Nsaji Mpoki
JF-Expert Member
- Nov 5, 2007
- 396
- 65
Ni kipindi cha maandalizi ya kupitisha bajeti ya serikali kwa mwaka 2009/2010. Pilika pilika zimeanza ambapo Wizara na Mikoa zitatakiwa kupeleka makisio yao kwa ajili ya mapitio kabla Kamati za Bunge hazijakaa na kupitia na kisha Bw. Fedha wa Taifa Mustafa Nkullo atawasilisha kwenye Bunge la Juni. Huo ni mchakato ambao huanzia kwa Wizara na Mikoa kupewa ceilings za fedha kwa matumizi ya kawaida (Other charges) na fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo (development fund). Kwa maka ujao wa fedha kila Wizara, Idara ya Serikali, Mikoa na Halmashauri imetakiwa kupunguza bajeti kwa asilimia 20 kwa maelezo kuwa hali ya uchumi kidunia si nzuri. Tuache hayo; nina hoja mbili za msingi kuhusu bajeti hii; Moja; ni kama Waziri Mkuu anakumbuka kama kipindi hiki ni cha bajeti na anatakiwa kuhakikisha kuwa bajeti hizi zinalenga katika kutatua matatizo ya wananchi vijijini na si kutenga fedha za mikutano, safari holela na kongamnao. Wote mtakumbuka jinsi alivyokuwa mkali mwishoni mwa mwaka jana kuhusu namna fedha zinavyopotea kwenye matumizi yasiyo na msingi. Wakati ni huu hana haja ya kusubiri kufanya 're-allocation' mwezi desemba, 09 au kutafuta kisingizio cha kutojua nini Wizara zimefanya. Hadi sasa hatujaona kama kuna serious thinking kuhusu hili.
Hoja ya pili kubwa inayonisukuma kuandika ni namna tunavyoendelea kugawana resources kupitia bajeti ya seriakali. Wote mnafahamu kuwa serikali inaendelea kupeleka shughuli/huduma kwenye ngazi za chini (D by D). Mfano inaimarisha elimu (ya msingi na sekondari) katika ngazi ya kijiji na kata. Kuna kundi kubwa la walimu wa sekondari ambao sasa wanapangiwa kufanya kazi kwenye sekondari za kata maarufu kama St. Kata. Tumeanza pia kujenga vituo vya afya kila kata na zahanati kila kijiji. Watumishi na huduma hizi zote zinatakiwa kusimamiwa na Sekretarieti za Mikoa zikishirikiana na Halmashauri za Wilaya. Hii ina maana kwamba kunatakiwa resources zaidi kwenye ngazi hiyo ya Mkoa na Halmashauri. Lakini ukiangalia Ceilings za bajeti ambazo Mikoa na Halmashauri imepewa unaweza kulia. Bado tumeendelea na traditional thinking ya kujaza fedha wizarani. karibu asilimia 80 ya fedha zote za uendeshaji imeachwa kwenye wizara na mikoa na Halmashauri imepewa asilimia 20 tu. Kwa hali ilivyo sasa na kwa kuzingatia ukumbwa wa mahitaji ya wananchi vijijini ilipaswa Wizara zibakie na asilimia 10 ya fedha zote zinazotengwa na asilimia inayosalia iende waliko wananchi, yaani vijijini. Kwa kufanya hivyo tungechochea kile 'wenzetu' wanachokiita kazi ziko kwenye kilimo. Ingawa hatuna hata kiwanda kimoja cha kuzalisha majembe ya mkono. UFI ilizikwa zamani.
Nimeona tuanzishe mjadala huu mapema kuwakumbusha viongozi wetu wa siasa hasa wabunge waaanze sasa kuingilia kati na si kusubiri kupiga mayowe mwezi juni. Kinachofanyika wakati uke wa bunge la bajeti kwa tunaofahamu mchakato wenyewe huwa ni usanii. Waheshimiwa wanatoa machozi ya kujisafisha kwa kushindwa kwao kujua ni wapi na wakati gani walipaswa kupiga kelele. Miongozo ya bajeti imetolewa kwenye kila wizara na kila Mkoa waitafute sasa ili wakabiliane na Waziri wa Fedha vizuri. Vinginevyo haya matatizo ya madai ya watumishi, nchi kukumbwa na njaa kila leo na umaskini uliokithiri hautatokomea.
Mwisho, inasaidia nini kuendesha kulundika fedha wizarani wakati Maafisa Tarafa, kata na Watendaji wa vijiji ambao ndio wahangaikaji wakuu kule kwenye grassroot wanatembea maili kwa maili kwa miguu au juu ya pikipiki wakipigwa mvua kuhamasisha maendeleo. Niliwahi kufika Ludewa na Makete Iringa. Na nilibahatika kutembelea tarafa ya Masasi iliyo kando ya ziwa nyasa na makao makuu yake ni Lupingu utawaonea huruma watumishi walioko kule. Kama si uzalendo wengi wangekwisha kimbia. Nilifika pia Kijombo kwenye tarafa ya Ukwama Makete. Milima na hali ya mvua kwa mwaka huwezi kumpa mtu pikipiki. Achilia mbali kule tunduru, Mpanda anakotoka PM, Kigoma na kwingineko. kama kweli akina Prof. Mwalyosi, Dr. Binilith Mahenge, Zitto kabwe, Anne Kilango mna uchungu wahini sasa.
Hoja ya pili kubwa inayonisukuma kuandika ni namna tunavyoendelea kugawana resources kupitia bajeti ya seriakali. Wote mnafahamu kuwa serikali inaendelea kupeleka shughuli/huduma kwenye ngazi za chini (D by D). Mfano inaimarisha elimu (ya msingi na sekondari) katika ngazi ya kijiji na kata. Kuna kundi kubwa la walimu wa sekondari ambao sasa wanapangiwa kufanya kazi kwenye sekondari za kata maarufu kama St. Kata. Tumeanza pia kujenga vituo vya afya kila kata na zahanati kila kijiji. Watumishi na huduma hizi zote zinatakiwa kusimamiwa na Sekretarieti za Mikoa zikishirikiana na Halmashauri za Wilaya. Hii ina maana kwamba kunatakiwa resources zaidi kwenye ngazi hiyo ya Mkoa na Halmashauri. Lakini ukiangalia Ceilings za bajeti ambazo Mikoa na Halmashauri imepewa unaweza kulia. Bado tumeendelea na traditional thinking ya kujaza fedha wizarani. karibu asilimia 80 ya fedha zote za uendeshaji imeachwa kwenye wizara na mikoa na Halmashauri imepewa asilimia 20 tu. Kwa hali ilivyo sasa na kwa kuzingatia ukumbwa wa mahitaji ya wananchi vijijini ilipaswa Wizara zibakie na asilimia 10 ya fedha zote zinazotengwa na asilimia inayosalia iende waliko wananchi, yaani vijijini. Kwa kufanya hivyo tungechochea kile 'wenzetu' wanachokiita kazi ziko kwenye kilimo. Ingawa hatuna hata kiwanda kimoja cha kuzalisha majembe ya mkono. UFI ilizikwa zamani.
Nimeona tuanzishe mjadala huu mapema kuwakumbusha viongozi wetu wa siasa hasa wabunge waaanze sasa kuingilia kati na si kusubiri kupiga mayowe mwezi juni. Kinachofanyika wakati uke wa bunge la bajeti kwa tunaofahamu mchakato wenyewe huwa ni usanii. Waheshimiwa wanatoa machozi ya kujisafisha kwa kushindwa kwao kujua ni wapi na wakati gani walipaswa kupiga kelele. Miongozo ya bajeti imetolewa kwenye kila wizara na kila Mkoa waitafute sasa ili wakabiliane na Waziri wa Fedha vizuri. Vinginevyo haya matatizo ya madai ya watumishi, nchi kukumbwa na njaa kila leo na umaskini uliokithiri hautatokomea.
Mwisho, inasaidia nini kuendesha kulundika fedha wizarani wakati Maafisa Tarafa, kata na Watendaji wa vijiji ambao ndio wahangaikaji wakuu kule kwenye grassroot wanatembea maili kwa maili kwa miguu au juu ya pikipiki wakipigwa mvua kuhamasisha maendeleo. Niliwahi kufika Ludewa na Makete Iringa. Na nilibahatika kutembelea tarafa ya Masasi iliyo kando ya ziwa nyasa na makao makuu yake ni Lupingu utawaonea huruma watumishi walioko kule. Kama si uzalendo wengi wangekwisha kimbia. Nilifika pia Kijombo kwenye tarafa ya Ukwama Makete. Milima na hali ya mvua kwa mwaka huwezi kumpa mtu pikipiki. Achilia mbali kule tunduru, Mpanda anakotoka PM, Kigoma na kwingineko. kama kweli akina Prof. Mwalyosi, Dr. Binilith Mahenge, Zitto kabwe, Anne Kilango mna uchungu wahini sasa.