Bado ufugaji wa bata unadharauliwa sana

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
7,789
8,915
Bata wako under rated sana ila ni project ambayo mtu anaweza tengeneza pesa ndefu sana tena mno. Wengi tunakomaa na kuku nakujikuta Market share ndi ndogo sana.

Mayai ya Bata ndio hutumika kwenye Bekar, sema kwa sababu hayapo basi yanatumika ya kuku ila yangejuwepo hakuba mtu mwenye Bekar angetumia mayai ya kuku.

Wahindi, Wachina na Wazungu , ukiwawekea mayai ya Bata ba Kuku wata opt mayai ya Bata, mayai ya Bata ni bora zaidi ya kuku na soko kubwa linaweza kuwa kwemye Super market kubwa hizi.

Hakuna Super Market hata moja yenye mayai ya kuku na si kwamba hawataki kuyauza haoana ni hayapo, na yangekywepo yangekuwa yanaisha kabla ya mayai ya kuku.

Na mayai ya Bata si lazima hawa wa kizun gu hapana hata hawa wa Kiswahili na unacho weza kufanya ni kuwafuga kwa wingi sana ili uweze kupta mayai ya kutosha na nina sema kwa wingi kwa sababu wanavyo taga kuna wakati watasimama kwa ajili ya kutaka kuatamia hivyo wakiwa wemgi gap hutaliona.

Pia unaweza ondoa jogoo ukabakia na majike tupu, ili wanapo taga yanakuwa ni kwa ajili ta kula pekee.

Sijazungumzia nyama yake ambayo kwa sokoni wanapendelea bata wakiqa wachanga na miezi mitatu, nyama ikiwa bado laini.

Ukiwa na shamba kubwa na bwawa la wao kuogelea na majani ya kutosha basi ufugaji wa Bata ni mzuri sana na haina haja wote kukomaaa na kuku na mwisho kuanza kurogana.

Kuna Dada huku Arusha alipewa tenda taani anahangaika hadi basi imebidi aachie Dili make kila anapo enda unakuta mtu ana bata wanne watano, mayai 10.
 
Mkuu nilishawahi kufuga bata mwaka 2017 na 2018 walifika hadi 100 ila nilikosa soko nikaishia kuwagawa na wengi kuuza kwa bei ndogo sana !
Hata sasa ninaweza kuwafuga tena Kama soko lipo naishi dar kiluvya gogoni .eneo lipo kubwa la kuwafugia

0755404226 tafadhali niunganishe na soko
 
Mkuu nilishawahi kufuga bata mwaka 2017 na 2018 walifika hadi 100 ila nilikosa soko nikaishia kuwagawa na wengi kuuza kwa bei ndogo sana !
Hata sasa ninaweza kuwafuga tena Kama soko lipo naishi dar kiluvya gogoni .eneo lipo kubwa la kuwafugia

0755404226 tafadhali niunganishe na soko
Nitakutafuta tuyajenge ndugu nami nafikiria kuanza wafuga hawa bata.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom