Balozi Maajar and REX Attorneys

Tangu mwanzo niliona uwezekano mkubwa kwamba Tanesco/Serikali haikuwa na uwakilishi makini kwenye kesi iliyofunguliwa ICC, kadri muda unavyopita ndivyo wasiwasi wangu unazidi kudhihilishwa kuwa ulikuwa na chembe ya ukweli.
Hauhitaji sayansi ya nyukilia kuona tatizo kwenye uteuzi wa Rex Attorneys (kama kweli walikuwa mawakili wa RDC na waliiwakilisha Tanesco kwenye kesi na Dowans). Dowans waliletwa nchini na RDC na kwa kuwa hapakuwepo na tender ya wazi kumpata mrithi wa RDC kwa vyovyote vile RDC na Dowans wanauhusiano ambao unatia madoa makubwa juu ya umakini wa viongozi wa Tanesco/Serikali kuwateua Rex Attorneys wawe wawakilishi wao kwenye mgogoro unaotokana na mteja wao wa mwanzo. Tanzania tuna mawakili wengi wenye weledi na hapakuwa na sababu yoyote ya kuwateua Rex
 
Huu ni mchongo wa hao wakubwa hamna lolote,kila mmoja anajifanya eti hawana la kufanya na hawawezi kukata rufaa kwa sababu wanajua nani ni walipwaji wa hayo mapesa...bora hata na sisi tunaoshinda kwenye komputya hata kuchangia mawazo kuliko hao wabunge wanaosinzia bungeni na kuuliza maswali yaleyale kila mwaka..
 
Wait a minute ina maana REX Attorney walikuwa legal firm ya Richmond na ikisha wakaja wakawa wawakilishi wa Tanesco against Dowans bloody *** Hivi watanzania tumepatwa na nini? Tamaa au dhiki zetu wale wanasheria wa Tanesco hawakufanya their homework wakati wanatafuta wa kuwawakilisha? Au ndio ilikuwa inaandaliwa Tanesco ipatwe kushindwa maana fumbo mfumbie mjinga mwerevu hung'amua.
 
Mambo haya ni kichefuchefu, hata hivyo lazima hatua zichukuliwe kama siyo na Serikali basi na wananchi

Hapa inaashiria kuna kamchezo kanafinyangwa na SERIKALI ili kuiibia JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na WATU WAKE. Napata picha kwamba MEREMETA, KAGODA, TANGOLD, RICHMOND na DOWANS ni Watoto wa Baba Mmoja. Japo Baba yao hataki na kamwe hawezi kuja hadharani hata kama tutamfanyia DNA Test

Serikali iliyo macho wakati wowote kwa ajili ya Usalama, uwepo, uendelevu na maslahi mbalimbali ya Taifa iliwezaje kushindwa kuyabaini haya mpaka itufikishe kuilipa DOWANS Mabilioni hayo?

1. Richmond Kampuni Hewa iliwezaje kufanya uhamisho wa Mkataba kwenda kwa DOWANS Serikali yetu wala isiamke na kusema wewe HEWA umepata wapi utashi wa kuweza kuhamisha Mkataba?
2. Ama wewe HEWA ulikuwa wapi kuibuka ulipokuwa unatafutwa na Kamati Teule ya Bunge?
3. Kama itabainika kuwa kweli REX Attorneys waliwahi kusimamia Maslahi ya Richmond ambae kwa njia ya kuhamishiana Mkataba na DOWANS wamekuwa ndugu katika business, kweli MAJASUSI wetu ndani ya Serikali walishindwa hata kugonga kengele kuiamsha TANESCO usingizini juu ya possible conflicts of intersests with regard to the bias rule juu ya REX Attorneys kwenda kusimamia kesi hiyo?

LAKINI PIA WATANGAZAJI na WAANDISHI WA HABARI ZA KIUCHUNGUZI: Naamini UCHUNGUZI hapa huhusisha pia utafiti wa kina kwa njia ya mahojiano na kwanjia ya kupitia nyaraka mbalimbali zinazopatikana kwa njia ama namna mbalimbali. Hebu lisaidieni taifa hili, mdhihirishe madai yenu kwamba ninyi mnastahili kuitwa mhimili wa Nne wa dola,

1. HAMZA KASONGO, Adamu SIMBEYE, Twaha ULIMWENGU na MAkwaiya wa KUHENGA: kwenye vile vipindi vyenu vya Luninga ambavyo Mimi huwa napenda kuja kuchangia mawazo yangu HEBU WEKENI Suala la UHALALI WA MALIPO YA TANESCO KWA DOWANS lijadiliwe na MAGURU wa Sheria za Mikataba hapa nchini ili tuone porojo ama ukweli uliomo ndani ya jambo hili
2. Kubenea SAED na Waandishi wengine nguli hebu tafuteni yaliyotendeka kule ICC maana taarifa iliyoenea zaidi ni kulipa mabilioni lakini mchakato ulivyokuwa ni watanzania wachache sana wanauelewa. Nafikiri hata Serikali haitaki Watanzania waelewe kilichijili huko ndiyo maana kauli zao zinagusigusia malipo tu.

LAKINI PIA Nanyi WANASIASA wa vyama vyote vya SIASA hapa ndiyo mahali penu TOENI kauli zenye kuwaonesha Watanzania umuhimu wa kuwepo kwenu kama vyama mbadala vinavyoweza kukabidhiwa nchi

NANYI WAHADHIRI NA WANAFUNZI huko vyuoni, toeni kauli zenu zenye kusheheni USOMI wenu katika hili. Siyo lazima kauli zenu zipingane na ICC ila semeni jambo kwa kadri ya uelewa wenu ulioko vichwani mwenu ilikulitumikia TAifa

VIVYO hivyo kwenu Maaskofu, wachungaji, Mashehe , mabudha na Wapagani pazeni sauti zenu juu ya hili, taifa nanyi litawalilia endapo mtaachia tu dhuluma ichukue mkondo wake. Lakini pia umuhimu enu kitaifa kwa watanzania utakuwa hupo mkiacha hili liende bila kauli zenu

Sijawasahau wakulima na Wafanyakazi kupitia vyama vyenu, nanyi mna waajibu

Sijasahau vyama vya wapiga debe kama vipo huko stendi za mabasi na daladala pazeni sauti zenu kuzima udhalimu

DUNIA HII HUWA MAHALI HATARI SANA KWA KUISHI SUYO TU KWA SABABU YA MAOVU BALI PIA KWA SABABU YA KUWEPO WATU WANAYOYAONA MAOVU YANATENDEKA LAKINI HAWACHUKUI HATUA. Mwanazuoni mmoja alipata kuneena haya


 
Thanks, good contribution, I appreciate this kind of mind contruction. Bravo Penguine
 
Sasa hapo mkuu umegusa kwenye kisogo manake unamtafuta ubaya yule mama Maajar balozi wetu kule USA!! Manake yeye ni partner wa hiyo REX Attorneys.....who knows may be amepelekwa jikoni kufungisha midomo watu huko USA

Watu gani unaosema??????.... kama ni watanzania waishio Marekani WAO WANAWAZA KUVAA FUBU habari za huku hata hawajui kinachondelea.... wao wanawaza kupata uraia wa huko wala sio kurudi

Matatizo haya tumeyataka wenyewe KWA KUMPA KIKWETE USHINDI WA KISHINDO 2005
 
Wait a minute ina maana REX Attorney walikuwa legal firm ya Richmond na ikisha wakaja wakawa wawakilishi wa Tanesco against Dowans bloody *** Hivi watanzania tumepatwa na nini? Tamaa au dhiki zetu wale wanasheria wa Tanesco hawakufanya their homework wakati wanatafuta wa kuwawakilisha? Au ndio ilikuwa inaandaliwa Tanesco ipatwe kushindwa maana fumbo mfumbie mjinga mwerevu hung'amua.

Ni kama sinema ya wakati wa vita kati ya Tanzania na Uganda halafu Mwl Nyerere akae aridhike tuu kwamba Nduli Iddi Amin keshajitokeza kutoa kikosi maalu cha kwenda kumlinda Mama Maria Nyerere na wanawe wote wasidhurike na mabaya ya vita, mmmmhhhh, ama kweli!!!!!!!!!!

And withis level of cruel professional misconduct for Advocate-turned-Diplomat Maajar, she will still be walking shoulder high in foreign countries as a dignitary without taking responsibility of all these to RESIGN from office.

With the Mega-Loss for our country to the tune of 185 billion shillings part of which Balozi Maajar will also be a beneficiary in professional fee, it is now clear that there MUST HAVE BEEN A DELIBERATE SYNDICATION OF THE WHOLE MATTER FOR ADVOCATE MAAJAR TO GO AND KILL TANESCO in court be offering fible representation before the law AGAINST DOWANS (RICHMOND DEVELOPMENT CORPORATION COMPANY which is sister company to DOWANS in business) as HER HEART had never stopped believing that the RICHMOND CONTRACT WITH TANESCO that has since been declared NULL AND VOID was ideal, safe and correct deal to enforce in the country. As a result of this act of stealing from public coffers using her legal profession, reasons why President Kikwete again had to immediately honour her with the position of becoming a diplomat at a distant location in Europe to shade her off from public eyes is yet to be known.

Now, within this muck of fraudulent dealings in the court corridors; Mrs Maajar and co advocates must face the wrath of Tanzanian tax-payers. The TANESCO Board of directors that appointed Mrs Maajar and Rex Attorneys which knowing very well that this was the legal representative of their first cheat company RICHMOND that later gave rise to a relation with yet another CHEAT-COMPANY whose owners will never surface, their personal properties be attahed immediately to make good the loss in question.

As the current AG keep insisting that 'HIS CLIENTS DOWANS' must just be paid, full stop, the company of the anonymous owners of DOWANS TANZANIA LIMITED and their implicit or explicit sponsors MUST immediately start preparing for 'a-mother-of-all-wars' with Tanzanian taxpayers so duppped of their funds. Lucky enough, all the names are in public domain.

Tanzanians, let's wake up and go for someone's neck on this scandlous fraudulent network played in the court corridors; home and abroad!!!!!
 
REX attorneys wamewakilisha RICHMOND na TANESCO at the same time wamewakilisha DOWANS.
Hapo ndipo NIMECHOKA kabisa
 
Ukisoma websites za hizi law firms utaoona Wazungu wapo.
Unajiuliza Je Hakuna Watanzania wenye ujuzi wa sheria kiasi chakuajiri Wazungu hawa?

Je una hela gani ya kuwalipa hawa WAZUNGU?
Ah,kama utafanya mikataba fake kwa niaba ya serikali,na kulipwa billioni 8 na BOT au billioni 5 za TANESCO unaweza kuajiri foreigners .

Do you think hizi firm zingekuwa zinashughulikia Human Rights only,hawa Wazungu wangeajiriwa?

WAKE UP TANZANIA,nchi inaliwa na mafisadi papa na vibaraka wao
 
Ndugu yangu mmakonde na WaTz wengine.
hakuna kinachoshindikana katika nchi hii.
Fanyeni mambo yenu tu kwani mtapata magonjwa ya moyo bure kwa kufuatilia mambo ya nchi hii.
miye mwenzenu moyo wangu ushakuwa sugu na vituko vya nchi hii.
 
Tatizo tunaofahamishwa haya mambo ni wachache wanaoelewa,na hii serikali inafanyo iwezalo ili watu wasielewe mambo yanavyoendeshwa..
 
inauma lazima tujuwe, kodi zetu jamani, Mungu ibariki Tanzania, mungu ibariki Africa
 
Wazungu wengi wameajiriwa TZ na Vibaraka wa Tanzania kama Mkono afanyafyo kwa kuwa sasa kwao uadirifu umeshika kasi sana na maendeleo ndio usiseme, Nchi yenye uongozi mbovu kama TZ kesi ndio aziishi, maana ni chukua chako mapema, na kwa kuwa Madvocate ndio wataalamu wa kupindisha sheria wakipata upenyo ndio wezi na matapeli wakubwa wa kimataifa, ndio wanoshirikiana na wazungu kuendeleza unnyonyaji, nilikuwa nafuatilia Makampuni Mengi kama yale ya Simu na madini wapo wengi sana wanalala mahoteli ya gharama, haya yote yafadhiliwa na Wanzania wenzetu kutumaliza huko wao wakineemeka, chukulia mtu kama Mkono alivyofanikiwa kupitisha rushwa kwa kutumia Ujanja wa M-pesa kuwaonga wajumbe pamoja na visim si unajua Vodacom mwenye shea kubwa ni RA, ndio kajaza Wazungu wengi sana,
 
Ukisoma websites za hizi law firms utaoona Wazungu wapo.
Unajiuliza Je Hakuna Watanzania wenye ujuzi wa sheria kiasi chakuajiri Wazungu hawa?

Je una hela gani ya kuwalipa hawa WAZUNGU?
Ah,kama utafanya mikataba fake kwa niaba ya serikali,na kulipwa billioni 8 na BOT au billioni 5 za TANESCO unaweza kuajiri foreigners .

Do you think hizi firm zingekuwa zinashughulikia Human Rights only,hawa Wazungu wangeajiriwa?

WAKE UP TANZANIA,nchi inaliwa na mafisadi papa na vibaraka wao
hili nalo neno
 
Monsignor, jina la Makani linaloonekana humo ni la; Victoria E.L.Makani,sina uhakika kama ni jamaa wa Bob au vipi. Lakini nijuavyo mimi Bob ni muislamu kwakuwa huyu ni mkristu uenda siyo mwanafamilia.
 
Kuna kitendawili kingine katika suala hili, inavyoelekea iliamriwa Dowans ilipwe dola 64 milioni ambazo ni sawa na shs.90 bilioni hivi, mimi sijui kwanini serikali inazungumzia kulipa shs 187 bilioni. ambazo ni zaidi ya mara mbili ya kiasi kilicho amriwa.
 
Richmond haikuwahi kuwakilishwa na REX Attorneys bali Law Associates. Angalieni Record zenu vizuri.
 
Back
Top Bottom