Bagamoyo kwalipuka tena - ni CCM vs CHADEMA

Bagamoyo kwalipuka tena - ni CCM vs CHADEMA

Mbinu hii chafu ya ccm ndo imesaidia kufanyika mageuzi ya kweli nchini kenya.
Mienzi minne baada
ya mwenyekiti wa CHADEMA wilaya Bagamoyo kutekwa na kuteswa na wanaCCM
Oktoba mwaka jana wakati wa uchaguzi wa kata ya magomeni. UBABE
umeendelea kutumika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda kila CHAGUZI!...
Hali hii imepelekea vurugu kubwa kuzuka katika kijiji cha kidomole!...

Hali hii inatokana na msimamo wa CCM kuhakikisha kwa namna yoyote
CHADEMA haichukui nafasi yoyote ya kuongoza eneo la BAGAMOYO kwa madai
kuwa ni aibu kwa WAKUBWA!...

Utamaduni wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukamia kila
uchaguzi mpaka chaguzi za vijiji na vitongoji umeleta kizaa zaa katika
kijiji cha kidomole mchana wa leo!...

Kidomole ni moja ya vijiji 7 vya jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo
ambavyo uchaguzi wa viongozi wa vijiji na vitongoji vyake umefanyika
leo.

Kwa wiki tatu mfululizo uongozi wa CHADEMA mkoa wa pwani, wilaya ya
Bagamoyo, jimbo la Chalinze na kata husika uliwekeza nguvu kubwa
kuwakikisha ushindi unapatikana.

Hali hii iliishitua CCM na kumwaga pesa na makada kwa siku 2 za mwisho
ambao wamekuwa wakizunguka nyumba kwa nyumba nyakati za usiku kushawishi
wapiga kura wawapigie. Viongozi wa serikali na yule kijana tajiri
kuliko wote TANZANIA walitia timu jana na juzi.

CCM iliamua kuwekeza nguvu kubwa kidomole ambako kuna migogoro mikubwa
ya ardhi iliyowafanya viongozi na wananchi kuvunja uongozi na kuhamia
CHADEMA april mwaka jana. Hivyo CCM iliamua kuhakikisha CDM haipiti.

Leo uchaguzi umeanza saa 2 asubuhi kukiwa na majina ya wagombea wa CCM
pekee vituoni - ya wagombea wa CHADEMA yakiwa yamefichwa na wasimamizi
wa uchaguzi. CCM walionekana wakiwazuia wafuasi wa CHADEMA KUPIGA KURA
na vikosi vya katibu mwenezi wa CCM aitwaye BOLIZOZO au ZOZO kwa ufupi
vikiwasaidia wanaCCM kupiga kura mara nne nne!!.

Wana CDM walipopinga hali hii waligeuziwa kibao na kuanza kupigwa kwa
fimbo, mawe na mapanga. Wanachadema wengi wameumizwa ingawa hawapo
katika hali mbaya. CCM walionekana kuwa wajiandaa kwa silaha.

Hivi sasa viongozi watatu wa CHADEMA wamekamatwa na wanaCCM polisi
wamekuja kuwachukua. Mwenyekiti wa CHALINZE Torongey mpaka sasa yuko
kituo cha polisi BAGAMOYO.

Source: Mimi - Katibu Mwenezi wa CHADEMA BAGAMOYO.
 
kitego cha usalama chadema hovyo kabisa..ccm nijuavyo mimi imejaa vizee vijana wengi wako chadema labda watoto wa nabalozi wa nyumba kumi kumi kwanini tusi watumia hazina kubwa tuliyo nayo tumebaki kulia lia tu..Mbowe alisema Arumeru watalalamika wao na kweli wali lalamika wao kwanini tusi fanye hivyo chaguzi zote..

Kaka CDM iko imara dhidi ya hujuma hizo!.. Uwezo wa kufanya mambo tunao!... Kwanza tujenge chama. Kinachofanyika ARUSHA SI LAZIMA KIFANYIKE BAGAMOYO mazingira ni tofauti na utamaduni ni tofauti!...
 
We got small axe,sharp and ready to cut CCM down.Waache waluke sarakasi zao zote but one day.we will cut them down!!!!
 
Pasco, Mimi ni katibu mwenezi wa CHADEMA Bagamoyo. Najua hofu yako ni UDINI. Ni kweli UDINI umepandikizwa saanaa na CCM!!.. Lakini tumefanya kazi saana na sasa mambo ni mazuri. Nakuomba ukija Bagamoyo unitafute.
wafuasi wa chadema bwana ni kama chura wanajaribishiwa sumu kama inauwa na viongozi wao
 
chadema kwa fujo hamuogopi mamlaka na kutii sheria bila shuruti wakipewa kipondo utasikia tunaonewa na ccm

Mwanaume ukikubali kutumiwa ki-fikra ni dhahiri waweza tumiwa kimwili. Pole sana kwani mwisho wa siku wakishamaliza kukutumia watakutupa kama toilet paper. Vipi mkuu siku hizi huonekani Kibaha au ndo umehamia Lumumba?
 
Hamna mahaali hapataenda upinzani wacha watumie nguvu muda wao umeisha siku nyingi
 
Mienzi minne baada ya mwenyekiti wa CHADEMA wilaya Bagamoyo kutekwa na kuteswa na wanaCCM Oktoba mwaka jana wakati wa uchaguzi wa kata ya magomeni. UBABE umeendelea kutumika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda kila CHAGUZI!... Hali hii imepelekea vurugu kubwa kuzuka katika kijiji cha kidomole!...

Hali hii inatokana na msimamo wa CCM kuhakikisha kwa namna yoyote CHADEMA haichukui nafasi yoyote ya kuongoza eneo la BAGAMOYO kwa madai kuwa ni aibu kwa WAKUBWA!...

Utamaduni wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukamia kila uchaguzi mpaka chaguzi za vijiji na vitongoji umeleta kizaa zaa katika kijiji cha kidomole mchana wa leo!...

Kidomole ni moja ya vijiji 7 vya jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo ambavyo uchaguzi wa viongozi wa vijiji na vitongoji vyake umefanyika leo.

Kwa wiki tatu mfululizo uongozi wa CHADEMA mkoa wa pwani, wilaya ya Bagamoyo, jimbo la Chalinze na kata husika uliwekeza nguvu kubwa kuwakikisha ushindi unapatikana.

Hali hii iliishitua CCM na kumwaga pesa na makada kwa siku 2 za mwisho ambao wamekuwa wakizunguka nyumba kwa nyumba nyakati za usiku kushawishi wapiga kura wawapigie. Viongozi wa serikali na yule kijana tajiri kuliko wote TANZANIA walitia timu jana na juzi.

CCM iliamua kuwekeza nguvu kubwa kidomole ambako kuna migogoro mikubwa ya ardhi iliyowafanya viongozi na wananchi kuvunja uongozi na kuhamia CHADEMA april mwaka jana. Hivyo CCM iliamua kuhakikisha CDM haipiti.

Leo uchaguzi umeanza saa 2 asubuhi kukiwa na majina ya wagombea wa CCM pekee vituoni - ya wagombea wa CHADEMA yakiwa yamefichwa na wasimamizi wa uchaguzi. CCM walionekana wakiwazuia wafuasi wa CHADEMA KUPIGA KURA na vikosi vya katibu mwenezi wa CCM aitwaye BOLIZOZO au ZOZO kwa ufupi vikiwasaidia wanaCCM kupiga kura mara nne nne!!.

Wana CDM walipopinga hali hii waligeuziwa kibao na kuanza kupigwa kwa fimbo, mawe na mapanga. Wanachadema wengi wameumizwa ingawa hawapo katika hali mbaya. CCM walionekana kuwa wajiandaa kwa silaha.

Hivi sasa viongozi watatu wa CHADEMA wamekamatwa na wanaCCM polisi wamekuja kuwachukua. Mwenyekiti wa CHALINZE Torongey mpaka sasa yuko kituo cha polisi BAGAMOYO.

Source: Mimi - Katibu Mwenezi wa CHADEMA BAGAMOYO.

Mkuu kwa nini hamkuomba msaada wa red brigade makao makuu mapema? hapo tushaliwa tena...
 
chadema kwa fujo hamuogopi mamlaka na kutii sheria bila shuruti wakipewa kipondo utasikia tunaonewa na ccm
Bro wewe ndo unahusika na masuala ya simu??? Hivi umeisoma hiyo habari?? Mbona kama unatoka usingizin na kuanza kucomment bila kusoma??? Ni dhahiri hapo CDM wameonewa tena haikuhitaj kusoma had la saba kujua hilo. Acha ushabiki, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Ndugu zangu wanachadema wakati wa ukombozi umeisha fika,hapa ndipo tunapo takiwa kuwa pamoja katika nyakati ngumu kama hizi.Hatutakiwi kukata tamaa bali kupigania haki zetu mpaka mwisho,maana tukiogopa watachukua kila kitu kwa kututisha.Nawapa pole makamanda wote mlio umizwa kwa kupigania ukombozi na mungu wetu ni mwema na atakuwa nasi sasa na hata wakati mgumu wowote ulio mbele yetu. Kwa mwenye akili anajua tu kuwa mfa maji haachi kutapatapa,CCM imeisha kufa bado tu kuizika.MAKAMANDA MSICHOKE KUPIGANIA UKOMBOZI.PEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEOOOOOOOOOOOOOPLE'S POWER
 
Hii ndiyo sura ya kweli ya CCM. Wako tayari kuua ili wabaki kwenye madaraka, na wameshaua sana. Evil begets evil; wanajua sasa wakiondoka madarakani wanaweza kufikishwa hata ICC. Damu za Mwangosi na Watanzania wengine waliouawa na CCM na Polisi wake zinawalilia.

Kazi inayowakabili Watanzania ni kubwa sana. Ni kazi ya kumwondoa mkoloni mbaya kuliko Mwingereza. Mwingereza hakujaribu kuuwa ili abaki madarakani. Mwingereza alisimamia uchaguzi huru hapa kwetu.

CCM watatoka tu. Kiasi watakavyojaribu kuleta nyokonyoko zaidi ni kiasi hicho hicho wanajipeleka zaidi kwa Pilato baada ya ukombozi.

Ni muhimu CDM kuwa na Idara ya Archives itakayoweka picha na documents za uhujumu wa CCM, na vile vile picha za mikutano kama ule wa Mbeya. Kuweko kwa Archivist CDM ni muhimu mno. We are witnessing the rebirth of a nation. That I submit, is worth documenting,
 
chadema kwa fujo hamuogopi mamlaka na kutii sheria bila shuruti wakipewa kipondo utasikia tunaonewa na ccm
hivi kichwa chako kina ubongo au kamasi hivi umeisoma thread nzima au wewe ni mfuasi wa mr. cameroun
 
Back
Top Bottom