Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limewajulisha Waislamu na wananchi wote kwa ujumla kuwa Sikukuu ya Eid El-Fitri itakuwa Machi 20, au 21, 2026 kutegemea mwandamo wa mwezi na kueleza kuwa sherehe za Eid El-Fitri kitaifa kwa mwaka huu zitafanyika Mkoa wa Dar es Salaam.
Taarifa ya leo Machi 12, 2026 iliyotolewa na BAKWATA imebainisha kuwa Swala ya Eid itaswaliwa katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI BAKWATA Makao Makuu Kinondoni kuanzia saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere Convention Centre kuanzia saa 09.00 mchana Inshallah.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Mgeni Rasmi katika Baraza la Eid atakuwa Rais wa Samia Suluhu Hassan.
Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dkt. Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally Mbwana amewatakia Waislamu wote Swaumu njema katika kumi la mwisho la mwezi Mtukufu wa Ramadhani na maandalizi mema ya Sikukuu ya Eid El-Fitri huku akiwaomba kuhudhuria kwenye Ukumbi kwa wingi na kwa wakati.
Taarifa ya leo Machi 12, 2026 iliyotolewa na BAKWATA imebainisha kuwa Swala ya Eid itaswaliwa katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI BAKWATA Makao Makuu Kinondoni kuanzia saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere Convention Centre kuanzia saa 09.00 mchana Inshallah.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Mgeni Rasmi katika Baraza la Eid atakuwa Rais wa Samia Suluhu Hassan.
Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dkt. Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally Mbwana amewatakia Waislamu wote Swaumu njema katika kumi la mwisho la mwezi Mtukufu wa Ramadhani na maandalizi mema ya Sikukuu ya Eid El-Fitri huku akiwaomba kuhudhuria kwenye Ukumbi kwa wingi na kwa wakati.