Bajeti ya 2009/2010 Tanzania

Naomba aliyekwisha ku-download kijarida cha cheche 41 anitumie kwenye private email kwani nashindwa kudownload hapa nilipo
 
Najuuuuuuuuuuta kuifahamu hii sirikali. Najuuuuta. Kuna mikoa TZ lami hawaijui Rukwa na Kigoma kwa uchache. Kuna wilaya ambazo kwa uchumi wake zapaswa kuunganishwa kwa lami lakini bado mavumbi tu lol. Aliyenacho kweli ataongezewa.
 
Hizi Kamati hazina nguvu yeyote ikija kwenye maslahi ya Taifa.
Na hao wana 'miogomvi yao wenyewe'
Mengine Je?
Hizi Ni siasa za siasa.
 
Hili ndiyo moja wapo la tatizo la waziri kuwa mbunge pia.

Waziri yeyote atataka afanye walau kitu cha maana jimboni mwake ili apate cha kusema wakati wa kuomba kura. Ila pia waziri ana takiwa kufanyia kazi watanzania wote. Sasa waziri achague nini, kupendelea jimbo lake ili apate kura au kuli tumikia taifa zima? Atasema bora kupendelea jimbo lake maana ndiyo wanaompa kura na si Tanzania nzima.

Hii system yetu mara nyingi inaleta conflict of interests na ndiyo chanzo cha matatizo yetu mengi.

hii ni kweli kabisa, huwezi kufikiria majimbo mengine na wapiga kura wako hujawaridhisha.
Lakini hata hivyo barabara kama ndiyo hiyo inayoongelewa (lushoto-kilosa-Mikumi) bado ni ya muhimu kwa maendeleo
 
Najuuuuuuuuuuta kuifahamu hii sirikali. Najuuuuta. Kuna mikoa TZ lami hawaijui Rukwa na Kigoma kwa uchache. Kuna wilaya ambazo kwa uchumi wake zapaswa kuunganishwa kwa lami lakini bado mavumbi tu lol. Aliyenacho kweli ataongezewa.

atafutwe mtu wa maeneo hayo apewe uwaziri wa fedha! kwikwikwikwikwi yaani hata Pinda hawamwogopi? Tehetehetehe
 
Ni kweli Mkuu Magufuri knows the answer,

Lakini kama ulisha wahi pita barabara ya Tabora kwenda Kigoma.. ambayo kimsingi ni muhimu sana kwani inauunga mkoa wa Kigoma kwa sehemu nyingine hivyo kuharakisha maendeleo yake,

[SIZE=3]I mean kama umepita huko hasa wakati wa mvua, leo hii ukaja ona mabilioni yanatengwa eti kutengeneza barabara kama ya msata and whatever.. haingii akilini kabisa! Huu ni uhuni na ubinafsi wa hali ya juu![/SIZE]

Na sidhani kwamba ni busara kuipendelea sehemu moja ya nchi wakazi wake wapate maisha mazuri ili hali wengine ni fukara wa kutupwa! Wakati kodi unazifata huko huko kwa mafukara hao bila huruma.
Kwa kweli inashangaza kufanya upendeleo wa wazi. Hebu tujaribu kufikiria hili, Bagamoyo kunatarajiwa pia kujengwa Bandari. Ni umbali usiozidi 6okms kutoka bandari ya Dar. Bandari ya Dar inashindwa kufanya kazi kwa ufanisi hadi JK anafunga safari za mara kwa mara bandarini hapo ili angalau mambo yaende. Bandari ya Tanga iliyo umbali usiozidi 300Kms kutoka Dar, hakuna msaada wowte wa kuifanya iwe mmbadala wa ile ya Dar. Itaingiaje akilini kuanzisha bandari mpya Bagamoyo wakati hizi mbili achilia ya Mtwara ziko hoi bin taabani. Au kwa kuwa Kawambwa na JK wanatoka huko! Kuna nini hasa kikubwa cha kukuza uchumi hapo Bagamoyo kushinda Korosho za Mtwara, Mahindi ya Ruvuma na Rukwa? Tusishangae kusikia hata upanuzi wa Uwanja wa Ndege Dar ukahamishiwa Bagamoyo.
 
Kwa kweli inashangaza kufanya upendeleo wa wazi. Hebu tujaribu kufikiria hili, Bagamoyo kunatarajiwa pia kujengwa Bandari. Ni umbali usiozidi 6okms kutoka bandari ya Dar. Bandari ya Dar inashindwa kufanya kazi kwa ufanisi hadi JK anafunga safari za mara kwa mara bandarini hapo ili angalau mambo yaende. Bandari ya Tanga iliyo umbali usiozidi 300Kms kutoka Dar, hakuna msaada wowte wa kuifanya iwe mmbadala wa ile ya Dar. Itaingiaje akilini kuanzisha bandari mpya Bagamoyo wakati hizi mbili achilia ya Mtwara ziko hoi bin taabani. Au kwa kuwa Kawambwa na JK wanatoka huko! Kuna nini hasa kikubwa cha kukuza uchumi hapo Bagamoyo kushinda Korosho za Mtwara, Mahindi ya Ruvuma na Rukwa? Tusishangae kusikia hata upanuzi wa Uwanja wa Ndege Dar ukahamishiwa Bagamoyo.[/QUOTE]

Mkuu kwani hiyo hujaisikia? Hiyo iko mbioni na tulisha ijadili sana humu..., na si hiyo tu nasikia pia wanaweka EPZ ile tu km chache kabla ya kufika Bagamoyo mjini, na kwa taarifa yako, wale wazee wa bagamoyo wameelezwa ardhi yao wasiuze, sasa viwanja havikamatiki, kuna kitu wanaita kieneo, hawaoni haya kukutajia mil 5, kwani wameambiwa mji wahamia huko, Bandari, uwanja wa ndege, EPZ Mungu awape nini??

Cjui masikini kule kwetu madongo kuinama nani aweza kuwa presidaa nasi tukakumbukwa katika ufalme wa Tanzania?

Nimeshangazwa sana na hili, cjui Nyerere naye angeamua kila kitu Butiama ingekuwaje?
 
Wandugu,
Pamoja na yote kwa waziri yryote kama umefuatwa na watendaji na wanakwambia hii barabara inakwenda kwa mwenye kaya lazima ipigwe lami. Nafikiri hakun a atakayebisha, hapa tu kwenye forums kuna watu wanasadikiwa ndo vingune wa forum hii hata wakiandika pumba watu wanashangilia na mtu akihoji anaambiwa anatumiwa. Ukweli hapa huu ni wakati JK aonyeshe maturity, aikatae hiyo barabara kama kweli yuko kama raisi wa watanzania wote.
 
Hivi ni kawaida Bunge la lala salama linakuwa la kuelezana ukweli. Na hivi Tanzania sikuhizi huru kuongea unaloamini.

Tusubiri, only tunawashauri wasijefanya kama majirani zetu makonde yakatambea pale Dodoma.
 
Nakumbuka ile barabara ya Msata kwenda Bagamoyo, ilikuwa na nia ya kuwa na alternative route in case kukiwa na tatizo daraja la Ruvu.

Hivi ndiyo barabara mnaongelea au ndio ipi?
 
hii ni kweli kabisa, huwezi kufikiria majimbo mengine na wapiga kura wako hujawaridhisha.
Lakini hata hivyo barabara kama ndiyo hiyo inayoongelewa (lushoto-kilosa-Mikumi) bado ni ya muhimu kwa maendeleo

Ni kweli inaweza kuwa ya muhimu kwa taifa ila bado kuna comflict of interest. Hata kama ni ya maendeleo kwa sababu ni kwa jimbo lake lazima watu wata jiuliza. Na angalia timing la swala lenyewe. Mkullo kaitoa mwaka mmoja kabla ya uchaguzi ina maana kama iki kubaliwa by the time kampeni zikianza mwakani ujenzi utakua ushaanza na anaweza kusema mnaona? Swala ni je kama ni kwa ajili ya taifa wakati wa kampeni hataitumia hiyo barabara kuombea kura? Narudia tena, inaweza kuwa kwa manufaa ya taifa lakini as long as there arecomflicting interests ni vigumu kujua motives za Mkullo.
 
ndio maana kuna umuhimu wa kuwa na utaratibu wa kuteua mawaziri nje ya bunge. mbunge anapokuwa waziri, anakosa ule uhuru wa kuisimamia serikalikwa sababu na yeye anakuwa sehemu ya serikali anayotakiwa kuisimamia.

Ume patia mkuu. Kazi kubwa ya mbunge ni kusimamia serikali. Sasa akiwa waziri halafu ni mbunge wajibu wake ni upi? Kwa serikali au wananchi? Ingeeleweka zaidi kama mtu akipewa uwaziri akavua ubunge. Maana hapa ni lazima achagua moja kutumikia taifa zima ama jimbo na hawezi kufanya yote hayo kwa wakati mmoja.
 
Mi iwa wananiudhi hawa mawaziri wa Fedha kupandisha kodi ya vinywaji sasa sijui mnataka kutukomoa au inakuwaje?Mbona madini kule hampandishi kodi na watu wachache wananeemeka kupitia migodi. Jaribuni kuwa wabunifu nyie mawaziri wa Fedha sio vinywaji tu ndo mnako patia kodi.
 
Mzalendo Halisi,

Gari analotumia Askofu wa RC sio lake, ni la Jimbo. Hana gari, hana mke, ni mtumishi tu wa Taifa la Mungu. Utamdai kodi toka pato lipi? (Hana pato).

"Askofu" wa kujipachika "Uaskofu" mwenyewe kama akina Kakobe ni haki kabisa alipe kodi. Wana income, tena kubwa. Lakini akianzisha taasisi ya kuhudumia watu bila kutafuta faida, kama hospitali, basi isilipe kodi.
 
Kama kawa TBL TCC cocacola na viwanda vya spirits jiandaeni na bonge la kodi. Ila mjua hata mpandishe Kodi vipi Bia hatuachi. Kuna maeneo mengi sana y akupata mapato ila serikali haiko creative. Hivi nchi hii kuna TUME YA MIPANGO?

Unajua kuwa wadanganyika tunalipa kodi nyingi sana. Ukiangalia kwenye vileo kodi ikiongezwa inatukumba sisi watumiaji na sio kwenye kiwanda husika. ukia kwenye Salary kuna PAYE inatukamua. yani kila mahali kodi lakini nchi bado masikini kabisa. hivi watanzania tumelogwa???
 





Na Restuta James



6th June 2009
















Slaa.jpg

Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk. Willbrod Slaa.



Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk. Willbrod Slaa, amesema bajeti ya mwaka huu imetungwa kisiasa zaidi jambo ambalo halitaleta tija kwa taifa na haitawasaidia wananchi.
Amesema pia kuwa kitendo cha serikali kutegemea fedha zote za maendeleo kutoka kwa wahisani, kinaweza kuiumiza nchi iwapo wafadhili watashindwa kutoa fedha kutokana na msukosuko wa kiuchumi unaoendelea duniani.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa alisema pamoja na mtikisiko wa kiuchumi duniani, serikali haijaonyesha mipango madhubuti ya kukabiliana na hali hiyo. Alisema hata vipaumbele vilivyainishwa ni vingi mno ikilinganishwa na kiasi cha fedha kilichopo.
"Mimi nadhani kwa sababu wimbo wa serikali kwa sasa ni 'Kilimo Kwanza' nilitarajia kuwa vipaumbele vingekuwa Elimu, Afya na Kilimo ili tuweze kuziba pengo la uhaba wa chakula lililopo...ni aibu kwa nchi kama Tanzania yenye ardhi ya kutosha kuomba chakula nje, serikali inatakiwa kuwa makini katika kuinua kilimo," alisema.
 
Ndg. Yangu Dr. Slaa,

Kama kipaumbele ni kutenga hela tu bila kuweka hata matayarisho ya hizo hela zitumike vipi then I'm lost.

Kwa mfano isingekuwa busara kutenga fedha za kilimo kwa ongezeko la 100% yet ukijua kwamba bado actual kilimo kinafanywa na sekta binafsi, kazi ya serikali ni kugenga miundo mbinu na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji kwenye kilimo.

Sidahani ndani ya mwaka unaweza kufanya feasibility study, utape mjenzi wa mifereji, uweke mashamba yalimwe na yavunwe... la muhimu ni kwamba progressively hela zitengwe za kutosha kwa miaka zaidi ya mitano ijayo kwenye kilimo.

Na wewe pia usiongee kisiasa kama serikali, by the way wewe si mwanasiasa kila unalosema si siasa tu.

Ikumbukwe kwamba uwekezaji kwenye miundo mbinu kwenye maji ni sehemu ya uwekezaji kwenye kilimo!
 
Wakuu mwenye access na hiyi budget tafadhari naomba aipost hapa. tuweze kuipitia pia. Nimejaribu kugoogle sijapata isipokuwa summary za magazetini tu
 
Mi iwa wananiudhi hawa mawaziri wa Fedha kupandisha kodi ya vinywaji sasa sijui mnataka kutukomoa au inakuwaje?Mbona madini kule hampandishi kodi na watu wachache wananeemeka kupitia migodi. Jaribuni kuwa wabunifu nyie mawaziri wa Fedha sio vinywaji tu ndo mnako patia kodi.


Mkuu hii diyo kansa ya bajeti ya Tanzania! siku macho yao yakifumbuka wakaangalia vyanzo mbadala, Tanzania itabadilika maramoja.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom