Balile kwa hili umekurupuka

Balile kwa hili umekurupuka

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,162
Reaction score
162,591
Akionge katika kipindi cha star tv cha Jicho letu ndani ya habari asubuhi ya leo,mhariri Balile ametoa taarifa ya uongo kuwa wanafunzi wa vyuo vya elimi ya juu wanalipwa sh1800,000 kwa miezi mitatu na ndio maana wanaendesha maisha ya anasa.

Pia ameongeza kuwa kutokana na hela nyingi wanazolipwa wakiwa chuoni husababisha wao kushindwa kuishi pale wanspoanza kazi kwa maana mishahara wanayolipwa inakuwa midogo kulingana na hela wanazolipwa wakiwa vyuoni.Balile ametoa mfano wa UD ambapo amesema ukienda bkock six utakuta wanafunzi wanaishi maisha ya anasa kwa kumiliki vitu kama TV na ipad ambazo amedai wanazitumia kuangalia picha za ngono badala ya kusoma.

Kwanza napenda kumwambia kama hana data bora akae kimya.Mwanafunzi analipwa sh 459,000 kama meals and accomodation allowance ikiwa na malipo kwa kipindi cha miezi miwili tu.Na ada inalipwa chuoni moja kwa moja.Sasa anapodai wanafunzi wanalipwa 1800,000 kwa miezi mitatu hizo taarifa kazitoa wapi?Cha kushangaza anadai eti hata ulaya hawatoi pesa kwa wanafunzi.Sasa hii kauli ina ukweli wowote ule?

Hivi kweli hawa ndio waandishi tunaoweza kuwategema kama taifa?Mwandishi gani mkongwe anakuwa na mawazo haya ya mwaka 47?!

Balile, kwa leo umechemka na umetia aibu waandishi wenzako!
 
Ndugu yangu we acha tu, jana nimemsikiliza Star tv,alianza kutoa data akawa anaelekea vizuri ila muda ukaisha. Leo sasa akaja na hoja zake za hao waliomtuma si ndio hapo sasa akaonyesha picha halisi alikuwa na lengo gani. Kwanza alianza kwa kujistukia kwamba eti amesikia watu wanasema ametumwa na serekali ambapo si vibaya hata akitumwa na serekali lakini aongee mambo yanayowahusu wananchi. Amejifanya ana uchungu na nchi na anaongea kama mtu wa mamlaka na sio kama muandishi wa habari. Ila haongelei kama mikataba itawekwa hadharani na kwanini wanazungumzia tu faida kama walivyoambiwa wananchi wa nyamongo, geita nk bila hizo faida kuonekana.

Ndugu yangu Balile sisi watanzania sio wajinga kama unavyodhani ama hao wanaokutuma wanavyodhani, tunaomba tuheshimiane na kila mtu afaidike na rasilimali zetu na usitake kujipatia mlo kwa kuja na propaganda wakati hali halisi tunaiona. Ungetuambia kama sera ya gesi imeshapitishwa tungekuelewa sio watu wapite shortcut wakutume wewe kwenye tv. Ukiweza muambie na yule mwenzako anayesema ni balozi wa Amani nadhani ni somebody mwaulanga kwamba aache mambo yange ya nadharia kwamba viongozi wa dini wanapewa ruhusa kwenda ikulu. Waambieni wanaowatuma waende kwanza kwa wananchi wa Mtwara wazungumze nao wakubaliane na kisha waje kwenye tv watueleweshe na sisi watanzania hatuna ugomvi nao.

Mungu ibariki Tanzania
 
Yaani leo ndio mnamshangaa Balile? Huyu naona huwa hajitambui anapotaka kuongea au anaugua ugonjwa wa megalomenia maana huwa anaongea vitu kuwa kuwa na variables. Na watu wote ambao huongea bila variables huja na vihoja vya takwimu ambazo ni inconsistent. Kwanza kuwaweka wanafunzi wote ndani ya kapu moja kuwa steriotype. Kama umewaona wanafunzi wa Hall 6 wakiwa na vitu vya anasa hivi kweli hiyo inamaanisha kuwa they are getting lion shares? Sasa anasa zenyewe kumbe TVs na IPADs ambazo nyingi ni second hand au counterfated from middles East and China. Sasa ukikua mwingine anatoka familia nzuri au save na kuweka scale of preference kweli utasema yuko overpaid?

Ushauri wangu kwa Balile kwanza yeye bado ni mdogo na anaweza kutumia fursa zilizopo kujiendeleza na kuhakikisha kuwa kabla hajaongea anatengeneza conceptual framework na anamwita yule anayemzidi katika upeo na ujengaji wa hoja ili amfanyie proof reading ya presentation yake aone kama ni viable au hydraheaded kama hoja aliyojenga ambayo uzi huu umesimama
 
Poleni vijana wa tanzania..
Huyu ni kibaraka wa mafisadi, uandishi wake maoni yake yote huwa anayatoa akiwa anawaza ni namna gani yatamsaidia Fisadi wake kuingia Ikulu...! Naona anawaza kupata cheo cha msemaji wa ikulu kama alivyopata Salva Rweyemamu!!

Kuna jambo alikuwa analiongea pia kuwa nchi za afrika zina haribiwa na mataifa ya nje pasee!! Ana akili kweli huyu yataingiaje bila kuwatumia watu walioko Afrika hasa viongozi!!?
 
Binafsi nimefatilia kipindi hicho na kuskiliza hoja zake kwa issue ya Mtwara.Tatizo nililoliona kwake ni kuja na kitu kipya cha Wana Mtwara kutumiwa na Watu toka nje hivyo anaona hawana hoja ila wanatumika tu! Kweli usomi wetu na fedheha kwa jamii zilizotusomesha!
 
Amesoma chuo gani huyo?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Akionge katika kipindi cha star tv cha Jicho letu ndani ya habari asubuhi ya leo,mhariri Balile ametoa taarifa ya uongo kuwa wanafunzi wa vyuo vya elimi ya juu wanalipwa sh1800,000 kwa miezi mitatu na ndio maana wanaendesha maisha ya anasa.Pia ameongeza kuwa kutokana na hela nyingi wanazolipwa wakiwa chuoni husababisha wao kushindwa kuishi pale wanaposnza kazi kwa maana mishshara wanayolipwa inakuwa midogo kulingana na hela wanazolipwa wakiwa vyuoni.Balile ametoa mfano wa UD ambapo amesema ukienda bkock six utakuta wanafunzi wanaishi maisha ya anasa kwa kumiliki vitu kama TV na ipad ambazo amedai wanazitumia kuangalia picha za ngono badala ya kusoma.Kwanza napenda kumwambia kama hana data bora akae kimya.Mwanafunzi analipwa sh 459,000 kama meals and accomodation allowance ikiwa na malipo kwa kipindi cha miezi miwili tu.Na ada inalipwa chuoni moja kwa moja.Sasa anapodai wanafunzi wanalipwa 1800,000 kwa miezi mitatu hizo taarifa kazitoa wapi?Cha kushangaza anadai eti hata ulaya hawatoi pesa kwa wanafunzi.Sasa hii kauli ina ukweli wowote?Hivi kweli hawa ndio waandishi tunaoweza kuwategema kama taifa?Mwandishi gani mkongwe anakuwa na mawazo haya ya mwaka 47?Balile kwa leo umechemka na umetia aibu waandishi wenzako.

Ni ukosefu wa exposure tu huyu. Msamehe bure opportunist mkubwa huyo. Atakuwa kaona ka-upenyo fulani tu hapo. Sijui hata kama ulaya kawahi kusoma akakuta wamefuta neno Full Scholarship. Msamehe bure huyo....
 
Mwaulanga na Balilie sijui kwanini wanaalikwa hapo.Wale wa Mwanza walikuwa wanatoa hoja ambazo zilionekana kuonyesha udhaifu wa watawala hasa hapa tanzania kitu ambacho mwandishi na mtangazaji Dotto Bullendu alikuwa anataka kukatisha.Simpendi na Juma lililopita niliandika kuhusu mtu huyu Risasi Mwaulanga anayejiita balozi wa Amani.Mimi namwona si balozi wa amani bali balozi wa Chuki.Anawalaumu watu wa dini.Anaonesha kabisa ana maslahi binafsi na CCM.Hili halina shaka.
 
Amesoma sekondari ya Kishoju kule kwao Kagera na baada ya shule alikuwa akifundisha shule ya sekondari Mugeza kuke Kagera. baadae alikwenda kusoma Saut Mwanza tena kwa kulipiwa na kanisa katoliki, baada ya hapo aliajiliwa mwananchi kama mwandishi kabla hajaokotwa na Mbowe na kumtumia kama mhariri kuanzisha Tanzania daima, baada ya hapo alipata scholaship ya hao wanaotumia watanzania (kama walimtumia na yeye may be) kwenda kusoma postgraduate kwao huko, aliporudi akakuta Kibanda kachukua nafasi yake hivyo kaenda kwa fisadi wa mafisadi Habari corporation akiandikia mtanzania. Kwa sasa alijinyofoa huko na kuanzisha jarida linaitwa gazeti la Jamhuri.
 
Akionge katika kipindi cha star tv cha Jicho letu ndani ya habari asubuhi ya leo,mhariri Balile ametoa taarifa ya uongo kuwa wanafunzi wa vyuo vya elimi ya juu wanalipwa sh1800,000 kwa miezi mitatu na ndio maana wanaendesha maisha ya anasa.Pia ameongeza kuwa kutokana na hela nyingi wanazolipwa wakiwa chuoni husababisha wao kushindwa kuishi pale wanaposnza kazi kwa maana mishshara wanayolipwa inakuwa midogo kulingana na hela wanazolipwa wakiwa vyuoni.Balile ametoa mfano wa UD ambapo amesema ukienda bkock six utakuta wanafunzi wanaishi maisha ya anasa kwa kumiliki vitu kama TV na ipad ambazo amedai wanazitumia kuangalia picha za ngono badala ya kusoma.Kwanza napenda kumwambia kama hana data bora akae kimya.Mwanafunzi analipwa sh 459,000 kama meals and accomodation allowance ikiwa na malipo kwa kipindi cha miezi miwili tu.Na ada inalipwa chuoni moja kwa moja.Sasa anapodai wanafunzi wanalipwa 1800,000 kwa miezi mitatu hizo taarifa kazitoa wapi?Cha kushangaza anadai eti hata ulaya hawatoi pesa kwa wanafunzi.Sasa hii kauli ina ukweli wowote?Hivi kweli hawa ndio waandishi tunaoweza kuwategema kama taifa?Mwandishi gani mkongwe anakuwa na mawazo haya ya mwaka 47?Balile kwa leo umechemka na umetia aibu waandishi wenzako.

Sasa tatizo ni nini hapo? si ni 230,000/= kwa mwezi?
Kwa mwaka mmoja unapata sh 2,760,000/=.
Hata ukipanga chumba cha sh 30,000 kwa mwezi utatumia sh 360,000 kwa mwaka.Ukitumia sh 60,000 kwa mwezi kwa chakula jumla ni sh 720,000/= na kuvaa,vitabu nk huwezi maliza 2,760,000 kama kweli uko makini.
Hii fedha wadongo zangu mtaijutia pindi mkiingia uraiani?
tatizo lenu wengi wenu mnajitumbukiza katika siasa na anasa huo ni ukweli sema si wote!
 
Haya ni majanga ya waandishi wetu wa kibongo! Anakula kwa mafisadi
 
Sasa tatizo ni nini hapo? si ni 230,000/= kwa mwezi?
Kwa mwaka mmoja unapata sh 2,760,000/=.
Hata ukipanga chumba cha sh 30,000 kwa mwezi utatumia sh 360,000 kwa mwaka.Ukitumia sh 60,000 kwa mwezi kwa chakula jumla ni sh 720,000/= na kuvaa,vitabu nk huwezi maliza 2,760,000 kama kweli uko makini.
!

Kwenye red: 153,000/=

Endelea na ukokotoaji.
 
Sasa tatizo ni nini hapo? si ni 230,000/= kwa mwezi?Kwa mwaka mmoja unapata sh 2,760,000/=.Hata ukipanga chumba cha sh 30,000 kwa mwezi utatumia sh 360,000 kwa mwaka.Ukitumia sh 60,000 kwa mwezi kwa chakula jumla ni sh 720,000/= na kuvaa,vitabu nk huwezi maliza 2,760,000 kama kweli uko makini.Hii fedha wadongo zangu mtaijutia pindi mkiingia uraiani? tatizo lenu wengi wenu mnajitumbukiza katika siasa na anasa huo ni ukweli sema si wote!
Acha kutetea hoja za upotishaji!Anapodai mwanafunzi analipwa sh 1800,000 kwa miezi mitatu ina maana hajui au ana malengo yake?Hawa waandishi hata matatizo kama haya ya wanafunzi hawayajui ingawa ni ya kila siku!Mwandishi unapaswa kuwa mchunguzi ili umudu vizuri fani yako.
 
Mi sikusikiliza hayo lakini kinacho ongewa na watu ni kwamba huyu jamaa ni kibaraka!
 
Akionge katika kipindi cha star tv cha Jicho letu ndani ya habari asubuhi ya leo,mhariri Balile ametoa taarifa ya uongo kuwa wanafunzi wa vyuo vya elimi ya juu wanalipwa sh1800,000 kwa miezi mitatu na ndio maana wanaendesha maisha ya anasa.Pia ameongeza kuwa kutokana na hela nyingi wanazolipwa wakiwa chuoni husababisha wao kushindwa kuishi pale wanaposnza kazi kwa maana mishshara wanayolipwa inakuwa midogo kulingana na hela wanazolipwa wakiwa vyuoni.Balile ametoa mfano wa UD ambapo amesema ukienda bkock six utakuta wanafunzi wanaishi maisha ya anasa kwa kumiliki vitu kama TV na ipad ambazo amedai wanazitumia kuangalia picha za ngono badala ya kusoma.Kwanza napenda kumwambia kama hana data bora akae kimya.Mwanafunzi analipwa sh 459,000 kama meals and accomodation allowance ikiwa na malipo kwa kipindi cha miezi miwili tu.Na ada inalipwa chuoni moja kwa moja.Sasa anapodai wanafunzi wanalipwa 1800,000 kwa miezi mitatu hizo taarifa kazitoa wapi?Cha kushangaza anadai eti hata ulaya hawatoi pesa kwa wanafunzi.Sasa hii kauli ina ukweli wowote?Hivi kweli hawa ndio waandishi tunaoweza kuwategema kama taifa?Mwandishi gani mkongwe anakuwa na mawazo haya ya mwaka 47?Balile kwa leo umechemka na umetia aibu waandishi wenzako.

Kuhusu umiliki wa vitu hivyo wanafunzi wa ulaya uvipata kwa kufanyakazi, hela ya serikali wanayopewa ni ndogo sana, maana wanapewa hela kulingana na uwezo wa mzazi ( yaani kama mzazi anapata mshahara mkubwa GROSS kwa mwaka na hela ya serikali inapungua)
Hata hivyo bado sio hela ndefu ni hela ya room,chakula na nauli za kila siku hakuna salio kwenye hiyo hela kutosha kununua vitu kama TV au iPad hata ujibane vipi, sana hela yote inakwisha kwenye nauli, wazazi wenyewe wanafunzi vyuoni wana support watoto wao kutokana na udogo wa fungu wanalopewa.

Hela wanayopewa mkononi ni ya accomodation (chakula,makazi, nauli) hela ya vitabu hawapewi mikononi ila wanapewa kadi maalumu au vocha ambayo utumika kwenye maduka maalumu hapo chuoni,
Vyuo lazima vibuni mifumo ambayo itasadia mwanafunzi na vyuo vyenyewe, kwa mfano mwanafunzi anapopewa hela ya vitabu basi iwe katika vocha na zitumike kwenye maduka ya vyuo ili kulinda ubora wa materials ambazo wanafunzi wanatumia kujiaanda na masomo yao.
Hii itasaidia wanafunzi kununua vitabu badala ya vitu ambavyo avikulengwa, hizo vocha ziwe na expiring time na sio transferable, mifumo bora inatakiwa chuoni,
fungu wanalolipwa wanafunzi lifanyiwe utafiti upya kuona kama linaendana na hali halisi ya maisha ya mwanafunzi, pesa anayopewa mwanafunzi ni kwa ajili ya kumudu masomo na sio vinginevyo,
 
Unajua unapoongea vitu vingine lazma ufikirie, hv hajui maisha ya wanafunzi wengine kuanzia manyumbani kwao ni ya juu? Au anafikiri wote wanategemea mkopo? Aache weus.
 
Sasa tatizo ni nini hapo? si ni 230,000/= kwa mwezi?
Kwa mwaka mmoja unapata sh 2,760,000/=.
Hata ukipanga chumba cha sh 30,000 kwa mwezi utatumia sh 360,000 kwa mwaka.Ukitumia sh 60,000 kwa mwezi kwa chakula jumla ni sh 720,000/= na kuvaa,vitabu nk huwezi maliza 2,760,000 kama kweli uko makini.
Hii fedha wadongo zangu mtaijutia pindi mkiingia uraiani?
tatizo lenu wengi wenu mnajitumbukiza katika siasa na anasa huo ni ukweli sema si wote!

Mathias Byabato kumbe na wewe ndo wale wale. Msipende kukurupuka kuandika vitu msivyo na uhakika navyo.

Kwanza unafahamu mwanafunzi wa elimu ya juu analipwa shilingi ngapi kwa siku?(meals and accomodation allowance). Kama hujui ni bora ukae kimya kuliko kuandika madudu.
 
Last edited by a moderator:
Sasa tatizo ni nini hapo? si ni 230,000/= kwa mwezi?
Kwa mwaka mmoja unapata sh 2,760,000/=.
Hata ukipanga chumba cha sh 30,000 kwa mwezi utatumia sh 360,000 kwa mwaka.Ukitumia sh 60,000 kwa mwezi kwa chakula jumla ni sh 720,000/= na kuvaa,vitabu nk huwezi maliza 2,760,000 kama kweli uko makini.
Hii fedha wadongo zangu mtaijutia pindi mkiingia uraiani?
tatizo lenu wengi wenu mnajitumbukiza katika siasa na anasa huo ni ukweli sema si wote!

kama hujui ki2 usiongee ki2 aliyekwambia 2napewa pesa kama hyo ni nani?1.chuoni ha2kai miez 12 kama hesabuzako zilivyo, it wrong calculation, Meal and accomadation,tsh 1836000/ kwa miezi 8, hapo kuna pango la nyumba, kumalizia ada coz magamba hawatoe 100%,2. Photocopy na kunua vitabu hapo hapo, 3.nauli wakati wa likizo hapo hapo so hakuna anaye fanya asana kwa sababu ya hyo pesa coz haitoshi! Kabisa pole
 
Back
Top Bottom