Mshauri wa rais ni mtu mwenye akili nyingi sana kuliko rais mwenyewe na ni mtu ambaye hamtakii mema rais.
Ukisoma majibu ya mamlaka ya bandari kwa undani ni kwamba mamlaka inambishia rais kwamba hakukuwa na kitu kama hicho na kwamba ulinzi uliopo na taratibu zilizopo kamwe meli 65 zisingeshusha mzigo na kutoweka.
Mimi naamini anayempa rais habari hana nia njema naye na kwa ajabu rais hafanyi verification za habari anazopata. Tumeona sehemu nyingi akidanganywa hadi kufanya maamuzi ambayo baade anayabadiri. Mfano, kusitisha ujenzi wa bandarini ya bagamoyo, wafanyakazi hewa BoT, wakurugenzi wanaolipwa 36M, kupiga marufuku uingizaji sukari, nk. Ifike wakati rais awe na uhakika na anachoambiwa na ajiridhishe, raia wa Tz anamshangaa rais anaposema kuna meli 65 zimeshusha bila kulipa kodi kipindi hiki ambacho wakusanya kodi wako macho zaidi. Mwananchi wakawaida anajiuliza kwanini usalama wa taifa unaompa rais taarifa hizo haukuwapo wakati meli zikifunga Nanga? Huyo aliyempa taarifa hizi bado amebaki kazini?