BAKWATA Yakataa Serikali 3

BAKWATA Yakataa Serikali 3

Deo Corleone

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2011
Posts
17,023
Reaction score
13,370
Hivi Tanganyika yetu itarudi kweli?
source:Magaazetini _RFA.
 
Mkisharudisha Tanganyika mtanufaikaje? ili iweje. Hongera bakwata.
 
Hoja zenu za kutaka Tanganyika ni dhaifu na zimetawaliwa na chuki na ulevi.
Ni zao la chuki aliyo ipandikiza mtikila. Hakuna manufaa ya kiuchumi wala ya kijamii yatakayo patikana kwa kurudisha serikali tatu. Achaneni na siasa za chuki na jazba
 
Hoja zenu za kutaka Tanganyika ni dhaifu na zimetawaliwa na chuki na ulevi.
Ni zao la chuki aliyo ipandikiza mtikila. Hakuna manufaa ya kiuchumi wala ya kijamii yatakayo patikana kwa kurudisha serikali tatu. Achaneni na siasa za chuki na jazba

Umesahau na chuki aliyoieneza Padri Slaa
 
BAKWATA NI JUMUIYA YA CCM!!!inawafuasi wachache sana
 
Naona tunakoelekea itakuwa ni Kura kati ya Wakristo (3) na Waislam (2); maana waislamu wanaona Zanzibar ikijitenga na kuwa serikali kamili mara moja itakuwa nchi ya Kiislam huku Tanganyika ikichagizwa kuwa nchi ya kikiristo. Kazenji kadogo na kanategemea Bara. Haha ha kazi ipo. Ngoja niishie hapa wasije wakakaba wenye Zanzbar yao.
 
Hivi Tanganyika yetu itarudi kweli?
source:Magaazetini _RFA.

Wee waache wafanye hashuo lao tu! Mwisho wa siku huo upuuzi wanaouandika kwenye katiba lazima ukubaliwe na majority ya Tanganyika na majority ya Zanzibar!
Naamini katiba inaweza ikapita Tanganyika, but nauhakika katiba itafeli kwa kukataliwa Z'bar!
Na hapo kitakachofata ni Mungu aturehemu! CCM wanacheza ngoma wasioijua!
 
Hoja zenu za kutaka Tanganyika ni dhaifu na zimetawaliwa na chuki na ulevi.
Ni zao la chuki aliyo ipandikiza mtikila. Hakuna manufaa ya kiuchumi wala ya kijamii yatakayo patikana kwa kurudisha serikali tatu. Achaneni na siasa za chuki na jazba

Hizi serikali kama ni mzuri kwanini zipingwe na majority ya Watz?
 
Wanaotaka serikali tatu ni wale waliopanga kugawana vyeo wala siyo kuimarisha nchi.
 
Muundo ambao utaimarisha umoja na mshikamano wa taifa hili ni serikali mbili.
 
Wanaotaka serikali tatu ni wale waliopanga kugawana vyeo wala siyo kuimarisha nchi.

Mngekuwa na akili mngesema ili kuondoa hizi kelele basi twende kwenye serikali moja na nchi moja tu, vinginevyo safari hii hamtapata mlango wa kutokea
 
Hoja zenu za kutaka Tanganyika ni dhaifu na zimetawaliwa na chuki na ulevi.
Ni zao la chuki aliyo ipandikiza mtikila. Hakuna manufaa ya kiuchumi wala ya kijamii yatakayo patikana kwa kurudisha serikali tatu. Achaneni na siasa za chuki na jazba

Kama ni hivyo unaonaje tukiwa na NCHI MOJA NA SERIKALI MOJA ili tuwe na manufaa ya kweli ya kiuchumi na kijamii?. Pia tutakua na umoja na mshikamano wa dhati na pia tutaokoka gharama za kuendesha serikali tatu. Unaonaje mkuu?
 
Kama ni hivyo unaonaje tukiwa na NCHI MOJA NA SERIKALI MOJA ili tuwe na manufaa ya kweli ya kiuchumi na kijamii?. Pia tutakua na umoja na mshikamano wa dhati na pia tutaokoka gharama za kuendesha serikali tatu. Unaonaje mkuu?

Infact malalamiko ya wa Zanzibari kuhusu muungano yana make sense kuliko ya Wabara. Wao wana sababu za kiuchumi. Sisi tuna lalamika eti wao wana bendera sijui katiba yao imekuaje, and all nosense. Ili kutoimeza zanzibar na kuifanya kama mkoa kuna umuhimu wa wao kuwa na serikali yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom