BAKWATA yakosoa Washukiwa wa Ugaidi kuuawa kabla ya kufikishwa Mahakamani

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,618
Katika maoni yake kwa Tume hiyo, Bakwata imeshauri kuboresha vipengele vya sheria tano, ikiwamo ile ya kuzuia ugaidi ya mwaka 2002 inayotoa mamlaka kwa polisi kupiga risasi na kumuua mtuhumiwa wa ugaidi kabla ya kuthibitishwa mbele ya mahakama.

“Watuhumiwa wanauawa kabla ya mahakama kuthibitisha, unamuuaje wakati mahakama haijathibitisha? Kwa nini asitumie mbinu nyingine za kumkamata? Kama mahakama ndiyo eneo la kutoa haki, mamlaka haya yanakuwepo kisheria kwa nini?” alihoji mwanasheria wa baraza hilo, Hassan Fatiu.

Mjadala kuhusu suala kama hilo uliibuka baada ya Jeshi la Polisi kueleza umma kwamba uchunguzi wake ulibaini mtuhumiwa wa ugaidi, Hamza Mohammed (30) alikuwa gaidi.

Hamza aliuawa Agosti 25 mwaka huu nje ya geti la Ubalozi wa Ufaransa katika Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, baada kufanya shambulio na kuua askari wanne, akiwamo mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi na kujeruhi wengine sita.

Fatiu alisema sheria hiyo pia imejenga mtazamo hasi kwenye jamii kutokana na waathirika wengi kuwa kundi la imani fulani.

Maoni hayo yamekuja wakati kukiwa na malalamiko ya baadhi ya watuhumiwa wa ugaidi, wakiwemo masheikh kusota miaka mingi gerezani bila kesi zao kumalizika.

Chanzo: Mwananchi
 
Back
Top Bottom