Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Nafikiri ni wazo zuri sana kujenga airport Bagamoyo. Statistics zinaonyesha Dar airport inaelemewa sana na traffic ya midege inayotua kila dakika. Hata ikipanuliwa hivi inavyotakiwa kupanuliwa bado haitaweza kuhimili. Tunahitaji specifically airport mpya bagamoyo kwa sababu ya urahisi wa bagamoyo road kuingia dar. Barabara ni pana sana, haina magari mengi hasa kutokea Tegeta-Mbezi Beach-Ali H Mwinyi hadi city centre; barabara iko idle kabisa, pana ya kutosha magari yanaenda full speed. Bandari pia itajengwa Bagamoyo kwa sababu hiyo hiyo ya urahisi wa barabara kuingia Dar. Mizigo mingi zaidi itashukia kule italetwa na magari fasta jijini. Yaani serikali hii ina mawazo endelevu mazuri sana.
Mkuu,
Umenivunja MBAVU. Mwanzo nilikuwa nashangaa huyu jamaa kaandika MADUDU gani? Nilivyokusoma katikati ya mistari nimekupata mkuu wangu. Ni Limbukeni tu anaweza kwenda kujenga uwanja wa ndege Bagamoyo na kutegemea watu watumie kuingia mjini Dar. Kama ile barabara ya Bagamoyo kwa sasa imeshafurika, ukiongeza na watu wanaoenda Bagamoyo? Pia huko ni mbali saana. Itabidi mtu uondoke masaa 5 kabla kama una ndege za jioni.
Nchi nyingi wakijenga viwanja kama hivi basi wanaweza vitu kama Metro au Matrain ya speed kali ili kufikisha watu mjini haraka. Sasa sisi tutabanana wote kwenye hicho kibarabara? Pale ulipo wa sasa ni safi sana ila sema walijisahau kujenga HIGHWAYS walau mbili kuja pale Airport ambazo zinauzunguka mji kutoka Kivukoni hadi Mbezi beach/Tegeta.
Nyie mbona hamtaki kueleze ukweli
hivi vyote vingejengwa Moshi au Arusha ingeonekana its normal
wacha wajenge Bagamoyo wakimaliza wakajenge na ule mradi mkubwa zaidi kule Pemba
sioni tatizo liko wapi
Mkuu GT,
Ili uyafahamu haya mambo, inabidi usome Traffic Engineering na UCHUMI. T.Eng. nimeshasema mara nyingi ni somo ambalo si tu usome na ufaulu ndiyo uwe Mhandisi, inatakiwa UZOEFU. Kutokana na Mkuu Moran75, hawa watu Tanzania wapo wachache sana ambao wengi ni wamesoma na hafanyi kazi kwenye hizo field.
Sasa Mkuu, hii kitu inahitaji kuipa heshima na kuwaacha wataalamu wafanye kazi. Yaleyale ya TANESCO.
Amini usiamini, ndege zote zitakazotaka kutua Bagamoyo zitakuwa na shida sana kupata WASAFIRI kwani wengi watataka kutua DIA. Historia dunia nzima inaonyesha hivyo. Hakuna atakayekuwa tayari kwenda mbali namna hiyo kupanda pipa labda kama hana njia nyingine. Hicho kiwanja kitakufa natural death na atabaki anakitumia yeye na wanae.