zetu za bongo na hizo ambazo tunazitoa huku zipo sawa???Then gari ya aina gani labda unaweza kupata kwa M8??
 
Uplift ya bei kwa TRA wanafanya sana kama umeagiza kutoka kwenye kampuni isiyoeleweka au umenunua kwa mtu binafsi. Ila kama umenunua kwa kampuni inayoeleweka huwa haina shida. Kuhusu show rooms za hapa Bongo ni hatari sana hasa kama huwafahamu wauzaji maana wanaleta magari mabovu sana kutoka Dubai na bei ni kubwa mno. Kama unataka gari agiza mwenyewe kutoka mnadani moja kwa moja Japan, bei ni rahisi mno na utaangalia details za gari unayoitaka kabla hujanunua. Epuka kununua gari yenye zaidi ya miaka 10 ili kuepuka faini ya 10%. Kama unataka gari ingia hapa http://www.tradecarview.com/stock/pr/7656/220/?si=220. Kuhusu clearing agents nafikiri kwa gari ndogo kama Mark II haizidi laki 2 siyo laki 5.



Nashukuru sana mkuu...Nimeona hiyo link hapo na nimecheck nimeona magari yao..Then nimeona MAMA anasema kwamba show room kuna gali ya M8 sasa bongo gari la M8 utapata gari la aina gani na lipo vipi???ila nashukurukwa hiyo link hapo na nitaicheck pia vizuri??
 
Kwa bahati mbaya sana, clearing agents wanaotakiwa kuwasaidia wateja wao kutoa mizigo yao bandalini yakiwamo magari, ndio hao hao wanaoshirikiana na watu wa TRA kuwaumiza wateja wao!! Mimi niliagiza gari kupitia Dar port sasa clearing agent wangu akazembea kuprocess documents; kumbe meli iliisha fika zamani na gari kushushwa nakuchelewa kwake kukanifanya nilipe demurrage charges almost $2000!! Licha ya kuniomba fedha za kuwahonga watu wa bandalini na gharama zake agent mwenyewe!!!. Ni muhimu kumtafuta clearing agent anaeheshimu kazi yake na muadilifu kwani si wote wachafu.



Mkuu sasa agent wa uwaminifu utampata wapi???Na utaweza kumjuaje kama huyu ni muamifu??????
 
Bongo kweli tumelala. Hii thread ipo siku ya pili sasa, Bandari ina Afisa masoko, Afisa uhusiano, mkurugenzi mkuu na maofisa kibao. Hamna hata mmoja anayekuja kuitetea bandari yao hapa !! Watu wanabishana kwenda Mombasa, lakini wao kimyaaa... Wanashindwa hata na Malkia Elizabeth mwenye Facebook!! Matangazo siyo lazima yatoke kwenye gazeti la Mzalendo.Kuja kutetea hoja hapa inaweza kulipa zaidi....


Nashukuru mkuu......ila labda wanajuwa kweli hivyo vitu vipo ndio maana watu wengi hawataki kushusha mzigo kwenye bandari yao!!
 
Angalia msidanganyike kirahisi hivyo, bandari ya Dar kwa upande wa magari kwa kweli kwa sasa wamejitahidi sana, wameboresha huduma, hata ule wizi siku hizi hakuna tena. Hiyo ya Mombasa ni njia ilikuwa inatumiwa wakati ule TRA wanafanya uzembe kule mipakani ambapo watu walitumia ujanja kuingiza magari bila kulipia zile tax muhimu zote. Lakini kwa sasa ukitumia Mombasa nakuhakikishia it will cost you more than if you use Dar port. Ninafanya sana hizo biashara najua what is happening this time. Last week kuna gari ya mdogo wangu mmoja mbishi sana naye tumemshauri atumie dar port amebisha. Kilichomtokea anajuta hadi leo. Amelipa 2times more than mwenzake aliyepitisha dar port.

Kuhusu gari kuchukua muda mrefu pale dar port sometimes tunawalaumu TRA kumbe uzembe ni wetu, watu wana forge documents ili CIF ionekane ndogo walipe kidogo. Sasa zile documents zikishakuwa proccessed ziko kwenye final kuna CIA wa TRA ambao wanapitia at last!! wakishagudnua hilo wanazirudisha inabidi uanze upya zoezi zima na utalipa Uplifted CIF.

Mkuu nakushauri tumia document zako kama zilivyo bila forgery yeyote utapata gari lako within two weeks.


Mpendanchi,

Umetoa very useful information kwa wale ambao hawakuwa wanafahamu zaidi.
Mimi binafsi nimekuwa nikitumia bandari ya Dar es Salaam wakati wote nilipoingiza magari yangu. Mara ya mwisho niliweza kutoa gari ambayo iliteremshwa saa 10 usiku na kuitoa ndani ya eneo la bandari siku ya tatu saa 5 asubuhi.
Je ni kwanini nilifanikiwa kutoa gari haraka
  • Nilihakikisha kuwa nimepata bill of lading mapema sana kabla ya meli kufika.
  • Nilianza process zote ambazo hazikuhitaji kuwepo kwa gari.
  • Nilifuatilia ratiba ya kuwasili kwa meli ikiwa ni pamoja na kujua kama kuna mabadiliko.
  • Niliweka utaratibu wa kitu gani agent awe amekifanya kwa maelekezo yangu na si kwa matakwa yake (mimi ndiyo muajiri wake kwa wakati ule)
  • Nilihakikisha agent hanipi kishawishi chochote cha kubadilisha maelezo ya kwenye nyaraka kwa kigezo cha kupunguza ushuru na kodi zingine.
Moja ya matatizo yanayowakuta waagizaji ni pamoja na kushawishiwa na baadhi ya maajenti au wao wenyewe kufikiria kuwa kurekebisha nyaraka kutaweza kusaidia kupunguza ushuru na kodi zingine. Kimsingi hili ni kosa kubwa kwani kwa kufanya hivyo tayari unakuwa umefungua mlango wa kutoa rushwa. Kitakachofuatia ni kuambiwa toa kiasi fulani tumpatie mtumishi wa TRA nk. Hata kama huyo mtumishi hahusiki au ana husika bado hili kosa hatupaswi kujenga dhana ya kudanganya ambayo huleta usumbufu kwenye kupitia documents zako.

Kama umeamua kuagiza gari kaa chini jua ni gari la thamani gani unataka kuagiza, fanya estimates za gharama zote husika, then tenga pesa kwa ajili ya shughuli hiyo. Hakikisha document zote zinajieleza zenyewe bila ya kuzifanyia alterations. Fanya matayarisho ya mapema juu ya clearance ya gari kabla haijafika, jisikie huru kulipa gharama ambazo tayari umekwishazijua. Trust me utapata gari lako katika muda mfupi sana.
Hakikisha unakwepa short-cuts kwani ndizo mara nyingi huongeza muda wa kuprocess documents.
Si kushauri uteremshie gari lako Mombasa, gharama zitazidi kwani ule ujanja-ujanja wa mipakani sasa hivi haupo.

Mwisho TRA wanaweza ku-uplift thamani ya gari endapo utashindwa kuthibitisha gharama halisi kama iko chini ya viwango vilivyopangwa na TRA. Hii inatumika ili kuwabana wale ambao wana-undervalue mizigo yao kwa ajili ya kukwepa kulipa ushuru halali. Endapo utawapa TRA value yenye utata basi muagizaji unahitajika kuthibitisha ikiwemo kutoa vielelezo vyote tangu unaagiza na hadi ulipotuma fedha za malipo. TRA wana haki ya kutafuta ukweli wa bei hiyo kutoka kwa muuza na wakikuta ni tofauti then wanakuwajibisha kwa mujibu wa sheria na taratibu zao.
Sasa hapa ndipo huwa kuna matatizo na watu hulalamika kumbe vyanzo vya matatizo ni kutaka kukwepa ushuru.
Ni wazi kuwa gari lako litaendelea kukaa bandarini na kuchajiwa kwa kuwepo pale, vinginevyo unaweza kuliondoa bandari kwa makubaliano na TRA lakini utalipeleka katika Bonded Warehouse ambayo pia utabidi ulipe kwa makubaliano na mwenye warehouse hiyo.
In short tufanye homework zetu kabla hatujafanya maamuzi ya mwisho
 
Mpendanchi,

Umetoa very useful information kwa wale ambao hawakuwa wanafahamu zaidi.
Mimi binafsi nimekuwa nikitumia bandari ya Dar es Salaam wakati wote nilipoingiza magari yangu. Mara ya mwisho niliweza kutoa gari ambayo iliteremshwa saa 10 usiku na kuitoa ndani ya eneo la bandari siku ya tatu saa 5 asubuhi.
Je ni kwanini nilifanikiwa kutoa gari haraka
  • Nilihakikisha kuwa nimepata bill of lading mapema sana kabla ya meli kufika.
  • Nilianza process zote ambazo hazikuhitaji kuwepo kwa gari.
  • Nilifuatilia ratiba ya kuwasili kwa meli ikiwa ni pamoja na kujua kama kuna mabadiliko.
  • Niliweka utaratibu wa kitu gani agent awe amekifanya kwa maelekezo yangu na si kwa matakwa yake (mimi ndiyo muajiri wake kwa wakati ule)
  • Nilihakikisha agent hanipi kishawishi chochote cha kubadilisha maelezo ya kwenye nyaraka kwa kigezo cha kupunguza ushuru na kodi zingine.
Moja ya matatizo yanayowakuta waagizaji ni pamoja na kushawishiwa na baadhi ya maajenti au wao wenyewe kufikiria kuwa kurekebisha nyaraka kutaweza kusaidia kupunguza ushuru na kodi zingine. Kimsingi hili ni kosa kubwa kwani kwa kufanya hivyo tayari unakuwa umefungua mlango wa kutoa rushwa. Kitakachofuatia ni kuambiwa toa kiasi fulani tumpatie mtumishi wa TRA nk. Hata kama huyo mtumishi hahusiki au ana husika bado hili kosa hatupaswi kujenga dhana ya kudanganya ambayo huleta usumbufu kwenye kupitia documents zako.

Kama umeamua kuagiza gari kaa chini jua ni gari la thamani gani unataka kuagiza, fanya estimates za gharama zote husika, then tenga pesa kwa ajili ya shughuli hiyo. Hakikisha document zote zinajieleza zenyewe bila ya kuzifanyia alterations. Fanya matayarisho ya mapema juu ya clearance ya gari kabla haijafika, jisikie huru kulipa gharama ambazo tayari umekwishazijua. Trust me utapata gari lako katika muda mfupi sana.
Hakikisha unakwepa short-cuts kwani ndizo mara nyingi huongeza muda wa kuprocess documents.
Si kushauri uteremshie gari lako Mombasa, gharama zitazidi kwani ule ujanja-ujanja wa mipakani sasa hivi haupo.

Mwisho TRA wanaweza ku-uplift thamani ya gari endapo utashindwa kuthibitisha gharama halisi kama iko chini ya viwango vilivyopangwa na TRA. Hii inatumika ili kuwabana wale ambao wana-undervalue mizigo yao kwa ajili ya kukwepa kulipa ushuru halali. Endapo utawapa TRA value yenye utata basi muagizaji unahitajika kuthibitisha ikiwemo kutoa vielelezo vyote tangu unaagiza na hadi ulipotuma fedha za malipo. TRA wana haki ya kutafuta ukweli wa bei hiyo kutoka kwa muuza na wakikuta ni tofauti then wanakuwajibisha kwa mujibu wa sheria na taratibu zao.
Sasa hapa ndipo huwa kuna matatizo na watu hulalamika kumbe vyanzo vya matatizo ni kutaka kukwepa ushuru.
Ni wazi kuwa gari lako litaendelea kukaa bandarini na kuchajiwa kwa kuwepo pale, vinginevyo unaweza kuliondoa bandari kwa makubaliano na TRA lakini utalipeleka katika Bonded Warehouse ambayo pia utabidi ulipe kwa makubaliano na mwenye warehouse hiyo.
In short tufanye homework zetu kabla hatujafanya maamuzi ya mwisho



Mkuu nashukuru sana tena sana na nimekuelewa tena vile vile......

Sasa maswali yangu ni kwamba je tatizo ambalo la muhimu sana hao TRA wanahitaji kujua ukweli wa idadi uliyonunulia gari lako pamoja na kusafirisha???Nadhani ushuru ni sawa kwa kila mtu kulipa na inategemea huo ushuru utakuwa kiasi gani kutokana na gari lenyewe jinsi lilivyo na thamani iliyonunuliwa.........Lakini nimekuelewa vizuri na nashukuru sana kwa kukaa chini kwa kuniandikia maelezo malezo na yenye upeo zaidi!!
 
Mkuu nashukuru sana tena sana na nimekuelewa tena vile vile......

Sasa maswali yangu ni kwamba je tatizo ambalo la muhimu sana hao TRA wanahitaji kujua ukweli wa idadi uliyonunulia gari lako pamoja na kusafirisha???Nadhani ushuru ni sawa kwa kila mtu kulipa na inategemea huo ushuru utakuwa kiasi gani kutokana na gari lenyewe jinsi lilivyo na thamani iliyonunuliwa.........Lakini nimekuelewa vizuri na nashukuru sana kwa kukaa chini kwa kuniandikia maelezo malezo na yenye upeo zaidi!!

Kama nimekuelewa vizuri swali lako unamaanisha thamani badala ya neno 'idadi'. Kitu cha muhimu hapa usijaribu kufanya alterations katika nyaraka zako. Wacha nyaraka zako zioneshe bei halisi ambayo mara nyingi ni CIF au C & F. TRA wanaweza kutilia mashaka bei kwa kuangalia aina ya gari, mwaka na ujazo wa injini. TRA wanaelewa kabisa average ya bei au gharama inaweza kuwa ni kiasi gani kutokana mahali uliponunulia. Kwa mfano mimi nikinunua gari Dubai Toyota Mark II mwaka ya 2006 yenye 2000cc na wewe ukinunua the same type of car Japan kwa bei ileile niliyonunulia Dubai, bei zetu za kukadiria ushuru na kodi zitatofautiana kwavile freight ya Dubai ni ndogo ukilinganisha na Japan.
 
Last edited:
Mfano uliotoa hauko sahihi,
Kodi ya mzigo uliotoa Mombasa hauilipii Bandarini, unailipia mpakani Horohoro na bei yake haitofautiani na ile ya DSM unless unadhamiria kucheza ''karate''. Ukijumlisha na gharama za kuusafirisha mzigo mpaka Dizim unarudi palepale. Bandari ya Mombasa wanaitumia watu wanaitaka kucheza carate mpakani, ili kuepuka kodi. Huo ndio uhalisia wenyewe, na tunaujua ipasavyo.
Swala la sababu kubwa ya ucheleweshaji waliotangulia wamelifafanu ipasavyo, nadhani umepitia michango yao.
Tusipokuwa wazalendo tutashindwa kuwafundisha watoto wetu uzalendo halafu wataishia kuwa watumwa.

Duh, naona umeshindwa tena kunielewa. Umeacha kujielewesha concept niliyoitoa na badala yake umejikita kwenye mfano nilioutoa kana kwamba ni kadhia halisi.

Nilichokuwa nakisema ni kwamba ktk large picture, individual mwenye uwezo wa mdogo kifedha hawezi kujitumbukiza kwenye vitu vyenye gharama zaidi kwa kisingizio cha utaifa. Hata watu wenye mitaji mikubwa ndio kabisa....

Ninachozungumzia ni kuwa uchumi huria unatoa options na uwigo mpana zaidi wa mtu kutumia njia inayomfaa ambayo anaona itafanya mambo yake yanyooke vizuri bila mikwaruzo, kwa ku-overcome mipaka ya kijiografia,nk.
 
.............Mwisho TRA wanaweza ku-uplift thamani ya gari endapo utashindwa kuthibitisha gharama halisi kama iko chini ya viwango vilivyopangwa na TRA. ........

Kifupi hapo kwenye uplift ni TATIZO KUBWA........mi nasema si mara moja wala mbili wala tatu nimeagiza gari.....na genuine docs yet still wana-uplift....SHENZI SANA TRA.......inabidi wawaambie basi wananchi kupitia mtandao au njia nyingine ni kampuni zipi ni genuine.........na wa-define kabisa what are the genuine docs kwa mtizamo wao.....otherwise ni uonevu sana unaendelea pale TRA...........

Nyie acheni kuzuga watu hapa kuwa eti mambo ni mazuri na eti straight forward pale TRA!!.......wee subiri upate feedback ya Papizo......utashangaa

hebu chukulia mtu kasevu vijidola vyake na sasa anaingia mtandaoni (tena hii ni risk kwa kuwa hao watu mtandaoni huwafahamu)..............mitandao iko mingi ya kuagiza magari na bei zao ni tofauti.......obviously one atakwenda kuagiza kule kwenye bei rahisi.......sasa anapokutana na UJINGA (uplift) wa TRA eti bei si genuine.....ndio USHENZI wa TRA ulipo......eti nianze kuthibitisha......thibitisha my foot....damn!!

Mfano mzuri wee ingia mtandaoni sasa hivi angalia bei ya Mercedes Benz 1998 or so....... saloon.......CIF mpaka dar unaweza kupata kuanzia $5000 na kuendelea.......sasa wewe nenda kakutane na TRA halafu niambie final cost mapka unatembea nayo mtaani..........

acheni kuzuga watu jamani...tuongelee hali halisi na sio kama wanasiasa

KWENYE UPLIFT TRA HAWAKO WAZI
 
Kifupi hapo kwenye uplift ni TATIZO KUBWA........mi nasema si mara moja wala mbili wala tatu nimeagiza gari.....na genuine docs yet still wana-uplift....SHENZI SANA TRA.......inabidi wawaambie basi wananchi kupitia mtandao au njia nyingine ni kampuni zipi ni genuine.........na wa-define kabisa what are the genuine docs kwa mtizamo wao.....otherwise ni uonevu sana unaendelea pale TRA...........

Nyie acheni kuzuga watu hapa kuwa eti mambo ni mazuri na eti straight forward pale TRA!!.......wee subiri upate feedback ya Papizo......utashangaa

hebu chukulia mtu kasevu vijidola vyake na sasa anaingia mtandaoni (tena hii ni risk kwa kuwa hao watu mtandaoni huwafahamu)..............mitandao iko mingi ya kuagiza magari na bei zao ni tofauti.......obviously one atakwenda kuagiza kule kwenye bei rahisi.......sasa anapokutana na UJINGA (uplift) wa TRA eti bei si genuine.....ndio USHENZI wa TRA ulipo......eti nianze kuthibitisha......thibitisha my foot....damn!!

Mfano mzuri wee ingia mtandaoni sasa hivi angalia bei ya Mercedes Benz 1998 or so....... saloon.......CIF mpaka dar unaweza kupata kuanzia $5000 na kuendelea.......sasa wewe nenda kakutane na TRA halafu niambie final cost mapka unatembea nayo mtaani..........

acheni kuzuga watu jamani...tuongelee hali halisi na sio kama wanasiasa

KWENYE UPLIFT TRA HAWAKO WAZI

Sasa ndg Ogah umekutana na tatizo la uplift kwa mara ya kwanza hukuchukua hatua za kujua kiini ni nini cha uplifts zilizokukuta? Umekutana na tatizo kwa mara ya pili mambo ni yaleyele na mara ya tatu hali kadhalika. Kwanini hujajipi nafasi ya kujiuliza inakuwaje? kwani kwa mara ya tatu? Je, ulikuwa unabahatisha kwa muda wote huo? Je hujajua kosa au tatizo lako liko wapi? Mbona mimi sijapata tatizo la uplift? Haya ni maswali ambayo unatakiwa ujiulize kwani kuna mahali umekuwa unakosea bila hata ya kurudi nyuma na kupata jibu la kudumu. kulalamika pembeni haisadii, ninakupa ushauri nenda kamuone Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi TRA HQ nina hakika unaweza kupata ufumbuzi wa tatizo lako. I remember alikuwa Bw. Mmanda sijui kama sasa hivi kuna mtu mwingine.
 
Angalia msidanganyike kirahisi hivyo, bandari ya Dar kwa upande wa magari kwa kweli kwa sasa wamejitahidi sana, wameboresha huduma, hata ule wizi siku hizi hakuna tena. Hiyo ya Mombasa ni njia ilikuwa inatumiwa wakati ule TRA wanafanya uzembe kule mipakani ambapo watu walitumia ujanja kuingiza magari bila kulipia zile tax muhimu zote. Lakini kwa sasa ukitumia Mombasa nakuhakikishia it will cost you more than if you use Dar port. Ninafanya sana hizo biashara najua what is happening this time. Last week kuna gari ya mdogo wangu mmoja mbishi sana naye tumemshauri atumie dar port amebisha. Kilichomtokea anajuta hadi leo. Amelipa 2times more than mwenzake aliyepitisha dar port.

Kuhusu gari kuchukua muda mrefu pale dar port sometimes tunawalaumu TRA kumbe uzembe ni wetu, watu wana forge documents ili CIF ionekane ndogo walipe kidogo. Sasa zile documents zikishakuwa proccessed ziko kwenye final kuna CIA wa TRA ambao wanapitia at last!! wakishagudnua hilo wanazirudisha inabidi uanze upya zoezi zima na utalipa Uplifted CIF.

Mkuu nakushauri tumia document zako kama zilivyo bila forgery yeyote utapata gari lako within two weeks.

Mkuu, u are really Mpendanchi!!I guess if we'd at least 5 ministers of ur type the country could be about 25 years ahead!!
 
Sasa ndg Ogah umekutana na tatizo la uplift kwa mara ya kwanza hukuchukua hatua za kujua kiini ni nini cha uplifts zilizokukuta? Umekutana na tatizo kwa mara ya pili mambo ni yaleyele na mara ya tatu hali kadhalika. Kwanini hujajipi nafasi ya kujiuliza inakuwaje? kwani kwa mara ya tatu? Je, ulikuwa unabahatisha kwa muda wote huo? Je hujajua kosa au tatizo lako liko wapi? Mbona mimi sijapata tatizo la uplift? Haya ni maswali ambayo unatakiwa ujiulize kwani kuna mahali umekuwa unakosea bila hata ya kurudi nyuma na kupata jibu la kudumu. kulalamika pembeni haisadii, ninakupa ushauri nenda kamuone Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi TRA HQ nina hakika unaweza kupata ufumbuzi wa tatizo lako. I remember alikuwa Bw. Mmanda sijui kama sasa hivi kuna mtu mwingine.

mkuu pundamilia inaonekana una bahati sana au unafahamika, suala la bandarini lina mauzauza mengi kwenye utoaji wa mizigo, tena iwe wewe ni mchukia rushwa (haupo tayari kutoa rushwa) ndio utalijua jiji, kwakweli kwa bongo gharama ya kutoa gari ni kubwa zaidi ya ile uliyonunulia na kusafirisha,

nina jamaa yangu alitaka kuiacha gari yake bandarini, kwa gharama alizoambiwa, mpaka alipolazimika kutoa chochote ndio wakamshushia gharama, sijui kama wamejirekebisha jana au juzi nikiwa namaana hii 2009!!
 
Back
Top Bottom