Richard Robert
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 632
- 340
Mienzi minne baada ya mwenyekiti wa CHADEMA wilaya Bagamoyo kutekwa na kuteswa na wanaCCM Oktoba mwaka jana wakati wa uchaguzi wa kata ya magomeni. UBABE umeendelea kutumika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda kila CHAGUZI!... Hali hii imepelekea vurugu kubwa kuzuka katika kijiji cha kidomole!...
Hali hii inatokana na msimamo wa CCM kuhakikisha kwa namna yoyote CHADEMA haichukui nafasi yoyote ya kuongoza eneo la BAGAMOYO kwa madai kuwa ni aibu kwa WAKUBWA!...
Utamaduni wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukamia kila uchaguzi mpaka chaguzi za vijiji na vitongoji umeleta kizaa zaa katika kijiji cha kidomole mchana wa leo!...
Kidomole ni moja ya vijiji 7 vya jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo ambavyo uchaguzi wa viongozi wa vijiji na vitongoji vyake umefanyika leo.
Kwa wiki tatu mfululizo uongozi wa CHADEMA mkoa wa pwani, wilaya ya Bagamoyo, jimbo la Chalinze na kata husika uliwekeza nguvu kubwa kuwakikisha ushindi unapatikana.
Hali hii iliishitua CCM na kumwaga pesa na makada kwa siku 2 za mwisho ambao wamekuwa wakizunguka nyumba kwa nyumba nyakati za usiku kushawishi wapiga kura wawapigie. Viongozi wa serikali na yule kijana tajiri kuliko wote TANZANIA walitia timu jana na juzi.
CCM iliamua kuwekeza nguvu kubwa kidomole ambako kuna migogoro mikubwa ya ardhi iliyowafanya viongozi na wananchi kuvunja uongozi na kuhamia CHADEMA april mwaka jana. Hivyo CCM iliamua kuhakikisha CDM haipiti.
Leo uchaguzi umeanza saa 2 asubuhi kukiwa na majina ya wagombea wa CCM pekee vituoni - ya wagombea wa CHADEMA yakiwa yamefichwa na wasimamizi wa uchaguzi. CCM walionekana wakiwazuia wafuasi wa CHADEMA KUPIGA KURA na vikosi vya katibu mwenezi wa CCM aitwaye BOLIZOZO au ZOZO kwa ufupi vikiwasaidia wanaCCM kupiga kura mara nne nne!!.
Wana CDM walipopinga hali hii waligeuziwa kibao na kuanza kupigwa kwa fimbo, mawe na mapanga. Wanachadema wengi wameumizwa ingawa hawapo katika hali mbaya. CCM walionekana kuwa wajiandaa kwa silaha.
Hivi sasa viongozi watatu wa CHADEMA wamekamatwa na wanaCCM polisi wamekuja kuwachukua. Mwenyekiti wa CHALINZE Torongey mpaka sasa yuko kituo cha polisi BAGAMOYO.
Source: Mimi - Katibu Mwenezi wa CHADEMA BAGAMOYO.
Hali hii inatokana na msimamo wa CCM kuhakikisha kwa namna yoyote CHADEMA haichukui nafasi yoyote ya kuongoza eneo la BAGAMOYO kwa madai kuwa ni aibu kwa WAKUBWA!...
Utamaduni wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukamia kila uchaguzi mpaka chaguzi za vijiji na vitongoji umeleta kizaa zaa katika kijiji cha kidomole mchana wa leo!...
Kidomole ni moja ya vijiji 7 vya jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo ambavyo uchaguzi wa viongozi wa vijiji na vitongoji vyake umefanyika leo.
Kwa wiki tatu mfululizo uongozi wa CHADEMA mkoa wa pwani, wilaya ya Bagamoyo, jimbo la Chalinze na kata husika uliwekeza nguvu kubwa kuwakikisha ushindi unapatikana.
Hali hii iliishitua CCM na kumwaga pesa na makada kwa siku 2 za mwisho ambao wamekuwa wakizunguka nyumba kwa nyumba nyakati za usiku kushawishi wapiga kura wawapigie. Viongozi wa serikali na yule kijana tajiri kuliko wote TANZANIA walitia timu jana na juzi.
CCM iliamua kuwekeza nguvu kubwa kidomole ambako kuna migogoro mikubwa ya ardhi iliyowafanya viongozi na wananchi kuvunja uongozi na kuhamia CHADEMA april mwaka jana. Hivyo CCM iliamua kuhakikisha CDM haipiti.
Leo uchaguzi umeanza saa 2 asubuhi kukiwa na majina ya wagombea wa CCM pekee vituoni - ya wagombea wa CHADEMA yakiwa yamefichwa na wasimamizi wa uchaguzi. CCM walionekana wakiwazuia wafuasi wa CHADEMA KUPIGA KURA na vikosi vya katibu mwenezi wa CCM aitwaye BOLIZOZO au ZOZO kwa ufupi vikiwasaidia wanaCCM kupiga kura mara nne nne!!.
Wana CDM walipopinga hali hii waligeuziwa kibao na kuanza kupigwa kwa fimbo, mawe na mapanga. Wanachadema wengi wameumizwa ingawa hawapo katika hali mbaya. CCM walionekana kuwa wajiandaa kwa silaha.
Hivi sasa viongozi watatu wa CHADEMA wamekamatwa na wanaCCM polisi wamekuja kuwachukua. Mwenyekiti wa CHALINZE Torongey mpaka sasa yuko kituo cha polisi BAGAMOYO.
Source: Mimi - Katibu Mwenezi wa CHADEMA BAGAMOYO.