Passion Lady
JF-Expert Member
- Nov 17, 2012
- 8,694
- 4,646
Salaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaam
Ndugu zangu Tarehe 6 April nitakuwa nikifunga pingu za maisha ( naoa).
Bado siku tisa tu nitakuwa na familia yangu
Bado siku tisa tu ambazo huyo muolewaji ataitwa Mrs
Ni hatua nzuri nafahamu, lkn maswali lukuki najiuliza
Chonde chonde
Kwa wale mlio pitia hii hatua naomba usia wenu
Uliwezaji kusahau machungu ya kutomkuta sealed?!
Nakupatia mistari hii, ni mizuri sana na ni changamoto kwa wengine, MANI, zumbemkuu, saudari karibieni hapa niwapige Neno. Neno hili linatoka Mhubiri 4:7-
Kisha nikarudi tena, na kuona ubatili chini ya jua.4.8 Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa.
4.9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
4.10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
4.11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
4.12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.
Sali sana. Mwenyezi Mungu mwenye rehema nyingi akuongoze kwa kila jambo.
Bado siku kenda uache kwenda club...
Bado siku kenda uache kulala na pensi
Bado siku kenda ratiba yako ya kijiweni iharibiwe vibaya
Bado siku kenda kabla hujaingia jela
Bado siku kenda uanze kupandwa vipresha kama unamrizisha
Bado siku kenda uanze kutoa ela ya mboga home
Bado siku kenda ukome kulala nje na home bila 'ruhusa'
Bado siku kenda washkaji zako ambao hawajaoa kukutenga
Bado siku kenda uanze kunyemelea nyumba ndogo
Bado siku kenda uache uasherati na uanze uzinzi
Bado siku kenda uwe na siku za kwenda kazini ukiwa umekasirika
Bado siku kenda uanze kuwaza kama mkeo anaibwa
BADO SIKU KENDA KABLA MUVI YA MAISHA YAKO KUANZA PART 2...
karibu huku kijiweni na kila la heri...
Salaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaam
Ndugu zangu Tarehe 6 April nitakuwa nikifunga pingu za maisha ( naoa).
Bado siku tisa tu nitakuwa na familia yangu
Bado siku tisa tu ambazo huyo muolewaji ataitwa Mrs
Ni hatua nzuri nafahamu, lkn maswali lukuki najiuliza
Chonde chonde
Kwa wale mlio pitia hii hatua naomba usia wenu