Bajeti 2023-2024 yapendekeza kuongeza Tsh. 100 ya Ushuru wa Barabara kwa kila lita

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,107
49,808
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo June 15, 2023 amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 Bungeni Jijini Dodoma ambapo moja ya mambo aliyoyapendekeza kwenye hotuba yake ni kufanyika kwa marekebisho kwenye Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta, SURA 220 kwa kuongeza Ushuru wa Barabara na Mafuta kwa kiasi cha shilingi 100 kwa kila lita ya mafuta ya Petroli na Dizeli.

“Aidha, inapendekezwa pia kufanya marekebisho kwenye kifungu cha 4A cha Sheria ya Ushuru wa Barabara SURA, 220 kwa kuongeza kipengele ‘c’ kitakachoelekeza fedha zitakazokusanywa kutokana na ongezeko hili la ushuru wa barabara na mafuta la shilingi 100 kwa mafuta ya petroli na dizeli zitumike kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati iIi kupata vyanzo vya uhakika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Hatua hii inatarajia kuongeza Mapato ya Serikali kwa kiasi cha.."

-----

Nawakumbusha tuu kwamba Jerry Silaa alipendekeza tozo ya mafuta kwa Dar na bila shaka ndio hii hapa japo haijaelezwa kiundani ila hii itawahusi watu wa Dar.

Swali, kuna tozo ya mafuta ya Tsh. 100 ilianzishwa mwaka juzi, je, nini tofauti yake na hii?

My Take
Chonde chonde Serikali hii tozo mpya ya 100 ilipwe Dar Ili kuleta msawazo wa bei za mafuta na Mikoani.

Kama ikiwa ni kwa ajili ya Nchi nzima Wabunge kataeni.
 
Broo yameongezwa kodi siyo dar pekee, pia mimi sipo Dar naishi mkoani kama wewe
Ndio nakwambia tozo hiyo itakuwa structured Ili ilipwe Kwa Dar na sio Mikoani
 
Ndio nakwambia tozo hiyo itakuwa structured Ili ilipwe Kwa Dar na sio Mikoani
Jidanganye
 
Hawa jamaa huwa hawana maarifa zaidi ya kukimbilia kwenye mafuta pekee. shame government
Kupata kodi lazima uwekeze ila akili hiyo hawana, ndio maana wanakimbilia sekta kama mafuta au pombe maana kule ni rahisi kukusanya bila kuwekeza chochote, wangewekeza kwenye utalii kule kuna billions za kutosha budget nzima ya nchi ila akili zao ndio zimeishia hapo tuu na hawataki kazi ngumu
 
Nawakumbusha tuu kwamba Jerry Silaa alipendekeza tozo ya mafuta Kwa Dar na bila shaka ndio hii hapa japo haijaelezwa kiundani ila hii itawahusi watu wa Dar..

Swali,Kuna tozo ya mafuta ya sh.100 ilianzishwa mwaka juzi,Je nini tofauti yake na hii?



My Take
Chonde chonde Serikali hii tozo Mpya ya 100 ilipwe Dar Ili kuleta msawazo wa bei za mafuta na Mikoani..

Kama ikiwa ni Kwa Ajili ya Nchi nzima Wabunge kataeni.

Mbunge gani anauwezo wa kukataa...🤔
 
Kupata kodi lazima uwekeze ila akili hiyo hawana, ndio maana wanakimbilia sekta kama mafuta au pombe maana kule ni rahisi kukusanya bila kuwekeza chochote, wangewekeza kwenye utalii kule kuna billions za kutosha budget nzima ya nchi ila akili zao ndio zimeishia hapo tuu na hawataki kazi ngumu
Budget zinyewe zinaandaliwa na ma-PS yeye kazi yake ni kwenda tu kusoma bungeni wala hajui kilichoandikwa kwa undani, ukipewa documents yote utakuta kuna miaka ya nyumba sababu ni copy and paste.
 
Kweli kabisa na bunge liuzwe kuliko bandari na kupandishiwa kodi zizizo halali...
Eeh
20230607_101715.jpg
 
Back
Top Bottom