Bakhresa achangia bajeti $800k

Bakhresa achangia bajeti $800k

MJIMPYA

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
506
Reaction score
273
Ni kampuni ya SSB imechangia wizara ya uchukuzi USD800,000 ili mabehewa ya treni yatengenezwe.

Anastahili pongezi.

Source: TBC jana.

==================
Ufafanuzi zaidi
==================

Muwe mnasoma bajeti vizuri na kuelewa Bakhera hajachangia hata kumi.. waziri kaeleza hivi - NANUKUU;

"Napenda kuchukua fursa hii kuipongeza kwa dhati kampuni ya kitanzania ya S.S Bakhresa kwa kuitikia mpango huo na kutoa dola laki 8 ambazo zimetumika kukarabati vichwa 2 vya train aina ya 73xx. vichwa hivo vinatumika pamoja na kazi nyingine kusafirishia ngano kutoka DSM mpaka mwanza kwa ajili ya soko la S S Bakhresa la Uganda. vile vile kampuni ya TICTS ltd imeonesha nia ya kutoa kiasi hicho hicho cha fedh kukarabati vichwa 2 vya injine aina ya 64xx na mabehewa 20 kwa ajili ya kusafirishia makasha kutoka bandari ya dsm kwenda kituo cha makasha cha Ubungo"
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure
 
KWA MARA YA KWANZA KATIKA HISTORIA YA TANZANIA!
Na huenda ni kwa mara ya mwisho...!
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure
ni kweli Kigogo!na kuchangia gani hadi atoe na directives za hiyo hela itumike wapi!!!
 
Last edited by a moderator:
Inawezekana kabisa,keshapewa tenda ya kuendesha mradi wa treni,hapa jijini Dar.

Kwa kuwa nakumbuka jana,waziri wa uchukuzi, Dr Mwakyembe,alitangaza kwenye bajeti yake kuwa,serikali ina mpango WA kubinafsisha,mradi wa treni,jijini Dar.

Kwa mtindo wa serikali hii,ingawa waziri Mwakyembe,ametuambia kuwa kampuni 14,zimebid tenda hiyo,upo uwezekano mkubwa kuwa Bakhresa,keshajibiwa na kuambiwa keshapewa tenda hiyo,hata kabla kikao cha tender board hakijakaa!!
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure



Wabongo na sisi tumezidi, sijui mtu afanyeje ndiyo atasifiwa!Juzi juzi ililetwa thread kuwa amekuwa miongoni mwa mabilionea wa Afrika kwenye list ya Forbes watu mkahoji anachangia nini kwenye pato la taifa na wengine wakasema huyu jamaa hatoi msaada wowote kwa watanzania wenzake, leo anachangia bajeti ya wizara mnaponda tena sijui afanyeje sasa?
 
cha msingi ni usimamizi wa hizo fedha ili zikafanye jambo lililokusudiwa.
 
Muwe mnasoma bajeti vizuri na kuelewa Bakhera hajachangia hata kumi.. waziri kaeleza hivi NANUKUU
Napenda kuchukua fursa hii kuipongeza kwa dhati kampuni ya kitanzania ya S.S Bakhresa kwa kuitikia mpango huo na kutoa dola laki 8 ambazo zimetumika kukarabati vichwa 2 vya train aina ya 73xx. vichwa hivo vinatumika pamoja na kazi nyingine kusafirishia ngano kutoka DSM mpaka mwanza kwa ajili ya soko la S S Bakhresa la Uganda. vile vile kampuni ya TICTS ltd imeonesha nia ya kutoa kiasi hicho hicho cha fedh kukarabati vichwa 2 vya injine aina ya 64xx na mabehewa 20 kwa ajili ya kusafirishia makasha kutoka bandari ya dsm kwenda kituo cha makasha cha Ubungo
 
Kama amechangia serikalini bora zaidi ya zile wanazotoa kuisaidia CCM.

What is the different between CCM and Serikali when the same crooks use government funds for their family manure? Fedha za serikali zinaishia mifukoni mwa magamba kwa njia moja au nyingine. Miradi ya maendeleo inakufa kwa mtindo huo huo. Badala ya kutumia 200m kwa kujenga visima, wanatumia 180 kununua gari la mradi ambalo baada ya miaka miwili wanajiuzia wenyewe at disposal
 
Back
Top Bottom